Hii kitu kiujumla inaitwa 'deregulation of electricity market', ni kitu kimefanyika nchi nyingi na kinaendelea kufanyika. Dhana ya mfumo huu ni kwamba shughuli za umeme (uzalishaji, usambazaji na uuzaji umeme) ni ngumu (complex) kiasi kwamba zinapofanywa na kampuni moja (e.g.TANESCO) kunakuwa hakuna ufanisi. Hivyo shughuli hizi zikigawanywa na kupewa makampuni mbalimbali basi kutakuwa na ushindani utakaopelekea kuwepo huduma bora na ufanisi
Mfano mzuri ni sekta ya mawasiliano ya simu (telecommunications). Utakuwa unakumbuka enzi za TTCL ambapo hata ukiwahonga wanaweza wasikuunganishie simu nymbani kwako. Hakukuwa na huduma nzuri kwa wateja-bili za kubambikiza, n.k. Baada ya 'deragulation', sasa tunapata dakika kumi na tano kwa shilingi 500.
Sasa katika kujibu swali lako, sekta ya umeme iko tofauti kidogo na sekta nyingine. Kama unafanya deregulation, lazima uhakikishe hakuna kampuni ina nguvu kubwa kupita kiasi katika soko, maana itazuia ushindani na inaweza hata kupandisha bei ya umeme kwa 'kutengeneza uhaba wa umeme' ambao kimsingi haupo ili kufanya bei ziwe juu. Nchi zote zinazofanya deregution ya umeme moja ya masharti zinazoyafuata ni kubinafsisha makampuni yenye monopoly. So kuuzwa kwa Tanesco ni kuzuia kitu inaitwa 'Market Power'. Ndo kusema Tanesco itatakiwa ibakiwe na kazi ya kujenga na 'kupangisha' transmission and distribution lines tu. Kutakuwa na makampuni ya uzalishaji umeme ya binafsi (tayari yapo-IPTL,Songas), makampuni ya kuuza umeme na kampuni moja ya umma ya kukodisha na kujenga transmission lines. Kenya hili wameshalifanya.
Kiujumla hili ni suala ya kulifanya kwa ueledi na uaminifu mkubwa maana kuna ujanja ujanja mwingi unaweza kukwamisha mambo kama ilivyotokea California, USA. Kuna wajanja watabuku transmission lines ili kuwazuia wengine wasipitishe umeme wao na hivyo kuzuia wengine wasifanye biashara. Kuna wengine watajifanya wanazifanyia plants zao matengenezo kumbe wanataka kutengeneza uhaba wa umeme ili bei iwe ya kuruka.
Mwisho, kama alivyosema mdau, hili wazo lipo zaido ya miaka 10 iliyopita, lilikosa fedha za utekelezaji tu.