Swali zuri, gumu na lenye kuelimisha sana.
(1) Kwa vile una taarifa ya kusudio la mtu kufanya kosa la jinai; una lazimika kutoa taarifa polisi. Ikujulikana kuwa ulikuwa na taarifa halafu hukutoa taarifa polisi unaweza kujikuta unaunganishwa kwenye kesi kama accomplice.
(2) Kisheria rafiki yako anaweza kufanya mauaji hayo na akatoka huru iwapo atamfumania jamaa red-handed akiwa anammegea mkewe na kumwua on the spot. Kuna vifungu vya sheraia anavyoweza kutumia kujitetea na mambo yakaisha. Lakini kwenda kutafuta background information na kupanga mauaji ni kosa la jinai, na iwapo atalitekeleza kwa mkono wake, basi ajue adhabu yake ni kwa yeye mwenyewe kunyongwa hadi afe. Na iwapo atalitekeleza kwa kuajri watu wengine wafanye hivyo, bado atakuwa na kosa la kushiriki na kutekeleza njama za mauaji, jambo ambalo linaweza kumtupa jela kwa miaka karibu 20.
(3) Siku njema huonekana asubuhi. Iwapo mke wake amekuwa anatemebea na mwanamme mwingine ndani ya ndoa kwa miaka minne, ajue kuwa huyo mwanamke hampendi kama mme bali labda yuko pale kwa ajili ya economic protection tu. Alitakiwa awe amejua hilo miaka minne iliyopita na kuachana na ndoa hiyo. Iwapo alisubiri muda weote huo na huenda kuwa amepata watoto basi atakuwa alifanya makosa sana. Ushahidi wa message za huko nyuma zilitosha kudissolve ndoa yao akatafuta mke atakayempenda ki-ukweli.
(4) Kutoka kwa yule anayewindwa tunapata somo kubwa sana hasa kwa vijana wa siku hizi. Kutembea na mke wa mwenzio ni kosa linaloweza kukupotezea uhai wako. Hata kama mmwanamke ni mzuri kiasi gani, na unamzimia sana, epuka kutembea na mke wa mtu ili upate baraka na ujiepushe na balaa. Wanaume hujisikia vibaya sana wanapomegewa na wake zao na wengine wao huweza kufanya maamuzi ambayo huenda yakaondoa uhai wako kama ambavyo jamaa huyu anapanga.
(5) Jamii nyingi za kistaarabu duniani haziruhusu mtu kutembea na mke wa mtu mwingine, na ni utamaduni ulioko hata katika vitabu vitakatifu kwenye Exodus. Unapotembea na mke wa mtu mwingine, siyo kuwa unafanya maudhi kwa mwenye mke tu, bali unakuwa umeudhi jamii nzima, hasa ya walio katika maisha ya ndoa. Unfortunately, mambo hayo yanpotekea yule mwanamke huwa halaumiwi sana bali ni mwanmme ndiye hubeba lawama zote, na hiyo ni natural. Kwa hiyo iwapo utatembea na mke wa mtu bila kujua, jitahidi ujitokeze mbele ya jamii uombe radhi na hasa iwapo ulikuwa hujui kuwa yule mama kaolewa. Na kama ulikuwa unajua, tafuta sababu ya msingi kuonyesha kuwa unajajutia ulilofanya na hutafanya tena. Kujiondokea kimya kimya kama vile huoni tatizo kwa wewe kummega mke wa mwenzio au kuendelea kumega licha ya maonyo unayopewa si njia nzuri na mambo yanaweza kugeuka kuwa mabaya sana dhidi yako; ama directly kutoka kwa uliyemmegea au kutoka kwa watu wengine ndani ya jamii.
Hili linaingia moja kwa moja katika tukio la aina hiyo la wiki tatu zilizopita kuhusu Diamond kummega Uwoya, halafu Ndikumana kuzirai baada kusikia kamegewa, na baada ya hapo Diamond kutojali kabisa na wala kutoongelea kabisa tukio hilo. Nadhani Diamond hakupata mshauri mzuri sana wa ku-handle situation ile hasa kwa vile inahusu celebrities; kimsingi alitakiwa atamke mara moja kujutia tukio hilo na hasa aonyeshe kuwa hakujua Irene alikuwa bado ndani ya ndoa yake na Ndikumana, kisha akaomba radhi kwa Ndikumana na jamii yote kwa yaliyotokea, akimalizia na kukemea vitendo vya ngono nje ya ndoa.