An open letter to President Magufuli

An open letter to President Magufuli

aanzishe pia utaratibu wa kuhimiza watu kudai risiti ambapo anaweza kuanzisha utaratibu wa kutoa motisha kwa mtu mwenye risiti nyingi mf ukiwa na risiti mia za manunuzi moja italipiwa na serikali
 
I agree chidou.

The will of the people must be respected. That's why there ought to be a referendum on the issue of Zanzibar and Tanganyika. The people must decide and legalize this union, not the politicians.

I do believe Magufuri he can, but ccm can not. Where Magufuli exams come,That why he requested prayers from goodwill Tanzanians. Unless we are going to loss him soon.
 
Last edited by a moderator:
Niseme machache

1.Ushauri wako mzuri ila si yote lazima Magufuli afanye ni kumwonea.

Mfano maswala ya kubadilisha sheria za kodi au sheria yoyote uliyoshauri ni kazi ya bunge sio Magufuli sheria hizo kazikuta.Njia bora ni kupeleka mashauri kama hayo kwa mbunge wako ili akalianzishe bungeni walijadili huko.Hoja za sheria zianzie kwa wabunge msimpelekee Magufuli.Wabunge wenu wanaokula sitting allowance kila siku ndio kazi yao

Kwa hiyo maswala ya VAT,Kupunguza au kuondoa kodi,uraia wa nchi mbili,maswala ya referendum ya muungano yote hayo ni maeneo ya kujadiliwa bungeni shauri wabunge wako walibebe waende nalo bungeni msisimamishe msafara wa magufuli kwenye hayo.Sheria za mambo hayo hatungi Magufuli

2.Niseme machache kwa baadhi ya Mambo

-Umeshauri watu wa nje kuingia bila visa.Hilo lipo ila ni kwa wale watokao kwenye nchi tunazojua wanaongeza thamani kwa nchi yetu sio wazururaji wanaotafuta Ardhi,kuhamia au ajira koko nchini mwetu au kuja kufanya ujambazi na utapeli.MMarekani,watu toka ulaya wenye pesa zao hupatia visa airport wakati wanigeria inabidi kwanza tuelewane kama wapewe visa au wasipewe.

-Pia umeshauri wasomi sana wa nchi zingine waruhusiwe tu kuingia!!! Wamesoma nini? Hicho walichosoma Tanzania wasomi wa aina hiyo tunao au hatuna? Hicho walichosoma kitatusaidiaje watanzania? Ana ADD VALUE GANI KWA KUJA NCHINI?
Kuna fani kibao wasomi hao huingia lakini kwa kusudi maalum.Mfano unakuta vyuo vikuu labda havina profesa wa Nuclear lazima atatafutwa toka nje na ataingia bila shida.Kuna wasomi wamesoma sana ma-phd kibao ya mambo ya ngojera na maigizo unataka turuhusu tu waje?
 
Mkuu Bavaria,

Hilo wazo ni muhimu sana. Mara nyingi, wafanyabiashara wanaonekana kama adui wa maendeleo. They are guilty until proven innocent. Wawekezaji wa nje wanasaidiwa kwa kila kitu, lakini wa nyumbani wanadharauliwa. TRA wanasumbua sana wafanyabiashara WOTE, hata kama ni mlipa kodi wa kweli.
 
Mkuu Abunuas,

Siyo raia wote wanaweza kupata visa uwanja wa ndege. Miaka mingi tunawabagua kwa mfano raia wa Afrika na kuwapendepea raia wa ulaya. Hatuangalii nani ni tajiri au masikini. Tuwe kama Malaysia. Hawajali umetoka wapi, ili mradi una fedha za kutosha, raia wa zaidi ya nchi 160 wanapewa visa uwanja wa ndege. Mwaka huu, Indonesia imefuata. Japan mwaka jana, kwa mara ya kwanza, imeruhuhusu raia wa nchi za kimasikini za Asia kupata visa uwanja wa ndege. Leo maduka yao yamejaa watalii wa China. Leo naweza kula chakula cha HALAL mjini Tokyo, nashukuru watalii wa Indonesia na Malaysia, waliolazimisha huduma hii.
 
Last edited by a moderator:
Tokyo40, Mr president has good will with our nation, the Greatest obstacles his ruling party. Before doing those mentioned he must bring back Warioba constitution
the one who kata mtama Warioba has given chance to be district commisioner Kinondoni.you can imagine
 
Mkuu PHYLOSOPHER,

Ni wazo zuri sana.

Utamaduni wa kukwepa kodi upo miaka mingi, na ni watu wachache ambao wanalipa kodi kihalali Tanzania. Huo ndio ukweli. Tatizo lipo kwenye kodi na ushuru mkubwa, pamoja na umasikini. Raisi akishusha kodi na ushuru, itakuwa rahisi kwa mfanyabiashara kuuza mali yake kwa faida. Ukiwauliza, wateja 10, kama wanataka risiti pamoja na VAT, 9 watanunua vitu bila risiti, kukwepa kodi ili kupunguza gharama za maisha. Tanzania ni nchi masikini, lakini kodi ya mauzo ni sawa na ya nchi tajiri. Hapo unakaribisha rushwa tu na ukwepaji wa kodi.
 
Last edited by a moderator:
Namba kumi sikubaliani nayo! Kwani imekosa pointi za kutetea!
 
Tokyo umesema vizuri.
Kuna eneo moja sikubaliani nalo in like LA kodi Kwa biashara zinazopata FAIDA ya chini ya mil 4 Kwa mwezi. Hii in mil 48 Kwa mwaka. Hili ni pato kubwa sana kuto kutozwa kodi labda kama ulimaanisha mil 4 Kwa mwaka. Pia ubapozungumzia FAIDA Kwa biashara ndogo kuna tatizo kubwa LA kukokotoa faida halisi ya biashara ndogo ambazo nyingi mahesabu take in changamoto. Mpaja sasa nyingi zinakadiriwa Kofi Kwa kutumia mauzi(turnover)
 
Yaani Kingereza chako ni kichanga saana, una point ila hujui kingereza sijui kwa nini hukuandika tuu kiswahili. Ni nani alikudanganya kuwa unafahamu kingereza? sijawahi kuona kingereza kibovu hivi duniani, umejaribu ila huna vocablary za kutosha kitu ambacho kimekufanya uafnye direct translations.

Kwa kuwa sisi waliowengi tuko interested na ujumbe uliomo ndani na siyo vocabulary tumemuelewa sanaa.
 
How could he reform courts while it is the corrupt judge (Mr Lubuva) who brought him in power!!!
 
Hili ni andiko zuri sana, hivi haiwezekani tulituma ikulu ofisini kwake kwa email au other means?
Apeleke kwa mbunge wake apeleke hayo aliyosema bungeni wakayajadili huko.Raisi hawezi badili sheria yoyote iwe ya kodi,uhamiaji,uraia nchi mbili,VAT,UWEKEZAJI NK.Msimsumbue Raisi
 
Yaani Kingereza chako ni kichanga saana, una point ila hujui kingereza sijui kwa nini hukuandika tuu kiswahili. Ni nani alikudanganya kuwa unafahamu kingereza? sijawahi kuona kingereza kibovu hivi duniani, umejaribu ila huna vocablary za kutosha kitu ambacho kimekufanya uafnye direct translations.
Acha Mkuu, kingereza ?nakijua. Unataka kusema wanaoandika "Habali, akuna" hawajui kiswahili? JPM akisoma barua ya Kiingereza atamuelewa zaidii kuliko hiyo ya Kiswahili. Cc Tokyo40
 
Last edited by a moderator:
I do believe Magufuri he can, but ccm can not. Where Magufuli exams come,That why he requested prayers from goodwill Tanzanians. Unless we are going to loss him soon.

Umeandika lugha gani? Andika kiswahili hujui kingereza kabisa.
 
Hili ni andiko zuri sana, hivi haiwezekani tulituma ikulu ofisini kwake kwa email au other means?

Andiko lina mapungufu kibao, mjeshimiwa awezi soma uchafu huu unaobeba wahamiaji wakati raisi anataka apambane na hilo.
 
BARUA YA WAZI KWA MHESHIMIWA RAISI MAGUFULI

Ndugu Mheshimiwa Raisi Magufuli,


Kama Watanzania wengi, nakupongeza kwa kazi yako ya kuwafuata na kuwashughulikia ipasavyo wakwepaji kodi na wala rushwa serikalini.

Hata hivyo, ili kuwafanya Watanzania walipe kodi kwa hiari na kupunguza rushwa, inabidi mageuzi makubwa ya kiuchumi na YA kisiasa yafanyike na kutekelezwa haraka iwezakanavyo.

Napendekeza yafuatayo kwa serikali yako:

1. Punguza VAT iwe ASILIMIA 10
Upunguzaji wa VAT utasaidia na kuchochea uchumi kwa kufanya bei ya vitu rahisi kwa wananchi wenye uwezo mdogo.

2. Ondoa kodi ya mapato kwa wafanyazazi wenye mshahara wa chini ya milioni moja kwa mwezi na kwa wafanyabiashara wanaopata faida chini ya milioni nne kwa mwezi. Hii itawasaidia wananchi wa hali ya chini kuzidisha matumizi na kuwasaidia kulipa gharama kubwa ya maisha. Hii pia itawafanya wafanyabiashara wadogo kulipa kodi kitiifu zaidi bila ya kuumiza mitaji yao ya biashara, na pesa inayobaki wanaweza kuzidishia katika uwekezaji wao.

3. Punguza kodi kwa wafanyabiashara. Kodi kubwa bila ya kufanywa marekebisho kulingama ma hali ya uchumi wa nchi, ni sababu kubwa ya zaidi ya asilimia 99 ya wafanyabiashara kukwepa kodi. Hali ngumu ya maisha pia inawafanya wafanyakazi wa serikali kuomba rushwa ili walipe gharama za maisha. Kodi kubwa pia inawahamasisha wafanyabiashara kutoa rushwa ili kupunguza gharama za bidhaa zao, hasa wakati mgumu wa kibiashara.

4. Anzisha mageuzi katika sekta ya wafanyakazi wa serikali. Wachapa kazi walipwe zaidi na kupandishwa chea haraka. Wavivu wa kazi wafukuzwe kazi, wala rushwa wapelekwe mahakamani na kuadhibiwa kwa kifungo kirefu. Mishahara mikubwa kwa wafanyakazi wa serikali pia itasaidia kupunguza rushwa kwa kuwa watakuwa na uwezo wa kukabiliana na hali ngumu ya maisha.

5. Zidisha kiwango cha mshahara wa chini kifike 500,000 kwa mwezi. Watanzania wengi kwa sasa wanashindwa hata kula milo mitatu kwa siku, sembuse kulipa ada za shule na kodi ya nyumba kwa mshahara wa sasa. Kiwango hiki cha chini pia kiwe mshahara wa wafanyakazi wa nyumbani, ambao kwa miaka mingi wananyanyaswa kwa kutopewa mshahara wa kima cha chini.

6. Fanya mageuzi katika mfumo wa mahakama
Kuna vibaka wengi wapo jela zaidi ya miaka mitatu wanasubiri hukumu zao. Hawa ni Watanzania wasio na uwezo wa kutoa rushwa wala dhamana. Naomba uwatoe jela kwa kuwa makosa yao ni madogo madogo na wameshaadhibiwa vya kutosha jela. Kama adhabu, vibaka wapewe adhabu ya kusafisha nyumba na ofisi za serikali, kuokota taka mjini au wapewe adhabu nyingine. Pia, jela zimejaa wafungwa na nafasi ni ndogo mno. Wakipewa adhabu ya nje, itapunguza idadi kubwa ya wafungwa. Pia, wajengee vyoo vya kutosha. Ni aibu kwa taifa, kutofanya hivyo.

Mahakimu wasiruhusiwe kuhairisha kesi bila sababu maalumu. Kesi lazima zisikilizwe haraka ipasavyo na hukumu zitolewe haraka ili kukinga haki za wananchi. Mara nyingi kesi ndogo zinachukua hata miaka mitano.

Pia, tunaomba serikali iiheshimu na kufuata hukumu za mahakama na isiingilie kazi zake kama inavyosema katiba ya nchi. Mara nyingi serikali za awamu za nyuma zilidharau hukumu za mahakama. Hii inaipa sura mbaya nchi, siyo tabia ya kidemokrasia na haionyeshi kuwa nchi imekomaa kidemokrasia.

Kabla ya kuleta mahakama maalum za kuwahukumu wawekpa kodi, wala rushwa na mafisadi wengine, fanya mageusi kwanza. Ni tabu mno kwa mwananchi wa kawaida kupata haki yake mahakamani. Hukumu zinachukua mna mwingi kupita kiasi na mahakama zetu zinanuka rushwa. Siyo tu, mwananchi wa kawaida ananyimwa haki yake, pia, hali hii inawakata tamaa wawekezaji. Ni hasara kwa mfanyabiashara, kusubiri hukumu kwa muda usiojulikana kama kuna ugomvi wa kibiashara. Pesa za mtaji zinakwenda kutafuta haki, mwishowe watu wanafukuzwa kazi kupunguza gharama. Hasara hapa siyo ya mfanyabiashara peke yake, bali ya serikali kukosa kodi na ya mfanyakazi kukosa ajira.

7. Ruhusu wageni / watalii wa nchi nyingi zaidi waingie Tanzania kwa viza ya uwanja wa ndege. Hii itasaidia kuleta wageni zaidi bila ya kuomba viza katika ubalozi wetu. Serikali itapata fedha za kigeni zaidi na kuzalisha ajira zaidi.

8. Anzisha viza maalum kwa ajili ya wastaafu wa kitajiri. Wataleta pato la kigeni, ajira na kodi.

9. Ruhusu raia wa kigeni wenye kisomo cha juu kufanya kazi na kuishi Tanzania. Watoze ada. Hii italeta wasomi wenye elimu ambayo ipo pungufu au hamna kabisa Tanzania. Pia, italeta ajira na fedha za kigeni nchini.

10. Ruhusu uraia pacha.

11. Waelekeze maofisa wa posta wasitutoze kozi tukipokea mizigo kwa njia ya posta kama ni kwa ajili ya matumizi binafsi. (Chini ya thamani ya laki tatu). Toza ushuru mdogo kwa watumiaji wa posta ili wafanyabiashara wadogo wenye mtaji mdogo waweze kuagiza mali kutoka nje na kuuza kwa faida. Hii itaikuza biashara ya mitandao, itatoa ajira na kodi kwa serikali. Pia, wafanyabiashara wadogo hawatalazimika kutumia makontena ya gharama kubwa.

12. Wape moyo wazalishaji wa ndani kwa kuwatoza ushuru usioumiza biashara na faida na kwa kupunguza aina mbalimbali ya leseni na vibali na kodi tofauti tofauti. Warahisishie kazi kwa kuwapatia huduma zote sehemu moja, kama wanavyofanyiwa wawekezaji wa nje. Kodi isiwe ya kukomoana bali ya kujenga taifa na biashara za nyumbani.

13. Weka kodi kubwa kwa vitu visivyo na haja kubwa kwa jamii ili kukuza uchumi wa nyumbani na kusalimisha fedha za kigeni kutumiwa nje. Pia, vitu kama matunda ya Afrika Kusini au juisi, hatuvihitaji. Weka ushuru mkubwa ili wakulima wao waje kulima kwetu au Watanzania wale matunda ya nyumbani zaidi kusaidia wakulima wetu.

14. Kwa kuwa usafiri ni bado matatizo, Watanzania wengi wanategemea magari kwa usafiri. Kwa sasa, ushuru mkubwa unaotozwa na serikali unasaidia kuzidisha rushwa nchini. Ningependekeza ushuru wa gari uwe asilimia 25 kwa gari jipya na asilimia 35 kwa gari lililotumika sio zaidi ya miaka 10, kwa ukubwa wowote ya injini ya gari. Hii itawasaidia Watanzania wa hali ya kati wenye uwezo wa kununua gari kupata usafiri wa maana na serikali itaweza kuwatoza kodi ya barabara na ya usalama/ukaguzi wa gari kila mwaka.Hapa unaweza kutoza kodi kutokana na ukubwa wa injini na kuingiza kodi kati ya laki mbili mpaka milioni moja kwa kila gari, kila mwaka.

15. Ruhusu wananchi wa Zanzibar na Tanganyika wapige kura ya maoni ili wafanye maamuzi ya kutaka au kupinga umoja wetu. Nadhani wananchi wengi wanaupenda umoja na kura ya kutaka umoja itashinda. Lakini, hapa watakuwa wameombwa rasmi maoni yao kuhusu huu umoja. Tukirihusiw akupiga kura ya maoni, itaonyesha dunia kuwa tumekomaa kidemokrasia na tumetaka au tumekataa huu umoja wetu.


Mheshimiwa Raisi, nategemea mapendekezo yangu yatasaidia kidogo serikali yako. Nina uhakika watakuja wachangiaji wengine wa JF na kukupa mapendekezo yao pia. Tunachotaka sisi wananchi ni nchi iliyo na uchumi mzuri, imara, yenye nguvu na amani.

Nakutakia kila la kheri katika serikali yako.

Wako Mtiifu,

Tokyo40

The East African customs protocol is an obstacles on reducing VAT and other tax tariffs
 
Back
Top Bottom