Amsterdam 2025

Mleta mada amemaanisha upinzani wana mtindo wa kurudia makosa since 1995 yani wanajua hakuna Tume Huru ila bado wanashiriki na matokeo wanajua yatakuaje yani kufanya kitu kile kile kila wakati(kosa la kushiriki chaguzi isiyo na tume huru) then kutegemea kushinda kitu ambacho wamekirudia tena na tena miaka nenda rudi!

My take:
Huu ndio muda upinzani wanahitaji kufanya mageuzi kuliko wakati wowote ule yaliyojitokeza mwaka huu lazima waanze vuguvugu la katiba mpya mimi sitotoa support yangu kwa upinzani tena wakikubali kushiriki igizo kama la mwaka huu 2025
 
Inawezekana kama atachukuwa uraia wa tanzania,tatizo CCM ni chama chenye ubaguzi wa ndani kwa ndani waislamu na wakiristo wanalifahamu hilo,kina udini uliojificha,kina ukabila uliojificha linapokuja suala la kugombea, tunakumbuka yaliyomkuta Salim Ahamed Salim, lile ni jambo baya sana na lipo ndani ya CCM.

Tuone Rais anayekuja kama atakuwa Muislamu ili tufahamu utaratibu waliokuwa nao CCM, labda Samia Suluhu ambae ni Mzanizbari mwenye asili ya kinyamwezi. Jina Suluhu asili ni unyamwezini labda sijui historia vizuri.
 
Natoa pendekezo...

Kwa jinsi makamanda wanavyomhusudu huyu bwana...
Kweli kabisa maana platform ya Lissu 2020 ilikuwa ni matobo ya risasi wakati ya Amstersam 2025 itakuwa the Hague.The Hague tuliisikia toka 2015 kwa akina Mnyika (muflisi wa kisiasa) kwamba JK atapelekwa the Hague.

Hawa ndugu zangu wapinzani wengine wana miili mikubwa kwelikweli lakini vichwani mwao ni seti tupu.
 
Natoa pendekezo...

Kwa jinsi makamanda wanavyomhusudu huyu bwana...
Nadhani badala ya kujikita kumtaka ndo agombee tungejikita kujiuliza why ndani ya nchi yetu hatuna platform ya watu kuweza kudai haki yao pale wanapohisi mchakato wa uchaguzi wa rais haukuwa wa haki kwako.
 
Nadhani badala ya kujikita kumtaka ndo agombee tungejikita kujiuliza why ndani ya nchi yetu hatuna platform ya watu kuweza kudai haki yao pale wanapohisi mchakato wa uchaguzi wa rais haukuwa wa haki kwako.
Kweli mkuu, wazo zuri sema litapingwa na wengi.
 
Hata kama Chadema hawatafanikiwa Kwa lolote..
Au huyo Amsterdam asifanikiwe lolote...
Hivi kwanini huwa mnahisi ya kuwa Watanzania wote wanahusudu Demokrasia ? Hili ni kosa kubwa sana, bali mnatukosea sana sisi wengine ambao tunaona ya kuwa Demokrasia ni ushetani na ni utumwa wa kujitakia.

Rekebisha kauli yako, kama kweli wewe ni mkweli.
 
Mnafiki katika ubora wake , Mara moto , Mara baridi , Mara akosoe Mara aponde , Hana msimamo Kama waccm wote walivyo .
 
Yeyote yule mtetea HAKI za wanyonge ni adui wa CCM. kosa la Amsterdam ni kukubali kwake kumtetea kisheria Tundu Antipas Lissu aliyepigwa risasi zaidi ya 30 ili aweze kupata HAKI zake kama mtanzania.


CCM walitaka Lissu arejee nchini bila usaidizi wowote ule wa kisheria duniani, nafikiri wote mnajua ni kipi ambacho kingekuwa kimeshampata so far.
 
Natoa pendekezo...

Kwa jinsi makamanda wanavyomhusudu huyu bwana.

Napendekeza 2025 ndo awe mgombea wa urais kupitia CHADEMA.

Naamini akigombea kwa platform ya kumshitaki Rais Magufuli huko The Hague, atajizolea kura nyingi sana.

Makamanda mnasemaje? Twende na Amsterdam 2025?

Sheria inaruhusu asiye raia kugombea?
 
Yeyote yule mtetea HAKI za wanyonge ni adui wa CCM. kosa la Amsterdam ni kukubali kwake kumtetea kisheria Tundu Antipas Lissu aliyepigwa risasi zaidi ya 30 ili aweze kupata HAKI zake kama mtanzania.


CCM walitaka Lissu arejee nchini bila usaidizi wowote ule wa kisheria duniani, nafikiri wote mnajua ni kipi ambacho kingekuwa kimeshampata so far.

Kingempata rejea kauli ya mtoto wa dada
 
Back
Top Bottom