Anayoyasema Muhongo katumwa na Magufuli?

Anayoyasema Muhongo katumwa na Magufuli?

The Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2009
Posts
49,320
Reaction score
117,615
Kwanza niseme nimemuunga mkono Magufuli kwa kurekebisha kosa alilolifanya
la kumteua Eliai\kim Mawsi TRA bila kujali sana watu watasemaje, kitendo cha kumuondoa haraka Maswi ni kizuri.

Sasa cha kushangaza ni kuwa toka waziri Muhongo ateuliwe ni kama amekuja na 'sera zake binafsi' kuhusu umeme.

Muhongo hataki kabisa TANESCO wazalishe umeme wao, mara kwa mara
anazungumza na kusema 'WAWEKEZAJI WAJITOKEZE' au 'UZALISHAJI WA UMEME UFANYWE NA SEKTA BINAFSI', hili amerirudia zaidi ya mara 10 toka apewe hii wizara.

Kibaya zaidi ameanzisha mchakato ambao ulizuiwa alipoondolewa wa kubinfsisha
'uzalishaji umeme unaofanywa na TANESCO.

Anataka TANESCO ibaki na kusambaza na kusafrisha umeme tu huku 'IKINUNUA UMEME' kutoka kwa 'HAO WAWEKEZAJI BINAFSI ANAOWAPIGIA DEBE'

Yaani sio tu wawekezaji binafsi waje kuwekeza vyanzo vipya lakini na 'vyanzo vyote vya TANESCO viende mikononi kwa wawekezaji binafsi.

Ikumbukwe TANESCO haiwezi kununua umeme na kuuza....sababu 'umeme wa kununua ni ghali sana'

TANESCO ili iweze kununua inalazimika kupewa ruzuku na Serikali kuu'

Achilia mbali baadhi ya hao wawekezaji binafsi wanatumia mitambo ambayo ilinunuliwa na TANESCO lakini wanaitumia kuwauzia umeme TANESCO kwa bei ghali na kodi hawalipi kabisa au kulipa kidogo sana.

Hiii yote ilikuwa ni mipango ya Muhongo kabla hajaondolewa, alipoondolewa TANESCO ikaanza kujiimarisha kuzalisha yenyewe umeme.

Sasa karudi na keshaanza tena kuwapigia debe 'wawekezaji binafsi'

Swali ni je Magufuli ana yaa approve yote haya?

Hii ni sehemu ya mipango mipya ya Magufuli?

Kwamba TANESCO inunue umeme asilimia 90 au 100 ndo iuze? ina uwezo huo?
itasaidia kweli?

Ni mipango ya serikali yote au Muhongo binafsi?
 
We uko wapi, UMEME Wa simbion/IPTL, Gareco na wengineo kibao unadhani ni Wa nani ? Na sasa unasikia umeme Wa gas, unafikiri hayo makampun
Ni Ya serikali !!?
 
nadhani pia kwa usalama wa uchumi na taifa kwa ujumla utaratibu wa kubinafsisha uzalishaji wa umeme huenda ukawa hatari!fikiri kama mzalishaji kwa sababu yoyote ile akashindwa kuelewana na TANESCO na kuamua kusitisha uzalishaji nini kitatokea...nchi inaweza kuwa gizani!na vipi huyo mzalishaji akisema hapati faida au ghafla 'akafirisika' kama home shopping centre...tutakaa gizani!!!!
 
Magufuri angalia mtu huyu kujua kwingi huaribu maarifa akisema tanesco isizalishe kabisa umeme iwe inasambaza tu umeme tunarudi kule kwenye richmond watajipangia bei zao wataingia mikataba mibovu kama hivi leo muhongo sijui kafikiria nini
 
In way, anajejeli akina Mengi. Bado serikali itawekeza kwenye Nishati ya umeme lakini ushiriki wa sector binafsi ni muhimu.
Kikubwa ni uzalendo katika kuuziana umeme huo. Majizi ya 10 yakiingia tena hapo, we are finished!
 
In way, anajejeli akina Mengi. Bado serikali itawekeza kwenye Nishati ya umeme lakini ushiriki wa sector binafsi ni muhimu.
Kikubwa ni uzalendo katika kuuziana umeme huo. Majizi ya 10 yakiingia tena hapo, we are finished!
Ili mradi ni Muhongo ndo anasimamia hii sekta
tegemea business as usual ..
nadhani pia kwa usalama wa uchumi na taifa kwa ujumla utaratibu wa kubinafsisha uzalishaji wa umeme huenda ukawa hatari!fikiri kama mzalishaji kwa sababu yoyote ile akashindwa kuelewana na TANESCO na kuamua kusitisha uzalishaji nini kitatokea...nchi inaweza kuwa gizani!na vipi huyo mzalishaji akisema hapati faida au ghafla 'akafirisika' kama home shopping centre...tutakaa gizani!!!!

Muhongo anadai asilimia 90 ya umeme Tanesco inunue...
hatari sana
 
nadhani pia kwa usalama wa uchumi na taifa kwa ujumla utaratibu wa kubinafsisha uzalishaji wa umeme huenda ukawa hatari!fikiri kama mzalishaji kwa sababu yoyote ile akashindwa kuelewana na TANESCO na kuamua kusitisha uzalishaji nini kitatokea...nchi inaweza kuwa gizani!na vipi huyo mzalishaji akisema hapati faida au ghafla 'akafirisika' kama home shopping centre...tutakaa gizani!!!!
Mfano TTCL.
 
Baada ya baraza la mawaziri kutangazwa ,nilipoona jina la Simbachawene na Muhongo moja kwa moja nikahisi kuwa kuna kazi walikuwa wameianza katika baraza la mawaziri lililopita walikuwa wamekuja kuimalizia.Kumbuka Simbachawene alipeleka miswada ya gesi na nishati ikajadiliwe dakika za mwisho kwa hati ya dharura ,ikakataliwa kisha ikarudishwa na kupitishwa bila akidi kutimia dakika za mwisho-Hicho ndicho walichokuja kumalizia. Huu ni mwanzo tu!
 
The Boss,

Inawezekana hizi taarifa zilikupita lakini si za jana wala leo... in short ni mpango ambao uliasisiwa kabla ya Magufuli hajaingia madarakani na kabla wakati sakata la Escrow halijachukua kasi. Ikiwa umesahau, basi rejea ule mpango wa kuivunja TANESCO na kuwa mashirika matatu-- la uzalishaji, usafirishaji na usambazaji. Kwenye huo mpango ndo unakutana na hilo suala la sekta binafsi kuzalisha umeme!

Kwa upande mwingine usisahau-- pia hakuna jipya katika hilo manake tayari sekta binafsi zinazalisha na kuwauzia umeme TANESCO. Hawa ni pamoja na Symbion as well as IPTL. Kinachotokea hivi sasa ni kama tu kurasmisha suala la sekta binafsi kuingia huko kwavile wawekezaji binafsi karibu wote waliingia kwenye biashara hii kwa sababu maalum ambayo ilikuwa ni kutatua dharura ambayo ilitokea! Rejea ujaji wa IPTL na Richmond including PAN Energy (sina hakika na hili jina)! Hawa wote waliingia kwa dharura! So, the idea ni kwamba, badala ya kusubiri dharula itokee (upungufu mkubwa wa umeme) ndipo kuwataka sekta binafsi wazalishe umeme wa dharula basi ni heri wale wenye uwezo waruhusiwe kuingia kwenye hiyo biashara moja kwa moja ili kuzuia hizo dharula zisitokee! Kinyume chake ni TANESCO wenyewe wawe na uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha kwa kutumia vyanzo mbalimbali ambao hata kama utatokea ukame wa kutisha; isiwe tena sababu ya kuingia kwenye dharula! Now the question is: Je, TANESCO wanao huo uwezo? Ikiwa tunajiridhisha hawana na serikali haina uwezo au sababu ya ku-finance basi hakuna mbadala zaidi ya sekta binafsi kuingia mchezoni na sio kusubiria ukame halafu zabuni zianze tena kutolewa kwa vi-memo.
 
Pole sana mzalendo , hili ndilo lilimfanya magufuri azibe masikio na kutuletea mtu yuleyule aliyetimuliwa bungeni , tena eneo lilelile !
 
The Boss,

Inawezekana hizi taarifa zilikupita lakini si za jana wala leo... in short ni mpango ambao uliasisiwa kabla ya Magufuli hajaingia madarakani na kabla wakati sakata la Escrow halijachukua kasi. Ikiwa umesahau, basi rejea ule mpango wa kuivunja TANESCO na kuwa mashirika matatu-- la uzalishaji, usafirishaji na usambazaji. Kwenye huo mpango ndo unakutana na hilo suala la sekta binafsi kuzalisha umeme!

Kwa upande mwingine usisahau-- pia hakuna jipya katika hilo manake tayari sekta binafsi zinazalisha na kuwauzia umeme TANESCO. Hawa ni pamoja na Symbion as well as IPTL. Kinachotokea hivi sasa ni kama tu kurasmisha suala la sekta binafsi kuingia huko kwavile wawekezaji binafsi karibu wote waliingia kwenye biashara hii kwa sababu maalum ambayo ilikuwa ni kutatua dharura ambayo ilitokea! Rejea ujaji wa IPTL na Richmond including PAN Energy (sina hakika na hili jina)! Hawa wote waliingia kwa dharura! So, the idea ni kwamba, badala ya kusubiri dharula itokee (upungufu mkubwa wa umeme) ndipo kuwataka sekta binafsi wazalishe umeme wa dharula basi ni heri wale wenye uwezo waruhusiwe kuingia kwenye hiyo biashara moja kwa moja ili kuzuia hizo dharula zisitokee! Kinyume chake ni TANESCO wenyewe wawe na uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha kwa kutumia vyanzo mbalimbali ambao hata kama utatokea ukame wa kutisha; isiwe tena sababu ya kuingia kwenye dharula! Now the question is: Je, TANESCO wanao huo uwezo? Ikiwa tunajiridhisha hawana na serikali haina uwezo au sababu ya ku-finance basi hakuna mbadala zaidi ya sekta binafsi kuingia mchezoni na sio kusubiria ukame halafu zabuni zianze tena kutolewa kwa vi-memo.

Why tanesco wazuiwe kuzalisha sasa?
why generation ya Tanesco iwe ya kwanza kubinafsishwa?
why now? why so fast?

Why Tanesco inyang'anywe generation? na itakiwe kununua aslimia 90?
huku uwezo haina wa kununua? nani atakaeumia?
 
Mfano TTCL.
Kwa ajili ya usalama wa nchi, sector ingebaki mikononi mwa serikali. Nchi nyingi ambazo ni developed ndiyo sera yao. Au angalau kampuni ya nchi husika sio ya nje
Ili mradi ni Muhongo ndo anasimamia hii sekta
tegemea business as usual ..


Muhongo anadai asilimia 90 ya umeme Tanesco inunue...
hatari sana
 
Kuna vitu viwili ambavyo kwa maoni yangu serikali isingeachia sekta binafsi ivitawale. Kimoja ni uzalishaji na usambazaji wa nishati ya umeme na cha pili ni uagizaji na uuzaji wa nishati ya mafuta. Hivi ni vitu vya muhimu sana kwa uchumi na usalama wa nchi na nadhani ni kosa kuiachia sekta binafsi. Nilikuwa nangoja nisikie wakisema kuwa wanafufua kiwanda cha uchakataji wa mafuta ghafi-TIPER- ambapo serikali ingeagiza na kuchakata mafuta hayo humu nchini. Bei ya mafuta ingepungua sana na serikali ingepata faida kubwa licha ya ajira lukuki ambazo zingetengenezwa. Kwa sasa ambapo bei ya mafuta katika soko la dunia ni $30 sidhani kuwa bei ingekuwa wastani wa sh. 1800 kwa lita ambazo tunauziwa kwa sasa. Ni ukweli unaouma kuwa TANESCO ilishanyanganywa uwezo wake wa kuzalisha umeme isipokuwa ule wa vyanzo vya maji. Kwa gesi yetu ungedhani kuwa umeme ushuke bei lakini sivyo. Kuna vigogoi wanaoitwa wawekezaji ambao wamekopeshwa na serikali pesa za kununulia majenereta na wameyategesha wakaunganisha na gesi na wao ndo wanaoiuzia TANESCO umeme. Wananunua gesi kwa makampuni ya gesi inayoitwa ni yetu??? na wanazalisha umeme na kuiuzia TANESCO kwa bei juu. Nini kingekuwa kigumu kwa tanesco kumiliki majenereta hayo? Ilianza wakati wa Net group solutions wakati ule wa Mkapa....!!!!
 
Kuna vitu viwili ambavyo kwa maoni yangu serikali isingeachia sekta binafsi ivitawale. Kimoja ni uzalishaji na usambazaji wa nishati ya umeme na cha pili ni uagizaji na uuzaji wa nishati ya mafuta. Hivi ni vitu vya muhimu sana kwa uchumi na usalama wa nchi na nadhani ni kosa kuiachia sekta binafsi. Nilikuwa nangoja nisikie wakisema kuwa wanafufua kiwanda cha uchakataji wa mafuta ghafi-TIPER- ambapo serikali ingeagiza na kuchakata mafuta hayo humu nchini. Bei ya mafuta ingepungua sana na serikali ingepata faida kubwa licha ya ajira lukuki ambazo zingetengenezwa. Kwa sasa ambapo bei ya mafuta katika soko la dunia ni $30 sidhani kuwa bei ingekuwa wastani wa sh. 1800 kwa lita ambazo tunauziwa kwa sasa. Ni ukweli unaouma kuwa TANESCO ilishanyanganywa uwezo wake wa kuzalisha umeme isipokuwa ule wa vyanzo vya maji. Kwa gesi yetu ungedhani kuwa umeme ushuke bei lakini sivyo. Kuna vigogoi wanaoitwa wawekezaji ambao wamekopeshwa na serikali pesa za kununulia majenereta na wameyategesha wakaunganisha na gesi na wao ndo wanaoiuzia TANESCO umeme. Wananunua gesi kwa makampuni ya gesi inayoitwa ni yetu??? na wanazalisha umeme na kuiuzia TANESCO kwa bei juu. Nini kingekuwa kigumu kwa tanesco kumiliki majenereta hayo? Ilianza wakati wa Net group solutions wakati ule wa Mkapa....!!!!


serikali zinazo jielewa hata daladala marufuku
huduma na biashara ni vitu viwili tofauti
 
Mzimu wa Muhongo unawasumbua kwelikweli tueleze ni wapi na lini muhongo katamka kkwamba tanesco haitazalisha umeme??? Kinachosisitizwa na jembe hili ni wawekezaji binafsi pia kuzalisha umeme ili uwe wa kutosha na si kutegemea tanesco pekee. Kukiwa na mgawo wa umeme mnalalamika monopoly ya tanesco, watu wakialikwa kuzalisha umeme zaidi mnalalamika ooohhh tanesco inanyang'anywa jukumu lake. Acheni jembe lifanye kazi hizi cheap politics hazitawasaidia
 
Maswali yako mbona ya kitoto sana? Tena serikali ifanye haraka kuhamasisha wawekezaji kuwekeza kuzalisha umeme. Nchi zilizoendelea zinatumia utamaduni huo. Serikali ibaki na kazi moja tu ya kusambaza umeme kwa wananchi. Mambo ya uzalishaji waachiwe sekta binafsi. Wapo akina IPTL, SONGAS, AGGREKKO na wengine ambao wamekuwa wakifanya hivyo tangu muda mrefu. Cha muhimu hapa ni serikali kuwapangia bei hao wazalishaji ili wasituumize wananchi
 
Umemuuliza maswali ya msingi sana. Hawa jamaa kazi yao kuropoka tu
Mzimu wa Muhongo unawasumbua kwelikweli tueleze ni wapi na lini muhongo katamka kkwamba tanesco haitazalisha umeme??? Kinachosisitizwa na jembe hili ni wawekezaji binafsi pia kuzalisha umeme ili uwe wa kutosha na si kutegemea tanesco pekee. Kukiwa na mgawo wa umeme mnalalamika monopoly ya tanesco, watu wakialikwa kuzalisha umeme zaidi mnalalamika ooohhh tanesco inanyang'anywa jukumu lake. Acheni jembe lifanye kazi hizi cheap politics hazitawasaidia
 
Why tanesco wazuiwe kuzalisha sasa?
why generation ya Tanesco iwe ya kwanza kubinafsishwa?
why now? why so fast?

Why Tanesco inyang'anywe generation? na itakiwe kununua aslimia 90?
huku uwezo haina wa kununua? nani atakaeumia?
Miaka 50 sasa; huo umeme wanaozalisha uko wapi ukiacha ule wa maji?! Mara zote inapotokea dharula ya umeme TANESCO wameshawahi kuwa na uwezo ku-accommodate hiyo dharula zaidi ya kurudi kwenye sekta binafsi? Sasa kwanini tusubirie dharula kisha tuje na project za zima taa kama zile ya IPTL na Richmond?! Na ndio maana nikauliza; je tumejiridhisha ikiwa TANESCO wanao uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha ambao haitajalisha kwamba kuna ukame mwaka mzima au mvua mwaka mzima... bado umeme unaozalishewa na TANESCO uwe na uwezo wa kuhudumia wataje wake!

Kwamba WHY NOW, tayari nimeshakuambia kwamba huu mpango sio wa sasa/mpya unless kama unauliza why uwe implemented now! Huu mpango una miaka sasa na idea ya kuifanya TANESCO iwe kampuni 3 tofauti ina zaidi ya miaka 5 hivi sasa. Hata Muhongo alipochaguliwa kwa mara ya kwanza na JK, aliukuta huu mpango-- alichofanya yeye ni kuu-speep up.

Suala la generation kuwa kwenye sekta binafsi ni kuifanya TANESCO ifanye investment ya resources zake kwenye usambazaji badala ya kufanya kila kitu-- uzalishaji, usafirishaji na hadi usambazaji ni hao hao! Wadau wamejiridhisha kwamba kuwa na multiple functions ambazo zote zinahitaji resources za kutosha ni moja ya sababu ya kuifanya TANESCO ikose efficiency! Na hili halina mjadala manake linaonekana hata kwa jicho moja. Ikizima mashine moja tu; watu tunaingia gizani kwa sababu tayari tunakuwa na upungufu!Na huko kwenye uzalishaji ndo kwenye changamoto zaidi kwa TANESCO kwa kuwa kunahitaji mtaji wa kutosha!

Sasa hapo ni lazima uchague! Ama iachwe TANESCO iendelee na mwendo wake wa kusuasua... ukija ukame mnaanza kuitisha zabuni za zima taa au uruhusu sekta binafsi iingie rasmi! Ukisema sekta binafsi iingie na TANESCO iendelee kuzalisha umeme; sekta binafsi itasita kuingia kwenye game kwa kuchelea kuwa na competitor ambae ni shirika la serikali huku akiwa pia ndo mdau mwenyewe!
 
Back
Top Bottom