Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
Amwaga fedha kumpoza msichana wake wa kazi | |
Monday, July 04, 2011 10:59 AM BAADA kutoweka nyumbani kwake kwa takribani siku nne kukimbia dhahama aliyemsababishia msichana wake wa kazi imedaiwa bosi huyo amekwenda kumuangukia dada wa msichana wake na kumwagia fedha ili waweze kuyamaliza kimnya kimnya. | |
Mwanamdke huyo aliyetambulika kwa jina la Mama Mudy alimsababisha kubakwa kwa msichana wake wa kazi za ndani aitwae Grace [17] baada ya kumfukuza usiku kwa sababu ya kuchelewa kurudi katika ajira yake hiyo Imedaiwa kuwa, mwanamke huyo alitoroka usiku huo kwa kuogopa mahojiano kati yake na polisi na kutoweka nyumbani kwake hapo kwa takribani siku nne mfululizo Hata hivyo imedaiwa kuwa mwanamke huyo alitinga nyumbani kwa dada huyo kwa lengo la kutaka kuyamaliza kiundugu na kukiri kosa hilo na kuahidi kumsaidia msichana huyo na kumtaka dada huyo kutaja kiasi cha fedha anachokihitaji ili aweze kuyamaliza Hata hivyo imediwa kuwa dada binti huyo hakuhitaji fedha hizo na kuhofia afya ya mdogo wake huyo na bosi huyo kukiri kuwasaidia endapo atagundulika endapo atagundulika kama atakuwa na ujauzito Imedaiwa kuwa dada wa binti huyo alitaka kwanza kujua hatma ya afya ya mdogo wake ili mengine yafate baada na kudaiwa alikubali kupokea kwanza kiasi cha shilingi laki tano na kuahidiwa kiasi kingine kama hicho leo ili aweze kufuta kesi hiyo Chanzo cha habari kilidai kuwa, dada huyo anatarajiwa kupatiwa kiasi hicho leo mbali na hicho alichopewa na haijafahamika kama anamtega bosi huyo ama la |