Sakasaka Mao
JF-Expert Member
- Sep 29, 2016
- 9,911
- 11,779
Katika kikao cha Dpp kilichoitishwa Ikulu leo ili kuwasilisha idadi ya maombi ya watuhumiwa walioandika barua ya 'marejesho' ili wajinasue imemshangaza rais!
Hii imetokana na mwitikio mkubwa wa watuhumiwa kuandika barua kwa Dpp za kuomba msamaha na kurejesha fedha walizotuhumiwa kukwapua.
Amesema hakutegemea kusikia idadi ya watuhumiwa 467 waliopokelewa maombi yao na wengine ambao barua zao zimechelewa kuwasilishwa kutokana na sababu mbalimbali, wote hao wamechangamkia hiyo fursa adhimu.
Kaeleza huo 'mchezo' hautaendelezwa baada ya siku ya leo, kuendelea mbele, watakao ucheza sasa wataibeba misalaba yao kupitia mahakama.
Hautatolewa tena msamaha 'kabila hiyo' na wote watakao bainika sasa watabanwa moja kwa moja na sheria za mafisadi na wahujumu uchumi zilizopo.
Kasema kuwa kama mtu anapotoshwa aidha na mawakili ili aendelee kukamuliwa pesa, shauri yake.
Nafasi hii ya kupitishwa kwenye tanuri la moto na kisha kutokea kwenye tundu la sindano ni moja na ni ya mwisho.
Kweli nchi hii ilikuwa na wapigaji jamani!
Hivi ukiwapanga foleni kuanzia posta, si watafika hadi station kabisa, Dah!
Tunawatakia msamaha mwema na wenye kuleta maridhiano.
Hii imetokana na mwitikio mkubwa wa watuhumiwa kuandika barua kwa Dpp za kuomba msamaha na kurejesha fedha walizotuhumiwa kukwapua.
Amesema hakutegemea kusikia idadi ya watuhumiwa 467 waliopokelewa maombi yao na wengine ambao barua zao zimechelewa kuwasilishwa kutokana na sababu mbalimbali, wote hao wamechangamkia hiyo fursa adhimu.
Kaeleza huo 'mchezo' hautaendelezwa baada ya siku ya leo, kuendelea mbele, watakao ucheza sasa wataibeba misalaba yao kupitia mahakama.
Hautatolewa tena msamaha 'kabila hiyo' na wote watakao bainika sasa watabanwa moja kwa moja na sheria za mafisadi na wahujumu uchumi zilizopo.
Kasema kuwa kama mtu anapotoshwa aidha na mawakili ili aendelee kukamuliwa pesa, shauri yake.
Nafasi hii ya kupitishwa kwenye tanuri la moto na kisha kutokea kwenye tundu la sindano ni moja na ni ya mwisho.
Kweli nchi hii ilikuwa na wapigaji jamani!
Hivi ukiwapanga foleni kuanzia posta, si watafika hadi station kabisa, Dah!
Tunawatakia msamaha mwema na wenye kuleta maridhiano.