Amerudi nikiwa tayari nina mwingine

Amerudi nikiwa tayari nina mwingine

socket

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2014
Posts
305
Reaction score
434
Ni hivi nilikuwa na mpenzi kweli alinipa kila kitu.Sasa tumekuwa hatuelewani kila mara ikafika kipindi ikabidi tuachane na yeye ndio alishauri hvy na kweli akabadili mpaka line ya simu.

Baada ya kupita mda nikaona kimya kingi nikafanya maamuzi ya kuwa na mdada mwingine na ukweli mimi ni mpenzi wa kwanza kwake na anajielewa sana kwenye kujali hana tofauti na yule aliyepita sasa nisimsemee vibaya wa zamani.

Huyu tuliyeachana karudi ghafla na anataka turudiane na kudai hakuniacha ila ni alikosa mawasiliano baada ya simu yake kuanguka .

Ukweli namuhurumia sana na alikuwa ananipa mapenzi matamu sijapata kuona, na ni mzuri kwakweli ila tatizo niko na mwingine nae ananipenda sana na kawaambia mpka marafiki zake na ndugu tayari baadhi wananifahamu.

Najua sitarudi kwa niliyemuacha ila swali ni kwamba nitamsaidiaje maana huwa tunaongea vizuri tu hatuna ubaya wowote.
 
mpe namba yangu ebu tuangalie tunaweza kumsaidiaje.
 
Kama alitaka muachane anataka nini tena? Kuna watu visoi na vgeugeu kweli umsaidie kwan we shirika la kutoa misaada? Ushapata mwingine huyo n x wako tayar kosa kubwa sana kuruhus mawasiliano kwa jins ulivo mpamba n waz unampenda bado.
 
km vp muweke wa reserve bahari ikiwa chafu kw mpenzi wako wa ss unaenda kwake kujipoza na kumpunguzia machungu...
 
Nimeelezea uzuri wake tuu kweli simuhitaji but inafika hatua anataka no za ndugu zangu awasalimu na akujua sisi sio wapenzi ni marafiki tuu kwa sasa
 
songa mbele usirudi nyuma. ni makosa makubwa sana ukirudiana naye. hata ukimhurimia ukamrudia, utajuta maisha yako yote kwenye mapenzi.
 
We mwambie tayar upo na kitu kingine kama akikukazia sana mwambie awe mchepuko wako
 
Ni hivi nilikuwa na mpenzi kweli alinipa kila kitu.Sasa tumekuwa hatuelewani kila mara ikafika kipindi ikabidi tuachane na yeye ndio alishauri hvy na kweli akabadili mpaka line ya simu.

Baada ya kupita mda nikaona kimya kingi nikafanya maamuzi ya kuwa na mdada mwingine na ukweli mimi ni mpenzi wa kwanza kwake na anajielewa sana kwenye kujali hana tofauti na yule aliyepita sasa nisimsemee vibaya wa zamani.

Huyu tuliyeachana karudi ghafla na anataka turudiane na kudai hakuniacha ila ni alikosa mawasiliano baada ya simu yake kuanguka .

Ukweli namuhurumia sana na alikuwa ananipa mapenzi matamu sijapata kuona, na ni mzuri kwakweli ila tatizo niko na mwingine nae ananipenda sana na kawaambia mpka marafiki zake na ndugu tayari baadhi wananifahamu.

Najua sitarudi kwa niliyemuacha ila swali ni kwamba nitamsaidiaje maana huwa tunaongea vizuri tu hatuna ubaya wowote.

Muombe Mungu ampatie wakwake watakayependana,mwambie naye aombe seriously.
 
sikiliza nyimbo mpya ya malaika bend amerudi ikiongozwa na christian bella
 
Nmesoma uzi wako na jinsi ulivyompata msichana toka chuo sasa uyo aliyerud ni yupi ndio yule uliyempata chuo?
 
sorry bado unapewa hayo MAPENZI matamu na mpya au mpya hafikii utamu wa wazamani??
 
We mwambie una mwingine. Na uwe na mipaka usijekuta unakula huku na kule
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom