Anataka mwanae

Anataka mwanae

wat goes around comes around yameshamkuta huyo...unajua wakati mwengine binaadamu tunafikria yaliyopo sasa tu hatufikirii out of the box...
Ushauri wangu kwako ni kwamba huyo ndio baba mzazi wa huyo mtoto ijapokuwa alishamkataa na kwa nilivyoelewa hakusaidii katika malezi/matunzo ya huyo mtoto..lakini huwezi kubadili fact kwamba yeye ndio biological father.hata hili suala likichukuliwa kisheria huyo mwanaume ana haki ya kuwa baba wa huyo mtoto.na huyo mtoto ana haki ya kumjua babaake mzazi.
Naelewa misukosuko ulopitia nakupa pole sana kwa hilo lakini kumbuka ukifikiria sana jinsi watu/jamii watakavyokufikiria hutoendelea.katu usifanye kitu kumridhisha mtu au watu, fanya kitu kwasababu nafsi yako inataka hivyo isitoshe lolote utakalofanya watu hawakosagi la kusema.
Kuhusiana na mumeo anajua tangia ulipokuwa mjamzito kuwa huyo mtoto si wake,sidhani kama atakosa uelewa iwapo baba mzazi wa mtoto akitaka mwanae,yeye ndio mlezi mkuu wa huyo mtoto na kitu kimoja ni kwamba thamani yake haitoshuka kwa huyo mtoto abadani,mtoto anamthamini yule anaemlea kwa upendo...

word word word.,.critical thinker...by the way nibora kua mwazi kwa kila mtu namaanisha pand zote mbil kwa mume na nyumban kwa bint..then after al zungumzen na baba wa mtoto na kila mtu apewe hakh ya kumlea huyo mtoto bcoz nyote mu wazazi wake..na sio mikwaruzano kujakutibua ndoa yako.
 
Wanaume wa aina hii si wa kuvumilia wala kuhurumia.
Damu yake hakuijua mwanzo ndo aje aijue leo???

Ni kweli anayo haki kwa mwanae lakini pia anaikosa hiyo haki kwa kitendo chake cha kumkataa huyo mtoto.
Asikutishe na kwenda mahakamani, kinachotakiwa ni wewe kuwa ngangali hasa kama kweli hutaki kumkosa mwanao.
 
Dah mami kisa hiki kinasikitisha sana, Sina huruma na huyo hayawani aliekataa mimba mi ningempoteza kabisa asiniharibie ndoa yangu. Aliharibu usichana wako, na sasa anataka kuharibu ndoa yako.
Ninamhurumia huyu mwanaume hodari, mwema labda kama Yesu, mwenye mapenzi ya dhati, muungwana cjui nimuelezee vipi, aliyekuokota ukiwa umeanguka, akakubeba na kukupa sababu ya kuishi na kukupenda wa dhati. Hastahili kuumizwa kabisa na huyo hayawani, nadhani bunduki yake haikuwa na risasi ndo mana akakimbia mimba...
Nakushauri ongea na huyu mume kuhusu hili, kwavile anakupenda atakuelewa..
Hata ndugu na jamaa watakuelewa manake hili si ajabu la dunia. Mambo mengi makubwa na ya kutisha yanatokea kwny familia na jamii hili la kwako si la kutisha...
Nendeni mkapate ushauri wa kisheria...namna ambavyo mtaishi na mdau mwingine ktk ndoa yenu.
namna ya kumuona mtoto na haki za mtoto kwa baba yake mzazi, hakuna namna mtaweza kukwepa... huu ni ukweli mchungu, saa nyingine unaumeza na maisha yanaendelea.
 
Kwa madai ya kuwa mtoto wako yuko katika ndoa nyingine?
Ana ushahidi gani kuweza kuishawishi mahakama kuwa mtoto ni wake?
Jeanclaude! Sidhani kama ana haki yeyote;
Ni kama katika Biblia jinsi ESAU alivyouza haki yake ya mzaliwa wa kwanza.

Bazazi!

Ahsante Judge! Manake hii kesi ikija kwako huyu ni tupa kuleee!
 
Usichukulie poa, hapo baadaye itawaletea shida kubwa, kaa na mume wako zungumzeni kama vipi mpeni mtoto wake maana hiyo ni damu yake.

Suala hapa si kupewa mtoto hata mimi mngenichinja kwanza ndio mumpe mtoto. Haki yake ni kumuona mtoto, kumhudumia, na kutambuliwa na huyo mtoto kama yeye ndiye baba mzazi.
Mtoto akifika 14 basi na yeye anaweza kumfuata baba yake lakini si katika umri huu mdogo akakae na mama wa kambo! Never never! tumbo la uzazi wamama mnalijua linakataje!
Huko aliko ajaze vizuri bunduki yake risasi na ajue kulenga apate wa kukaa nao. Huyu awe ana kuja kumuona kwa muda maalumu tu.
 
baada ya kukosa ndipo anakumbuka aliyemkataa mwanaume wengine wanafaa kufungiwa jiwe watupwe baharini....namwinea huruma baba mlezi wa mtiti atajisikiaje pindi atakopopata taarifa hizo.....cha muhimu ongea na mumeo mjadiliane kwa kina inauma lakini mwaweza kufikia muafaka jaribu kujadili kwa upole bila kuleta vurugu kuharibu ndoa yako
 
hilo umelikoroga ndugu!binadamu hadhulumiwi kama fedha hapo hata umfiche vp mwisho wa siku kitanuka tu!cha muhimu fanya hima umalizane na mzazi mwenzi from the start ilitakiwa ueleze ukweli tu hukuwa na sababu ya kuficha wazaz na ndugu zako.
 
hilo swala lingekuwa wazi kwa wazazi wa pande zote mbili ingekuwa rahisi kuwashirikisha wao....ila kama wanajua mtoto ni wa mumeo....nadhani ndo kipindi cha wao kujua ukweli ......ongea na mumeo kuhusu kuwaeleza wazazi ukweli ili na wao wawasaidie kutoa mawazo ya nini cha kufanya......

Siyo sahihi

Kuna tatizo hapo...... hasa kwa huyu bi dada mleta uzi...

1. Anasema huyo bwana alikataa mtoto ikiwa ni mimba ya miezi miwili ...na hivi sasa huyo bwana anamsumbua kwa simu na hata ofisini anafika...tafsiri yake ni kwamba BADO WANA MAWASILIANO

2. Mtoto huyo kwa umri aliofikia sasa anafahamu kwamba baba mlezi ndiye BABA YAKE...fikiria maumivu ya kiakili atakayopata wakati atakapoambiwa kwamba huyo anayemlea kwa sasa siyo baba yake....

3. Huyu mleta uzi inaonesha amechanganyikiwa....unaweza kuliona hilo katika maandiko yake....bado anahisia na huyo MTUNGA MIMBA na mumewe hajui hilo na hawajawahi kulijadili...hilo linajieleza kwa yy kuleta hilo suala hapa kwenye jukwaa...KAA NA MUMEO PERIOD
 
huyo jamaa alifanya vibaya,lakini juu ya yote ukweli hautopingika ni mtoto wake.ni vizuri ungekaa chini ukazungumza na mume wako na huyo jamaa pia,kwani hapo mnaemuumiza ni huyo mtoto baadae akijua ukweli ataumia sana tu.kwa kumchukua moja kwa moja usikubali,yamemchanganya kwa kuwa huko hajapata mtoto.ila uwe mwangalifu maana wanaume wengine wanapenda kuharibu tu,bila kujali yupi anaemumia.mwambie akupe muda
 
mimi nashindwa kuelewa jambo moja hapa na hapa ningeomba Bazazi kaka yangu mpenzi anieleweshe. ivi mtu aliyekukataa miaka 5 liyopita ukiwa na ujauzito wa miez 2, leo hii anawasiliana na wewe je nini kilichowakutanisha hadi mkaanza kuwasiliana??

je kama jambo hili liko wazi kwa mume mlezi je mbona hujaweza kumwambia juu ya usumbufu wa huyu baba mzazi??

sawa alilea mimba na sasa analea mtoto je ipo wapi shida ya kuongea nae juu ya hatma ya huyu mtoto?
 
Last edited by a moderator:
mimi nashindwa kuelewa jambo moja hapa na hapa ningeomba Bazazi kaka yangu mpenzi anieleweshe. ivi mtu aliyekukataa miaka 5 liyopita ukiwa na ujauzito wa miez 2, leo hii anawasiliana na wewe je nini kilichowakutanisha hadi mkaanza kuwasiliana??

je kama jambo hili liko wazi kwa mume mlezi je mbona hujaweza kumwambia juu ya usumbufu wa huyu baba mzazi??

sawa alilea mimba na sasa analea mtoto je ipo wapi shida ya kuongea nae juu ya hatma ya huyu mtoto?

Maswali yako gfsonwin sina majibu kwa kuwa sioni mantiki ya mawasiliano yao.
Kwanza sijui ilikuwaje wakaanza kuwasiliana na ili iweje?
Kwa nini mwanamke anayaruhusu mawasiliano hayo?
Kwanini mwanaume (maluuni) hajifungi kibwebwe kumfuata mwanaume mwenzake wayaongee?
Hoja kama hii iliwahi kuletwa JF kama sikosei mwaka 2008:
Ingawa ziko tofauti kidogo;
Ile likuwa mtoto wa katikati (ndani ya ndoa) baada ya mwanamke kuzini.

Anayeweza kuiweka hapa amsaidie dada wa watu asije kuheuka bure?
Ingawa namshauri aachane na huyo maaluni wake asiye na hata chembe ya utu;
Ukatae mimba leo baada ya miaka kadhaa udai mtoto;
Hata hivyo nadhani jibu zuri ni kuwa baada ya kuikataa mimba niliitoa!


@nginaeli kwa nini huitumii elimu yako (Masters) kumaliza kikaango chako?
Je bado unakumbuko mikito ya baba ya mtoto?
Mumeo u nampenda kweli au ulimkubali kwa sababu alikubali mimba isiyo yake?
Piga chini mawasiliano na huyo maaluni haraka;
Huku ukimjuza mumeo lakini kama unampenda kweli.

Bazazi
 
nginaeli, Mwambie tu Mimba haikua yake, na mwenye mimba yake alishachukua mtoto wake, Pole sana kwa majaribu haya, Ila Mungu akupe ujasiri maana hata mtoto atayumba kupewa baba wawili tofauti
 
Last edited by a moderator:
ww mdada ni mpole sanaeeh!!
Hivi mtu anakataaje mimba halafu leo analeta ujinga wake hapo!!?,
..natamani ingenikuta mi!!angejuta kunifaham!
..usikubali, usimpe huyo mtt, simamia hayo maamuzi yako
..na hyo mtt bado mdogo utamu affect kisaikolojia kumwambia eti hyo sio baba ake,subiri awe mtu mzima ndo umweleze hali halisi!!
 
Maswali yako gfsonwin sina majibu kwa kuwa sioni mantiki ya mawasiliano yao.
Kwanza sijui ilikuwaje wakaanza kuwasiliana na ili iweje?
Kwa nini mwanamke anayaruhusu mawasiliano hayo?
Kwanini mwanaume (maluuni) hajifungi kibwebwe kumfuata mwanaume mwenzake wayaongee?
Hoja kama hii iliwahi kuletwa JF kama sikosei mwaka 2008:
Ingawa ziko tofauti kidogo;
Ile likuwa mtoto wa katikati (ndani ya ndoa) baada ya mwanamke kuzini.

Anayeweza kuiweka hapa amsaidie dada wa watu asije kuheuka bure?
Ingawa namshauri aachane na huyo maaluni wake asiye na hata chembe ya utu;
Ukatae mimba leo baada ya miaka kadhaa udai mtoto;
Hata hivyo nadhani jibu zuri ni kuwa baada ya kuikataa mimba niliitoa!


@nginaeli kwa nini huitumii elimu yako (Masters) kumaliza kikaango chako?
Je bado unakumbuko mikito ya baba ya mtoto?
Mumeo u nampenda kweli au ulimkubali kwa sababu alikubali mimba isiyo yake?
Piga chini mawasiliano na huyo maaluni haraka;
Huku ukimjuza mumeo lakini kama unampenda kweli.

Bazazi

Wondering down here...kitu km hiki ht sikileti jf namaliza mwenyewe..kwanza jibu 1 hurudii ht kunitafuta....
nimekwambia nina mimba na unajua sana ila tu kujifanya hutaki ujana mwingiii,
...basi nitazaa nitalea,ila tusijuane,..eti baadae unakuja kunambia huo ujinga, hakuna rangi utaacha ona!...kiruuuuuu
 
This is what I'm telling you. YOU DO NOT GIVE HIM HUYO MTOTO, alishindwa na alimkataa, then what. Mwambie huyo mtoto sio wa kwake ikiwezekana. Watu wa namna hii ndo huwa wanasababisha ongezeko la watoto wenye maisha magumu.Nahic aliamua kukuharibia maisha yako, so Kama na mbwai na iwe mbwai

Kumkataa au kutomkataa si hoja. Hoja ni kwamba ni baba yake - biological father. Kwani DNA itasema nini? Mpe mtoto wake kama kuna madai ya matunzo hilo suala lingine.
 
Usimpe kabisa huyo mtoto. Alikutelekeza wewe na mimba yako lakini Mungu si Athumani akakujaalia na kukutana na mume wako ambaye aliamua kukutunza wewe na ujauzito wako kama vile mimba ni ya kwake na amekuwa akifanya hivyo kwa miaka mitano sasa bila kumbagua mtoto huyo hata chembe. Usikubali kabisa kumtoa na kama anataka kufungua kesi mwambie afanye hivyo na mtakutana huko huko mahakamani. Mungu kamnanga hawapati ujauzito sasa ndio anakumbukua kwamba aliitelekeza mimba miaka mitano iliyopita. Pole sana.
 

Siyo sahihi

Kuna tatizo hapo...... hasa kwa huyu bi dada mleta uzi...

1. Anasema huyo bwana alikataa mtoto ikiwa ni mimba ya miezi miwili ...na hivi sasa huyo bwana anamsumbua kwa simu na hata ofisini anafika...tafsiri yake ni kwamba BADO WANA MAWASILIANO

2. Mtoto huyo kwa umri aliofikia sasa anafahamu kwamba baba mlezi ndiye BABA YAKE...fikiria maumivu ya kiakili atakayopata wakati atakapoambiwa kwamba huyo anayemlea kwa sasa siyo baba yake....

3. Huyu mleta uzi inaonesha amechanganyikiwa....unaweza kuliona hilo katika maandiko yake....bado anahisia na huyo MTUNGA MIMBA na mumewe hajui hilo na hawajawahi kulijadili...hilo linajieleza kwa yy kuleta hilo suala hapa kwenye jukwaa...KAA NA MUMEO PERIOD
kama bidada hajabadilisha namba ya simu lazima jamaa atakuwa na namba yake.....kwa hiyo kuwasiliana haikwepeki.....na huyu jamaa kamfwata bidada baada ya kuona ndani ya miaka mitatu ya ndoa yake hajapata mtoto ndo kakumbuka kuna mahali alikataa mtoto ndo mana imebidi amtafute huyo dada......kukaa na mumewe kulijadili hilo swala ni muhimu ila kumbuka walifanya siri kwa wazazi wote kuhusu baba wa huyo mtoto ndo mana nikasema ni vizuri akakaa na mumewe na pia ni kipindi cha wazazi wote kujua ukweli....ili waweze kuwasaidia kwa upande mwingine jinsi ya kulitatua hilo tatizo

binafsi mtoto ndo namwona ana wakati mgumu ingawa hajui lolote....bidada akomae tu amlee huyo mtoto na mumewe kama mwanzo mpaka mtoto akapokuwa mkubwa kiasi cha kuweza kuukubali ukweli na hali halisi na kuvumilia hicho atakachoelezwa...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom