Anayoyasema Muhongo katumwa na Magufuli?

Anayoyasema Muhongo katumwa na Magufuli?

Mzimu wa Muhongo unawasumbua kwelikweli tueleze ni wapi na lini muhongo katamka kkwamba tanesco haitazalisha umeme??? Kinachosisitizwa na jembe hili ni wawekezaji binafsi pia kuzalisha umeme ili uwe wa kutosha na si kutegemea tanesco pekee. Kukiwa na mgawo wa umeme mnalalamika monopoly ya tanesco, watu wakialikwa kuzalisha umeme zaidi mnalalamika ooohhh tanesco inanyang'anywa jukumu lake. Acheni jembe lifanye kazi hizi cheap politics hazitawasaidia
Usilolijua......unanisikitisha sana, kama unadhan mtoa post katoa kwa kwa bahati mbaya basi subiria matokeo
 
Kwa ajili ya usalama wa nchi, sector ingebaki mikononi mwa serikali. Nchi nyingi ambazo ni developed ndiyo sera yao. Au angalau kampuni ya nchi husika sio ya nje
Kwa ajili ya usalama wa nchi ndio maana usambazaji unaachwa mikononi mwa TANESCO!
 
Miaka 50 sasa; huo umeme wanaozalisha uko wapi ukiacha ule wa maji?! Mara zote inapotokea dharula ya umeme TANESCO wameshawahi kuwa na uwezo ku-accommodate hiyo dharula zaidi ya kurudi kwenye sekta binafsi? Sasa kwanini tusubirie dharula kisha tuje na project za zima taa kama zile ya IPTL na Richmond?! Na ndio maana nikauliza; je tumejiridhisha ikiwa TANESCO wanao uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha ambao haitajalisha kwamba kuna ukame mwaka mzima au mvua mwaka mzima... bado umeme unaozalishewa na TANESCO uwe na uwezo wa kuhudumia wataje wake!

Kwamba WHY NOW, tayari nimeshakuambia kwamba huu mpango sio wa sasa/mpya unless kama unauliza why uwe implemented now! Huu mpango una miaka sasa na idea ya kuifanya TANESCO iwe kampuni 3 tofauti ina zaidi ya miaka 5 hivi sasa. Hata Muhongo alipochaguliwa kwa mara ya kwanza na JK, aliukuta huu mpango-- alichofanya yeye ni kuu-speep up.

Suala la generation kuwa kwenye sekta binafsi ni kuifanya TANESCO ifanye investment ya resources zake kwenye usambazaji badala ya kufanya kila kitu-- uzalishaji, usafirishaji na hadi usambazaji ni hao hao! Wadau wamejiridhisha kwamba kuwa na multiple functions ambazo zote zinahitaji resources za kutosha ni moja ya sababu ya kuifanya TANESCO ikose efficiency! Na hili halina mjadala manake linaonekana hata kwa jicho moja. Ikizima mashine moja tu; watu tunaingia gizani kwa sababu tayari tunakuwa na upungufu!Na huko kwenye uzalishaji ndo kwenye changamoto zaidi kwa TANESCO kwa kuwa kunahitaji mtaji wa kutosha!

Sasa hapo ni lazima uchague! Ama iachwe TANESCO iendelee na mwendo wake wa kusuasua... ukija ukame mnaanza kuitisha zabuni za zima taa au uruhusu sekta binafsi iingie rasmi! Ukisema sekta binafsi iingie na TANESCO iendelee kuzalisha umeme; sekta binafsi itasita kuingia kwenye game kwa kuchelea kuwa na competitor ambae ni shirika la serikali huku akiwa pia ndo mdau mwenyewe!




Hivi unaelewa hata tunacho andika humu?
au uko kwa kazi ya kumtetea Muhongo?

Hakuna anaepinga wawekezaji kufanya generation lakini why wachukue generation ya Tanesco?

why wasianzishe za kwao?

Umeme wa dharula haujui kuwa ilikuwa ni dili la kupangwa?
hujui kweli au unajifanya hujui?
 
Usilolijua......unanisikitisha sana, kama unadhan mtoa post katoa kwa kwa bahati mbaya basi subiria matokeo
Na mimi naishi nchi hii na kufuatilia masuala ya nishati nimeomba andishi lolote, video au sauti ya muhongo alipoyatamka hayo maneno. Na wewe unanisikitisha sana kwa kuamini habari bila ushahidi wowote, kivuli cha profesa kinawasumbua sana
 
Na mimi naishi nchi hii na kufuatilia masuala ya nishati nimeomba andishi lolote, video au sauti ya muhongo alipoyatamka hayo maneno. Na wewe unanisikitisha sana kwa kuamini habari bila ushahidi wowote, kivuli cha profesa kinawasumbua sana
Kwa kuwa umetaja neno siasa sitoweza ongea mambo ya kisiasa ila utaelewa soon tu
 
Na wewe utaelewa tu kila mtu asubir
Sawa mkuu, japo naweza sema mimi nilishaelewa kabla hata ya uchaguzi. Hii issue ilitaka ifanyike tangu 2015 katikati mikakati ilishaanza kuna kimbembe kilitokea ikawa ngumu kumeza ikapigwa pending mpaka 2017 bahati mbaya mwenye mkakati akaingia ktk kashfa akakaa pembeni workers wakafurahi kidogo, sasa baada ya uchaguzi kabla ya kutangazwa mawaziri lilitokea neno moja linaitwa 2020 ndipo mpango ufanyike sasa baada ya mawaziri kutangazwa si ndio karudi yule yule so haieleweki bado kichwani mwake kuna neno 2017 au kichwa kimekua updated to 2020. Stay tune
 
Kwa ajili ya usalama wa nchi, sector ingebaki mikononi mwa serikali. Nchi nyingi ambazo ni developed ndiyo sera yao. Au angalau kampuni ya nchi husika sio ya nje
Kwa ajili ya usalama wa nchi ndio maana usambazaji unaachwa mikononi mwa TANESCO!
Hivi unaelewa hata tunacho andika humu?
au uko kwa kazi ya kumtetea Muhongo?

Hakuna anaepinga wawekezaji kufanya generation lakini why wachukue generation ya Tanesco?

why wasianzishe za kwao?

Umeme wa dharula haujui kuwa ilikuwa ni dili la kupangwa?
hujui kweli au unajifanya hujui?
Nimtetee Muhongo kwa misingi ipi? Maswali ambayo nimekuuliza hakuna hata moja ambalo umejibu! By the way, unapohoji kwanini wasianzishe za kwao; unamaanisha nini hasa? Kwani Songas leo hii wanapozalisha umeme si kwamba wameanzisha za kwao? Kwani Aggreko wanapozalisha umeme leo hii unadhani wanatumia mitambo ya TANESCO? Ikiwa kampuni X inazalisha umeme ni kwamba from the grassroots wanachoanzisha ni cha kwao! Ikiwa wanataka kuzalisha umeme wa mafuta... watalazimika kununua majenereta ya kuzalishia umeme na watalazimika kuagiza mafuta kwa ajili hiyo! The same apply kwa watakaokuwa wanazalisha kwa gas, upepo, maji n.k! Sasa ni nini hicho unachosema kwanini wasianzishe cha kwao?

Halafu unapohoji "kwanini wachukue generation ya TANESCO" unamaanisha nini hasa? Nina mashaka wewe ndo hujaelewa vinginevyo ni generation ya TANESCO ipi unayosema wanataka kuchukua? Kwani IPTL, Songas, Aggreko, Symbion wamechukua generation ya TANESCO?

Kwamba umeme wa dharula ulikuwa deal la kupangwa! Ina maana ule ukame wa 1991 ambao ulipelekea IPTL ulikuwa ni wa kupangwa? Ina maana ile 2007/2008 hakukuwa na matatizo ya umeme? Kinachopangwa ni upatikanaji wa hao wazalishaji lakini ukisema kwamba hata ile dharula ni ya kupanga wakati unafahamu kabisa kwamba wakati ule tulikuwa tunatgemea chanzo kimoja tu cha maji basi sidhani kama huu mjadala utafika mwisho
 
Kuna vitu viwili ambavyo kwa maoni yangu serikali isingeachia sekta binafsi ivitawale. Kimoja ni uzalishaji na usambazaji wa nishati ya umeme na cha pili ni uagizaji na uuzaji wa nishati ya mafuta. Hivi ni vitu vya muhimu sana kwa uchumi na usalama wa nchi na nadhani ni kosa kuiachia sekta binafsi. Nilikuwa nangoja nisikie wakisema kuwa wanafufua kiwanda cha uchakataji wa mafuta ghafi-TIPER- ambapo serikali ingeagiza na kuchakata mafuta hayo humu nchini. Bei ya mafuta ingepungua sana na serikali ingepata faida kubwa licha ya ajira lukuki ambazo zingetengenezwa. Kwa sasa ambapo bei ya mafuta katika soko la dunia ni $30 sidhani kuwa bei ingekuwa wastani wa sh. 1800 kwa lita ambazo tunauziwa kwa sasa. Ni ukweli unaouma kuwa TANESCO ilishanyanganywa uwezo wake wa kuzalisha umeme isipokuwa ule wa vyanzo vya maji. Kwa gesi yetu ungedhani kuwa umeme ushuke bei lakini sivyo. Kuna vigogoi wanaoitwa wawekezaji ambao wamekopeshwa na serikali pesa za kununulia majenereta na wameyategesha wakaunganisha na gesi na wao ndo wanaoiuzia TANESCO umeme. Wananunua gesi kwa makampuni ya gesi inayoitwa ni yetu??? na wanazalisha umeme na kuiuzia TANESCO kwa bei juu. Nini kingekuwa kigumu kwa tanesco kumiliki majenereta hayo? Ilianza wakati wa Net group solutions wakati ule wa Mkapa....!!!!
Tatizo ni usimamiaji nchi nyingi umeme unahodhiwa na mashirika binafsi mfano UK hii nishati inaendeshwa na mashirika binafsi sema serikali inahitaji kuwa makini na hao inayowaamini kusimamia hii nishati
 
Hivi unaelewa hata tunacho andika humu?
au uko kwa kazi ya kumtetea Muhongo?

Hakuna anaepinga wawekezaji kufanya generation lakini why wachukue generation ya Tanesco?

why wasianzishe za kwao?

Umeme wa dharula haujui kuwa ilikuwa ni dili la kupangwa?
hujui kweli au unajifanya hujui?
Labda ni generation zipi za tanesco ambazo zimetamkwa kwamba zitachukuliwa na wawekezaji binafsi nendeni kule mawengi, chipole muone wawekezaji binafsi wa umeme wa maji wanaouzia umeme wananchi na huku tanesco nayo ikizalisha umeme na kusambaza umeme sehemu nyingine. Hicho ndicho anachosisitiza muhongo, wawekezaji wengi zaidi kuzalisha umeme na si tanesco kunyang'annywa hilo jukumu.
 
Kwa ajili ya usalama wa nchi ndio maana usambazaji unaachwa mikononi mwa TANESCO!
Tumia akili una sambaza nini Kama anaye miliki generation ni mtu binafsi na yeye ni mfanya biashara na kuna vitu mmeshindana yeye ana switch off mitambo yake.umeme ni uchumi na umeme nyenzo ya ulinzi na usalama.
 
Utasambaza nini kama mzalishaji akigoma kuzalisha?
Labda kama unazungumzia uzalishaji wa Big G! Yaani mtu ameingia hasara ya billions of TZS halafu agome kuzalisha tu bila sababu? Unless kama hao wazalishaji wanakuwa vyama vya siasa!
 
Kwa ajili ya usalama wa nchi ndio maana usambazaji unaachwa mikononi mwa TANESCO!
Nimtetee Muhongo kwa misingi ipi? Maswali ambayo nimekuuliza hakuna hata moja ambalo umejibu! By the way, unapohoji kwanini wasianzishe za kwao; unamaanisha nini hasa? Kwani Songas leo hii wanapozalisha umeme si kwamba wameanzisha za kwao? Kwani Aggreko wanapozalisha umeme leo hii unadhani wanatumia mitambo ya TANESCO? Ikiwa kampuni X inazalisha umeme ni kwamba from the grassroots wanachoanzisha ni cha kwao! Ikiwa wanataka kuzalisha umeme wa mafuta... watalazimika kununua majenereta ya kuzalishia umeme na watalazimika kuagiza mafuta kwa ajili hiyo! The same apply kwa watakaokuwa wanazalisha kwa gas, upepo, maji n.k! Sasa ni nini hicho unachosema kwanini wasianzishe cha kwao?

Halafu unapohoji "kwanini wachukue generation ya TANESCO" unamaanisha nini hasa? Nina mashaka wewe ndo hujaelewa vinginevyo ni generation ya TANESCO ipi unayosema wanataka kuchukua? Kwani IPTL, Songas, Aggreko, Symbion wamechukua generation ya TANESCO?

Kwamba umeme wa dharula ulikuwa deal la kupangwa! Ina maana ule ukame wa 1991 ambao ulipelekea IPTL ulikuwa ni wa kupangwa? Ina maana ile 2007/2008 hakukuwa na matatizo ya umeme? Kinachopangwa ni upatikanaji wa hao wazalishaji lakini ukisema kwamba hata ile dharula ni ya kupanga wakati unafahamu kabisa kwamba wakati ule tulikuwa tunatgemea chanzo kimoja tu cha maji basi sidhani kama huu mjadala utafika mwisho
Kama hajakuelewa na hapa basi kiburi..!!
 
Labda kama unazungumzia uzalishaji wa Big G! Yaani mtu ameingia hasara ya billions of TZS halafu agome kuzalisha tu bila sababu? Unless kama hao wazalishaji wanakuwa vyama vya siasa!
Hehehee nimejikuta na cheka mwenyewe kwa hili jibu lako..!!
 
Tumia akili una sambaza nini Kama anaye miliki generation ni mtu binafsi na yeye ni mfanya biashara na kuna vitu mmeshindana yeye ana switch off mitambo yake.umeme ni uchumi na umeme nyenzo ya ulinzi na usalama.
Wewe ndo unatakiwa kutumia akili! Kwani suala la wafanyabiashara binafsi kuzalisha umeme ni geni hapa Tanzania?
 
Back
Top Bottom