Steven mushi mushi
JF-Expert Member
- Jul 25, 2016
- 533
- 741
Huyu binti nilikutana nae chuo mwaka 2014 nayeye alikuwa anasoma hapohapo chuo ila coz tofauti na niliyokuwa nasomea mimi, mm nilikuwa nasoma mambo ya tourism na yeye alikuwa anasomea childhood. Baada ya kufahamiana tukaanza urafiki na baadaye tukawa wapenzi, alipomaliza chuo mwaka jana akaomba fld moja kati ya shule za private hapa mjini na kwa bahati nzuri alipata fld na alipomaliza fld kutokana na kufanya vizuri kipindi yuko training ile shule ikaamua kumuajiri moja kwa moja kwa sababu na wenyewe walikuwa wanahitaji mwalimu kwa kipindi hicho hivyo wakaona heri wamchukue yeye. Mimi pia nilipomaliza nikaomba fld TANAPA maana mm nilisomea tourism na nashkuru mungu nilipewa nafasi ya training moja kati ya hifadhi zetu hapa nchini na juzi ndo nimemaliza na kwa sasa nipo mtaani natafuta ajira. Sasa tangu nirudi kutoka fld nashangaa huyu binti kaja na wazo anataka tuoane kwa sasa tofauti na mipango yetu, tulikubaliana kuwa tutakapo pata kazi tujipange kwanza angalau tuwe tumeshajenga ili tukioana angalau tuishi kwetu maana mm kwa sasa bado naishi na wazazi wangu ila nashangaa yeye analazimisha tuoane kwa sasa wakati naendelea kutafuta kazi eti kwa kisingizio kuwa tutatumia mshahara wake kujikimu na maisha wakati naendelea kutafuta kazi ila mm nimekataa katukatu kumuoa kwa sasa maana tulikubaliana tutaoana miaka minne ijayo. Sasa tangu jana kanuna hataki kunisemesha wala kuelewa yeye anachotaka tu ni ndoa kwa sasa. Ila mm nimemwambia ukweli kwamba kumuoa kwa sasa ni vigumu ingawa nampenda huyu binti na nina malengo naye na sababu sinazonifanya nisioe nimemwambia kwanza mm sina kazi pili sijajipanga na mbaya zaidi bado naishi na kwa wazazi wangu ila yeye hataki kunielewa. Hebu nishaurini wana JF nifanyeje maana naona huyu mchumba wangu anaanza kunivuruga kwa kuanza kwenda kinyume na mipango yetu tuliyokubaliana hapo awali juu ya kuoana kwetu.