Ametanga na njia sasa amerudi tena!!

Ametanga na njia sasa amerudi tena!!

bmusic

Member
Joined
Nov 17, 2017
Posts
20
Reaction score
23
Ni miaka kama 7 imepita toka huyu mdada aniache pasipo sababu ya kueleweka, nilikuta tu mtu kaanza kunichunia..miezi ikapita na hata nilipokuja kuonana naye, aliniambia wazi nitafute mtu mwingine!

Nikajisemea isiwe kesi ila kifupi niliumia sana, kwanza nilimpenda pili nilikuwa mwaminifu sana kwake, baada ya hapo nilijaribu mara kadhaa kujaribu kumrudisha ila ikashindikana!

Sasa muda umepita, kazunguka huko na mtoto kazalishwa sasa anakuja kwangu! Anajaribu kuomba msamaha eti aliyoyafanya kipindi kile alikuwa wrong, mi nimeshindwa nimfanye nini wala sijamjibu chochote japo nimekula mzigo kimya kimya. Kwa kifupi mimi sina pa kumpeleka yeye na mwanae.

NB: Wanawake huwa mnawaza nini kurudi kwa wanaume mliowaumiza mwanzo? Hivi hata kama mtu alikupenda, upendo utabaki vile vile pamoja na kuzurula kote na kuja na mtoto eti mtu akupokee? Akili zenu huwa mnaziweka wapi?
 
Kaka mimi huwa sijui wanawaza nn. Mm nilitemwa hivyo hivyo, i was loving and caring. Baada ya miaka mi nne akanitafuta, sijui namba yangu aliipataje ,alikuwa amechoka sana yaani kachakaa sijui nn kilimkuta. Nilimpotezea 500%.

Malipo huwa ni hapa hapa duniani
 
Back
Top Bottom