Anaumia kwa mambo yake ya nyuma

Anaumia kwa mambo yake ya nyuma

kinyangesi

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2012
Posts
247
Reaction score
86
Habari wanajamvi?

Mimi nna mwenzi wangu ambaye tumepanga kutambulishana kwa wazazi mwishoni mwa mwaka huu. Huyu binti ambaye natarajia awe mke wangu tulijuana zaidi ya miaka 6 ivi ila si kama wapenzi.

Tatizo linalomsumbua ambalo nimeona niombe ushaur wenu ili nimsaidie ni kwamba alipokuwa anasoma Sekondari aliwahi kukamatwa akifanya mapenzi, alifukuzwa shule na baadae wazazi waliamua kumuamisha Mkoa akaendelea na kumaliza elimu yake.

Sikuwahi kuijua story hii mpaka tulipokuwa wapenzi ndo aliniadithia. Amekuwa akirudia mara kwa mara kuniambia tukio lile la aibu uwa linamuumiza sana sasa hata anaogopa kuwaambia wazaz wake kuwa ana mtu anayetaka kumtambulisha ili baadae niwe mumewe.

Mimi na yeye tunaishi mikoa tofauti kwani yupo Arusha nami nipo Dar, pia sijawahi kufanya nae mapenzi. Mnishauri wana Jf jinsi ya kumsaidia huyu binti kwani nampenda.

Nahitaji awe huru
 
Kweli kuna zaidi ya hilo.mwambie afunguke tuu.Kuna kitu hajakwambia.na anahisi akikuambia unaweza kughair hyo ndoa ama hutompenda kama awali.
 
Kweli kuna zaidi ya hilo.mwambie afunguke tuu.Kuna kitu hajakwambia.na anahisi akikuambia unaweza kughair hyo ndoa ama hutompenda kama awali.

Mmh.. mi nimeshamwambia sitaacha kumpenda . Nadhan uwo ndo ukweli wake tu
 
Endelea kumpenda tu kaka, maana hamna namna sasa

Teheee...we nawe icho kiitikio cha pm umekikariri vizuri.
"Maana ni lazima tukubaliane tu ndoa zitakuwa kwa mujibu wa sheria. Sasa kama wewe hutaki unakuwa mbishi zaidi. Hautapendwa tu! #jokes
 
Huyu binti ambaye natarajia awe mke wangu
  1. tulijuana zaidi ya miaka 6 ivi ila si kama wapenzi.
  2. ni kwamba alipokuwa anasoma sekondari aliwahi kukamatwa akifanya mapenzi, alifukuzwa shule na baadae wazazi waliamua kumuamisha mkoa akaendelea na kumaliza elimu yake.
  3. sijawahi kufanya nae mapenzi.
  4. Mnishauri wana Jf jinsi ya kumsaidia huyu binti kwani nampenda. Nahitaji awe huru
  5. Mimi na yeye tunaishi mikoa tofauti kwani yupo arusha nami nipo dar,
haya hapo pakali ukiunganisha 1, 3 & 5 sina Neno kwani hakuna mapenzi hapo Hakuna
 
Yaliyopita sindwele angalia yajayo. Kama anakijutia kitendo hicho inaonyesha amejitambua na anaweza kuja kua mke mzuri. kanyaga mwendo songa mbele
 
mhh nimekuelewa vibaya nini au? miaka 6 hujamzama chumvini!!!!!!! Hakika tulia utengenezwe mana hilo tatizo halizuii kukutambulisha ila mko wawili na mwenzako amekuzidi kidog so bibie hana jinsi lazma atengeneze mkeka ili abet asiliwe.... Ila aya buana ngoja nielekee zangu kwa pusha mara moja.
 
mhh nimekuelewa vibaya nini au? miaka 6 hujamzama chumvini!!!!!!! Hakika tulia utengenezwe mana hilo tatizo halizuii kukutambulisha ila mko wawili na mwenzako amekuzidi kidog so bibie hana jinsi lazma atengeneze mkeka ili abet asiliwe.... Ila aya buana ngoja nielekee zangu kwa pusha mara moja.

Aisee umenielewa vibaya! Huyu binti tunafaamiana kama miaka sita ivi kama marafiki tu wa kawaida ila miez 5 iliyopita ndo tumekuwa karibu kama wapenzi
 
Back
Top Bottom