uttoh2002
JF-Expert Member
- Feb 3, 2012
- 14,649
- 26,379
Haifai kabisa kabisa, atakuja msimbua, anasem hivyo Leo lakini akishapata huyo mtoto ataanza demand mambo Mengine, oh mwanangu anataka akuobe, hapati usingizi, mwishowe anamtokea kwa wife, jamaa ataaribu ndoa yake, Mianamke ya hivyo HAIFAI hata kidogo, kwa nini asiolewe? Pumbafu na Aibu ...
Rafiki yangu mmoja jana tukiwa mahali alinipa kisa kinachohitaji mchango wa mawazo yako.
Kuna mrembo mmoja ambaye jamaa alijuana naye kupitia kaka yake(ie kaka wa huyu mrembo na huyu rafiki yangu walikuwa marafiki mpaka wakawa wanatembeleana nyumbani hapo ndo chanzo cha huyu mrembo kumjua huyu rafiki yangu.)Miaka kama 5 imepita bila yule jamaa kuonana na yule dada wa rafiki yake ambaye yeye alikuwa anamchukulia kama ni mdogo wake pia.
Juzi kati ghafla wakakutana Benk na yule mrembo wakaongea kidogo ikiwa ni pamoja na kubadilishana namba za simu.
Ikapita kama siku 4 mara simu ikaita kucheki ni yule mrembo wakaongea kikubwa yule mrembo akamuomba wakutane week end inayofuata.
Ikafika hiyo siku wakakutana wakaongea mengi sana na yule mrembo akatumia fursa hiyo kumweleza jamaa kwamba alikuwa hayupo nchini alienda Uingereza kuchukua Masters yake na ameshajenga nyumba yupo kwake ana gari 2.
Na ana pato zuri tu kwa mwezi.
Huyo Mrembo ndo ana miaka 29 sasa hivi.
Jamaa akafuraia mafanikio aliyofikia kwa kumpa hongera sana.
Yule binti akamwambia "Si nilichokuitia ila naomba usinifikirie vibaya kwani najua wewe ni rafiki mkubwa wa kaka yangu na ninajua una mke,Ninachoomba kwako ni nahitaji kuzaa na wewe kwani nimekuwa nikikupenda kwa mda mrefu sana ila niliogopa kukuambia mpaka ukaja kuoa ninachoomba kutoka kwako ni unipe mimba then mtoto atakaye zaliwa hasikuhusu kabisa kama una ogopa itakuletea shida kwa mkeo.
Na naomba sana usinifikirie vibaya kwani ni ukweli nakupenda sana na ukinikubalia nakuhaidi nitakupa zawadi nzuri sana"
Jamaa akamwambia nipe mda kidogo nifikirie then nitakupa jibu ndo jamaa kanitafuta jana kanipa kisa hiki.
Anaomba mchango wangu pamoja na wako juu ya hili.