Hivi ninyi mnafahamu kweli malaika? Jini mwenyewe hawezi kuanguka. Hao ni viumbe wa kiroho wataangukaje iwapo wawezaingia ndani ya nyumba mkiwa mmefunga kila mahali? Malaika aweza kupenya popote na wala hakuna wa kumzuia. Kwanza malaika akitokea mahali ule utukufu wake tu watu wanapigwa mweleka na kuanza kusujudi na kulia wakidhani ndiye Mungu kumbe la!. Achana kabisa na mambo ya kiroho ni habari nyingine. Kwanza malaika hawezi kumtokea mtu yeyote maana ni mjumbe maalum wa Mungu kwa mwanadamu aliyepewa kazi na Mungu. Sana sana hicho kiumbe nadhani ni mchawi tu wa kizungu kaanguka na ungo lakini kwa kuwa wazungu hawaamini kuwepo kwa wachawi wa ungo basi wanamlinganisha na malaika kisa eti ameanguka kutoka juu. Wazungu wengi hawajui na wala hawaamini mambo ya kiroho wamejikita tu kisayansi lakini kuna baadhi yao ni wachawi wa kutupwa na wanawanyanasa sana.