Ndugu zangu,
Ama kweli hii dunia tunapita, binamu yangu wa kiume kapata mchumba, tukamsindikiza kuvalisha Pete na kutoa kishika uchumba, hiyo sherehe ndogo ikafaana kweli kweli, tukala na kunywa tani yetu, shemeji yetu alikua mjamzito pia,
Wiki iliyopita amepaki gari pembezoni mwa barabara kuu, anavuka barabara kwenda upande wa pili kununua matunda aliyokua anayapenda, ghafla kagongwa na gari kafariki [emoji24][emoji24]
Sehemu ile ile tuliyofanyia sherehe ndiyo hiyo hiyo tuliyofanyia msiba, unatamani kupiga hata yowe hadharani, unabaki kujikaza kiume, binamu nae kachanganyikiwa
Haya maisha haya , haya maisha haya, acheni tu, dada wa watu ndo kafa hivi kweli?
Ama kweli hii dunia tunapita, binamu yangu wa kiume kapata mchumba, tukamsindikiza kuvalisha Pete na kutoa kishika uchumba, hiyo sherehe ndogo ikafaana kweli kweli, tukala na kunywa tani yetu, shemeji yetu alikua mjamzito pia,
Wiki iliyopita amepaki gari pembezoni mwa barabara kuu, anavuka barabara kwenda upande wa pili kununua matunda aliyokua anayapenda, ghafla kagongwa na gari kafariki [emoji24][emoji24]
Sehemu ile ile tuliyofanyia sherehe ndiyo hiyo hiyo tuliyofanyia msiba, unatamani kupiga hata yowe hadharani, unabaki kujikaza kiume, binamu nae kachanganyikiwa
Haya maisha haya , haya maisha haya, acheni tu, dada wa watu ndo kafa hivi kweli?