Anaumia kwa mambo yake ya nyuma

Anaumia kwa mambo yake ya nyuma

Habari wanajamvi?

Mimi nna mwenzi wangu ambaye tumepanga kutambulishana kwa wazazi mwishoni mwa mwaka huu. Huyu binti ambaye natarajia awe mke wangu tulijuana zaidi ya miaka 6 ivi ila si kama wapenzi.

Tatizo linalomsumbua ambalo nimeona niombe ushaur wenu ili nimsaidie ni kwamba alipokuwa anasoma Sekondari aliwahi kukamatwa akifanya mapenzi, alifukuzwa shule na baadae wazazi waliamua kumuamisha Mkoa akaendelea na kumaliza elimu yake.

Sikuwahi kuijua story hii mpaka tulipokuwa wapenzi ndo aliniadithia. Amekuwa akirudia mara kwa mara kuniambia tukio lile la aibu uwa linamuumiza sana sasa hata anaogopa kuwaambia wazaz wake kuwa ana mtu anayetaka kumtambulisha ili baadae niwe mumewe.

Mimi na yeye tunaishi mikoa tofauti kwani yupo Arusha nami nipo Dar, pia sijawahi kufanya nae mapenzi. Mnishauri wana Jf jinsi ya kumsaidia huyu binti kwani nampenda.

Nahitaji awe huru
muulize alikuwa anafanya mapenzi kawaida tu au kwa njia nyingine maana kama alikutwa akitumia njia ya kawaida huwezi kukuumiza lakini huko mgongoni lazima imuume roho
 
kama ni kweli huyo binti anamaanisha, ninachomwelewa ni kuwa hana imani na wewe na anahofia kuwaambia wazazi halafu wewe ukaingia mitini. Ushauri wangu kwako kama upo serious, ni wewe kwenda moja kwa moja kwa wazazi na wazee wako kuongea mahali, acha mbwembwe na longolongo zingine, HIT the POINT.
 
She z physical, psychological n emotion tortured. Kwa tatizo hilo lililomtokea limemuumiza Maeneo hayo Matatu. Baada ya tatizo lile kutokea inaelekea mpaka sasa hajaamini kama ni yy kweli alifanya ile dhambi. Bado anabishana na nafc yake kwamba dis can't be. Na Aibu aliyopata shuleni hadi nyumbani imemfanya mpk Leo asisahau na Awe MTU kujilaumu siju zote na wakutojiamini ktk mambo mengi hasa Wakati wakufanya Maamuzi mbalimbali. Ushauri: mwambie Asiendelee kujilaumu.. She should accept the Fact.. Akubali kutoka Moyoni Kosa alilofanya. Hata kama ukweli ni Mchungu vipi ili apone Lazima aukubali 1) Amuombe Mungu Msamaha kama hakufanya hivyo 2) Ajisamehe Yeye Mwenyewe.3) Awaombe Msamaha Wazazi wake tena.. Na awaeleze dhambi ile inavyomtesa asifiche kitu ili apone.. Hakika wazaz watampokea tena nakuona kuwa Amekua. 4) Awasamehe wazaz wake kwa Maneno waliyomtamkia na Adhabu baada ya tukio. 5) Awasamehe Wanafunzi wote kuanzia Ex wake na Marafiki waliomchomea awasamehe na Walimu. Ahakikishe Hakuna MTU aliyemuweka kwny gereza la Moyo wake kutokana na ile dhambi. Hapa Atakuwa
Huru na atahisi katua mzigo mzito.6) Nenda nae kwa Wazazi halafu Mpe ruhusa ya kukutambulisha kwa Wazaz wake coz watakuwa wamempokea mara ya pili hapa itamjengea confidence na kujiona ni MTU wa kuaminika tena 7) kaanae Karibu sana ukimtia Moyo hasa ukimjengea ujasiri "U Can" ziwe nyingi.. Mpatie na Nyimbo za kumtia nguvu kama HERO by Mariah Carey. Mzidi Kumuomba Mungu Awatetee katika Safari yenu ya Maisha.
 
Mi sioni kama kuna ishu hapa la da kama dem anataka kumpotezea.nilijua kabakwa na kutiwa mimba au la da katoa mimba mimba
 
Back
Top Bottom