Amri itoke magari yatumie gesi

Amri itoke magari yatumie gesi

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,252
Reaction score
16,170
Tanzania inayo gesi nyingi lakini uagizaji wa mafuta bado uko juu. Hela nyingi za kigeni bado zinahitajika kuagiza mafuta.

Kwanini Tanzania tusifanye maamuzi magari magumu ya kubadilisha magari yote hasa yake madogo nchini kuanza kutumia gesi yetu badala ya mafuta ya petrol?

Tunaweza kuanza na miji mikubwa Kama Dar, Tanga, Dodoma, Mwanza na Arusha Kama pilot.

Bila kufanya hivyo athali za CORONA zitatusumbua sana kwa miaka mingi.
 
Wazo zuri lakini naona kama ni future imposibble tense kwa TZ.

Coz kama tu vyuo (walipo elites na professors) vilishindwa kuendeleza masomo yao angali wanachuo wengi wana smartphone na computer kwa kutumia technology rahisi tu kama zoom meeting, Je kweli tutaweza kufanya hii transition ya gasoline/diesel to gas kwenye magari
 
Tanzania inayo gesi nyingi lakini uagizaji wa mafuta bado uko juu. Hela nyingi za kigeni bado zinahitajika kuagiza mafuta.

Kwanini Tanzania tusifanye maamuzi magari magumu ya kubadilisha magari yote hasa yake madogo nchini kuanza kutumia gesi yetu badala ya mafuta ya petrol?

Tunaweza kuanza na miji mikubwa Kama dsm, tanga, Dodoma, mwanza na Arusha Kama pilot.

Bila kufanya hivyo athali za CORONA zitatusumbua sana kwa miaka mingi.
Tunakaribia kushindwa kutumia gesi yetu kwani magari ya umeme yanakuja kwa kasi ni ndani ya miaka 10 tu yatatawala. Pia huwezi kuanza kutumia gesi kwenye magari kabla ya kui liquify iwe kimiminika. Huo ni uwekezaji wa matrilioni.
 
Tunakaribia kushindwa kutumia gesi yetu kwani magari ya umeme yanakuja kwa kasi ni ndani ya miaka 10 tu yatatawala. Pia huwezi kuanza kutumia gesi kwenye magari kabla ya kui liquify iwe kimiminika. Huo ni uwekezaji wa matrilioni.
Magari ya umeme yaje, na yale yetu yatumie gesi.
 
Kama Tanzania tutaendelea kuwa viongozi wazee kwenye wizara, mashirika, boards na vyuo maendeleo yatakuwa ndoto ya mchana.

Wazee wetu Hawa tuwaache wakapunzike wapate muda wa kutushauri kutokana na uzoefu wao badala ya kuwa watendaji wakuu na watoa maamuzi. Mara nyingi wazee ni watu wanaojisikilizia afya zao kila siku wanapoamka na kulala. Itategemea Leo wameamkaje mifupa, macho, pressure, kisukari, nyonga, na misuli yao.
 
Magari ya umeme yaje, na yale yetu yatumie gesi.
Ni kwa vile jiwe hashauriki ningemshauri kitu fulani cha msingi na tungeepuka kupoteza matrilioni kwenye gasi liquefaction, bomba la Uganda-Tanzania, Nyerere hydroelectric project nk. Otherwise tutapigika kimamba.
 
Tanzania inayo gesi nyingi lakini uagizaji wa mafuta bado uko juu. Hela nyingi za kigeni bado zinahitajika kuagiza mafuta.

Kwanini Tanzania tusifanye maamuzi magari magumu ya kubadilisha magari yote hasa yake madogo nchini kuanza kutumia gesi yetu badala ya mafuta ya petrol?

Tunaweza kuanza na miji mikubwa Kama dsm, tanga, Dodoma, mwanza na Arusha Kama pilot.

Bila kufanya hivyo athali za CORONA zitatusumbua sana kwa miaka mingi.
Hadi sasa LPG-Gas ya kwenye mitungi ya kupikia bado tunaagiza nje ... Je ya magari tutafika lini?

Sina hakika na mabeberu watakacho tufanyia
 
Hadi sasa LPG-Gas ya kwenye mitungi ya kupikia bado tunaagiza nje ... Je ya mgari tutafika lini?

Sina hakika na mabeberu watakacho tufanyia
Tusipoamua Sasa tutaamua lini, hili sio jambo la mtu mmoja. Kama tusiposema leo gas yetu, chuma chetu, bahari yetu na rasilimali zetu nyingine zitunufaisheji leo leo basi wageni watatuamulia kesho. Je, watu tuliowaweka serikalini, bungeni na kwenye mahakama zetu wanatufikisha tunakokwenda kwa speed ya dunia inakoelekea?
 
Mkuu gesi umeenda mbali. Viwanda vya magar vinauwezo wa kutengeneza magari ya kutumia umeme ambayo ni self or solar charging. Ila shida inakuja kwenye soko la mafuta. Hii ni biashara ambayo matajiri wanamkono mrefu sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kuna mtambo wa kujaza gesi pale ubungo maziwa, watu wanaofanikiwa kufungiwa magari yao wanahangaishwa kujaziwa gesi hadi wengine wanatamani wafungue hiyo mitungi. Wanadai hawawezi kukujazia hadi uwe na kibali, ukienda kufuatilia kibali na kwenyewe unazungushwa

Mara anayetoa vibali kasafiri nje ya nchi, mara utaambiwa ithibati yake ya kuruhusiwa kutoa vibali ime-expire ili mradi usumbufu wa hapa na pale. Wanaoweza kutoa virushwa vya hapa na pale kwa wale wanaojaza ndo wanajaziwa bila mgogoro.

Nilichogundua kingine hii project ya gesi kwenye magari inapigwa vita na wafanyabiashara ya mafuta na wanaweza hata kuishawishi serikali kwamba ndo walipaji wakubwa wa kodi....
 
Mkuu gesi umeenda mbali. Viwanda vya magar vinauwezo wa kutengeneza magar ya kutumia umeme ambayo ni self or solar charging. Ila shida inakuja kwenye soko la mafuta. Hii ni biashara ambayo matajiri wanamkono mrefu sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata umeme na wewe umeenda mbali pia ikiwa zile pikipiki za kuchaji kwa umeme haziwezi hata kupanda mlima izo gari itakuwaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu gesi umeenda mbali. Viwanda vya magar vinauwezo wa kutengeneza magar ya kutumia umeme ambayo ni self or solar charging. Ila shida inakuja kwenye soko la mafuta. Hii ni biashara ambayo matajiri wanamkono mrefu sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaongelea matoy ya watoto nini, hata huko Marekani na Ulaya hizo gari hazipo
 
Tusipoamua Sasa tutaamua lini, hili sio jambo la mtu mmoja. Kama tusiposema leo gas yetu, chuma chetu, bahari yetu na rasilimali zetu nyingine zitunufaisheji leo leo basi wageni watatuamulia kesho. Je, watu tuliowaweka serikalini, bungeni na kwenye mahakama zetu wanatufikisha tunakokwenda kwa speed ya dunia inakoelekea?
Kwanini serikali iliamua kujenga mfumo wa bomba kwanza?

Serikali inapambana na kuzuia uchomaji mkaa mitipori ambayo inategemewa sana na jamii. .. Mfano kule mbalali wananchi kucha wanapambana na migambo wananyang'anywa mikaa lakini bado wanaendelea

Kwanini wasinge tangulia kuchakata ya kuweka kwenye mitungi na bei zikapungua ....

adha ya mkaa ikapungua?
 
Unaongelea matoy ya watoto nini, hata huko Marekani na Ulaya hizo gari hazipo
Yqan unamaanisha gari za solar na kuchaji hazipo???

Mbona hio kitu iko kawaida sana siku hivi. Fatilia Ford na Tesla wanatengeneza high-performance cars zinazotumia umeme
 
Kwanini serikali iliamua kujenga mfumo wa bomba kwanza?

Serikali inapambana na kuzuia uchomaji mkaa mitipori ambayo inategemewa sana na jamii. .. Mfano kule mbalali wananchi kucha wanapambana na migambo wananyang'anywa mikaa lakini bado wanaendelea

Kwanini wasinge tangulia kuchakata ya kuweka kwenye mitungi na bei zikapungua ....

adha ya mkaa ikapungua?
Nasikia ile ya kwenye mitungi ya kupikia lazima itokane na mafuta ya petroleum, wataalamu wetu humu watatujuza
 
Yqan unamaanisha gari za solar na kuchaji hazipo???

Mbona hio kitu iko kawaida sana siku hivi. Fatilia Ford na Tesla wanatengeneza high-performance cars zinazotumia umeme
Zipo lakini hata huko majuu bado gari za hivyo ni 0.000008% ya magari yote duniani. Mengi bado Ni matoy ya kuchezea watoto.

Sisi watanzania kwakuwa tunayo gesi hata ya umeme yakija tubaki kwenye gesi yetu badala tena ya kuagiza batteries zake kutoka Japan na ujerumani. Tuwape uwezo nyumbu watengeneze magari na matrector yetu wenyewe kwa kutumia chuma chetu Cha liganga na mchuchuma na makaa ya mawe kuyeyushia chuma na gesi yetu kuendeshea magari yetu.
 
Back
Top Bottom