Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
Huu ni mjadala mwingine katika jamii, unaotawaliwa na hoja nyepesi nyepesi; Vinginevyo kilicho kizito ni kwamba kama mtu ni muumini wa nadharia za machafuko (theories of conflicts and violence), basi Tanzania ilitakiwa iwe katika machafuko kwa muda mrefu sasa; Kinyume na hayo, Tanzania bado inaendelea kuwa nchi ya Amani na Utulivu on a ‘MACRO SCALE', ukiachilia Mbali Matukio Ya Vurugu YA Hapa na Pale on a ‘MICRO SCALE'; Pamoja na haya yote, Kuna Kila Dalili Kwamba Hatupo Mbali Kupoteza Sifa Hii kama Taifa;
Kabla ya kunyosheana vidole na kulaumiana kwa hoja nyepesi nyepesi, nadhani ni muhimu tumrejee kidogo Mwalimu Nyerere; Kuna mambo mawili makubwa ambayo sidhani kama ni ya mjadala; Kwanza, ni Ukweli kwamba Mwalimu Nyerere Kuwa ndiye Mjenzi Mkuu wa Taifa la Amani na Utulivu ambalo sote bila ya kujali itikadi za vyama, tunajivunia; Pili, ni ukweli kwamba msingi wa Ujenzi wa Taifa hilo, ilikuwa ni Azimio la Arusha;
Ebu tutazame Mwalimu ana maoni gani juu ya suala hili lililopo mbele yetu (Shivji, 2000):
["It is not that peace has come by itself. The source of peace in Tanzania is not that the Arusha Declaration has done away with poverty even a little bit. Isn't there this poverty we are still living with? This poverty is right here with us. It is not the same economy we are grappling with? The fact is not that the Arusha Declaration has banished poverty even by an iota – nor did it promise to do so. The Arusha Declaration offered hope. A promise of Justice, hopes to the many, indeed the majority of Tanzanians continue to live this hope. So long as there is this hope, you will continue to have peace. Here in Tanzania we have poverty but no ‘social cancer'. It is possible it has just begun. But otherwise we don't have a social cancer. There isn't a Volcano in the making, that one day it is bound to erupt. We have not yet reached that stage because the people still have hopes based on the stand taken by the Arusha Declaration. It did not do away with poverty but it has given you all in this hall, capitalists and socialists alike, an opportunity to build a country which holds out a future of hopes to the many.
To be sure, you few Waswahili, do you really expect to rule Tanzanians through coercion, when there is no hope? When there is no hope, and then expect that they will sit quiet in peace? Peace is born of hope, when hope is gone, there will be social upheavals. I'd be surprised if these Tanzania refuse to rebel, why?
When the majority don't have any hope you are building a volcano. It is bound to erupt one day. Unless these people are fools. Many in these countries are fools, to accept being ruled just like that. To be oppressed just like that when they have the force in numbers, they are fools. So Tanzanians would be fools, ****** (imbecile, morons, retarded/majuha), if they continued to accept to be oppressed by minority in their own country. Why?
Therefore we cannot say that we have now reached a stage when we can forget the Arusha Declaration. Don't fool yourselves. This would be like that fool who uses a ladder to climb and when he is up there kicks it away. Alright, you are up there, you have kicked away the ladder, right, so stay there because we will cut the branch. You are up there, we are down here and you have kicked away the ladder. This branch is high up, we will cut it. Your fall will be no ordinary fall either.
Let me say no more. It is sufficient to say we should accept our principles, we should continue with our principles of building peace and peace itself. Tanzanians should continue to have faith in the party, in the government and in you in positions. Tanzanians should see you as part of them not their enemies. They should trust the party, the government and you who have opportunities for there is no country where everyone is equal. These fingers of mine are not equal, and in that sense there is no such equality anywhere."]
Mwalimu Anatufunda Nini?
Kwanza: Hali aliyoinzungumzia Nyerere Miaka 25 iliyopita, inazidi kujitokeza leo Tanzania;
Pili: Mwalimu alizungumza maneno haya Wakati wa Mfumo wa Chama Kimoja Cha Siasa (CCM), na ilikuwa ni MIAKA NANE (1987) Kabla ya Kuzaliwa kwa CHADEMA (1995), Hivyo SIO SAHIHI Kuelekeza Lawama Hizi Moja Kwa Moja Kwa Chadema;
Tatu: Mwalimu alikuwa anatuonya Kwamba, Kitendo Cha Kuachana na Azimio La Arusha Bila Kwanza Ya Kuangalia Yepi Bado Yanatufaa, Kitapelekea Mmomonyoko wa Amani na Utulivu Tanzania;
Nia yangu sio kujenga hoja kwamba nani anahusika na hali ya sasa ya kutoweka kwa amani, na badala yake, kujenga mazingira ya mjadala huo kwa faida yetu sote; Nitafanya hivyo kwa kujadili nadharia za machafuko (theories of conflict and violence) katika mataifa, ili baadae tuje kuzijadili kwa mazingira ya Tanzania. Zipo nadharia kadhaa zinazoelezea vyanzo vya machafuko ndani ya taifa, na kama nilivyojadili hapo awali, kwa muumini wa nadharia hizi, Tanzania ilitakiwa iwe katika machafuko makubwa muda mrefu uliopita;
Nadharia hizi Zinaelezea Virutubisho Vikuu Vya Machafuko Katika Taifa Kama ifuatavyo:
Swali linalofuata ni, Je, Virutubisho Hivi Vipo Tanzania? Ufuato ni Mtazamo wangu juu ya hili:
1. Ukosefu mkubwa wa ajira katika taifa
Hiki ni kirutubisho cha kwanza cha machafuko ndani ya nchi; Mamilioni ya watanzania wanakabiliwa na tatizo la ajira, wengi wao ikiwa ni vijana walio kati ya umri wa miaka 15 na 25; Kwa mujibu wa Benki ya Dunia (2010), jumla ya watanzania 850,000 huingia katika soko la ajira kila mwaka, huku wachache wakifanikiwa kupata ajira rasmi na za kudumu; Benki ya Dunia inakadiria kwamba - ifikapo mwaka 2015, jeshi hili litaongezeka by an extra 1.3 Million; Swali linalofuatia ni je:
ELIMU YA MSINGI
Tukianza na vijana wanaomaliza elimu ya msingi, jumla ya wanafunzi katika mfumo wetu wa shule za msingi inakaribia MILIONI TISA; Katika hawa, inaelezwa kwamba ni 80% ndio huwa wanafanikiwa kumaliza elimu ya msingi, [sawa na karibia watoto MILIONI SABA NA LAKI MBILI], huku 20% ya wanafunzi waliobakia wakishindwa kumaliza elimu yao ya darasa la saba kwa sababu mbalimbali – [sawa na karibia watoto MILIONI MOJA NA LAKI NANE];
Kwa maana hii kila baada ya miaka michache, watoto zaidi ya Milioni Moja Wenye Umri wa Kuwa Shule, huishia mitaani wakiwa na umri chini ya miaka 15;
MUHIMU
Kati ya wanafunzi tuliobaini wanamaliza elimu ya msingi (watoto milioni saba na laki mbili), ni 20% tu ndio hufanikiwa kuendelea na elimu ya sekondari (milioni moja la laki nne), na watoto waliobakia (takribani milioni tano na laki saba), hujumuika na wale wenzao ambao hawakuweza kufika darasa la saba, hivyo kufanya Jumla ya watoto wanaoishia mitaani bila ya elimu zaidi ya darasa la Saba, katika interval ya miaka michache, kuwa takribani MILIONI SABA NA NUSU;
Hili ni sehemu ya kundi katika jamii ambalo Mwalimu Nyerere anawazungumzia kwani wanaishi katika mazingira yaliyokosa kila aina ya haki (Social injustice, Economic injustice&Political injustice); Kundi hili kwa kiasi kikubwa sana limeshakata tamaa na Utawala Wa CCM; Tukumbuke pia kwamba kabla ya kufariki dunia, Nyerere aliwahi sema maneno haya (1995):
"Watanzania wanataka Mabadiliko, na Wasipoyapata CCM, watayatafuta kupitia Chama Kingine"
Sasa, kwa bahati mbaya au nzuri, kutegemea Mtu Yupo Upande Upi wa Hoja, Chadema kinaendelea kuwa Chama Mbadala alichozungumzia Mwalimu, na isitoshe, wakati wa uhai wake, Mwalimu alitaja Chadema kwa jina - kwamba kina kila dalili ya kuja kuwa na mafanikio siku za usoni;
ELIMU YA SEKONDARI
Mbali ya tatizo lililopo kwenye elimu ya msingi, kwa mujibu wa Benki ya Dunia (2010), katika kipindi cha mwaka 2000 – 2010, jumla ya wanafunzi milioni moja la laki tatu walimaliza elimu yao ya Sekondari; Kati ya hawa:
Kwa maana hii, iwapo tunachukulia kwamba wanafunzi waliopata madaraja ya Kwanza hadi Tatu ndio uendelea na elimu ya juu, basi ina maana kwamba kati ya wanafuzi milioni moja na laki tatu waliomaliza elimu zao za sekondari katika kipindi hicho (2000 – 2010), waliofanikiwa kuendelea na elimu ya juu ni 25% tu [sawa na wanafunzi 325,000 kati ya jumla ya wanafunzi 1,300,000]; Hivyo, katika kipindi hiki, wanafunzi wa sekondari walioishia mitaani ni karibia 975,000; Hata kwa wale wanaofanikiwa kuendelea na elimu ya juu, bado suala la ajira huko mbeleni sio la uhakika;
MUHIMU
Ni dhahiri kwamba wengi ya watoto (vijana) hawa ambao hawaendelei na elimu za juu, wanaingia kwenye soko la ajira wakiwa hawana ujuzi wa kutosha kuweza kumudu ushindani katika soko; Lakini hili lisingekuwa tatizo sana iwapo wangekuwa wanavutiwa na ajira kwenye sekta ya KILIMO; lakini kwa bahati mbaya, ni idadi ndogo sana ya vijana hawa wanavutiwa na ajira katika Sekta ya Kilimo; Hili ni tatizo, hasa ikizingatiwa kwamba bado KILIMO kinatambulika rasmi kama sekta kuu ya ajira, na pia Uti wa Mgongo wa Taifa ‘Kiuchumi';
2. Idadi kubwa ya Vijana Ndani Ya Taifa
Hiki ni kirutubisho cha pili cha machafuko ndani ya nchi; Suala hili linaenda sambamba na lile la awali – yani tatizo la ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana; Lakini kwa kuongezea tu, kwa mujibu wa African Economic Outlook (2010), zaidi ya 60% ya watanzania hawajavuka umri wa miaka 25, na inakisiwa kwamba ifikapo mwaka 2015, idadi hii itaongezeka na kufikia 75% ya jumla ya idadi ya watanzania; Kwa maana hii, ifikapo mwaka 2015, watanzania zaidi ya milioni 33 watakuwa chini ya umri wa miaka 25; Hili ndio "TIMING BOMB" ambalo wanasiasa mbalimbali wamekuwa wanajaribu kulijadili kisiasa;
3. Idadi kubwa ya Makabila na mgawanyiko mkubwa wa imani za kidini
Kirutubisho hiki kipo bayana: Inasemekana Tanzania ina makabila zaidi ya mia moja na ishirini, na pia Taifa limegawanyika karibia nusu kwa nusu kati ya Waumini wa Kislam na Waumini Wa Kikristo;
4. Machafuko ya Kisiasa Kwenye Nchi Zinazopakana na Taifa husika
Hiki ni kirutubisho cha nne; Tanzania imezungukwa na nchi ambazo - karibia zote zimepitia machafuko ya aina mbalimbali, huku nyingine zikiendelea kuwa katika hali ya machafuko; Kutokana na machafuko haya, Tanzania ilishawahi kupokea jumla ya wakimbizi karibia milioni moja kutoka nchi za maziwa makuu zilizokuwa katika mapigano ya wenyewe kwa wenyewe; Kuna wakati Tanzania ilikuwa ni moja ya mataifa yenye idadi kubwa ya wakimbizi duniani;
5. Hali duni za vipato vya wananchi walio wengi
Hiki ni kirutubisho cha tano; Kwa mujibu wa takwimu za IMF, Pato la Taifa Tanzania ni takribani Dola Bilioni 23 kwa mwaka; Vile vile, kwa miaka kumi na mbili mfululizo (2000 – 2012), uchumi wa nchi unakuwa kwa wastani wa karibia 7% kwa mwaka; Huko nyuma, Benki ya Dunia iliwahi kutamka kwamba - nchi ikiwa na kasi ya namna hii kwa miaka zaidi ya kumi mfululizo, inakuwa katika nafasi nzuri ya kufikia malengo yote ya MILLENIA, hasa kupunguza umaskini kwa 50%;
Lakini Je, Umaskini Tanzania Umepungua Kwa Kiasa Gani?
Pato la taifa la Dollar Bilioni 23 kwa mwaka, linaiweka Tanzania katika nafasi ya kumi na nne kwa ukubwa kiuchumi barani Afrika (kati ya mataifa 53), na nafasi ya ‘98' duniani kati ya jumla ya mataifa 185 yaliyomo kwenye orodha ya Benki ya Dunia (2011); Kasi yetu ya kukua kwa uchumi (takribani 7% kwa mwaka), inaiweka Tanzania kuwa nchi ya 12 Afrika na ya 43 duniani;
Hizi discrepancies hapa ni tosha kuleta mashaka kuhusu thamani ya uchumi wetu ni kwa faida ya nani; Vinginevyo, kilicho dhahiri ni kwamba - Tanzania ina rasilimali nyingi zinazovutia mitaji mingi kutoka sehemu mbalimbali za duniani (kwani uchumi wetu unaendeshwa na mitaji ya nje kwa karibia 75%), lakini mitaji hiyo haiji kwa ajili ya watanzania walio wengi, wala kwa manufaa ya watanzania walio wengi, bali inakuja kutokana na rasilimali nyingi zilizopo Tanzania na kwa manufaa ya wachache;
Swali linalofuatia ni JE:
Bila shaka jibu ni kwamba – sio watanzania walio wengi, hasa wakulima vijijini; Zipo tafiti zinaonyesha kwamba asilimia ya waanchi wanaofaidika na uchumi wa leo Tanzania, haizidi 10% ya watanzania wote, licha ya nchi kujaliwa kila aina ya rasilimali; Kwa maana nyingine, kukua kwa pato la taifa na uchumi hakupelekei Maisha Bora kwa watanzania walio wengi;
Ifuatayo ni sehemu ndogo ya ushahidi juu ya hili:
Pamoja na Tanzania kuwa ni nchi ya '98' kwa ukubwa wa uchumi duniani, na nchi ya '43' kwa kasi ya kukua kwa uchumi duniani, katika suala la GDP Per Capita, Tanzania ni nchi ya sita kutoka mwisho Duniani; Tanzania ni bora kwa nchi zisizozidi tano ambazo ni: Malawi, Madagascar, Burundi, Liberia na DRC; Kwa maana nyingine rahisi, kwenye suala la vipato kwa wananchi, Tanzania ni nchi ya sita kutoka mwisho duniani, hivyo kufanya watanzania kuwa miongoni mwa watu maskini kuliko wote duniani, huku nchi yao ikiwa ni moja ya nchi tajiri kupindukia duniani;
Wapo wanaoweza kujenga hoja kwamba GDP Per Capita sio kielelezo kizuri, hivyo tujaribu kuangalia vielelezo vingine juu ya umaskini wetu watanzania: Idadi ya Watanzania wenye $1.25 (karibia 2,000/=) au chini ya hizi mifukoni mwao kila siku ni karibia 70% (karibia watanzania milioni 30); Na Watanzania wenye $2 (takribani 3,000/=) mifukoni mwao kila siku, ni karibia 90% (sawa na watanzania takribani milioni 36);
Je: Shillingi elfu mbili au elfu tatu kwa siku inatosha kwa matumizi ya aina gani kwa mtanzania wa leo kwa mahitaji kama vile nauli, chakula cha familia, mahitaji ya watoto shule n.k? Ni dhahiri haitoshi, na kwa maana hii, zaidi ya watanzania milioni 30 wanaishi maisha ya kuunga unga, na yasio na matumaini kama alivyojadili Nyerere awali;
6. Utegemezi wa misaada usiokwisha kutoka nje, kuendesha bajeti ya nchi
Hiki ni kichecho cha mwisho cha machafuko, kukijadili; Tunafahamu kwamba Tanzania ni moja ya nchi zinazoongoza duniani kwa kutegemea misaada kutoka nje kuendesha bajeti ya nchi; Kwa miaka zaidi ya 30 sasa, Tanzania imekuwa katika kumi bora ya orodha hii kidunia; Inakadiriwa kwamba, tangia uhuru, zaidi ya dollar za Kimarekani Bilioni KUMI zimeingia Tanzania kwa njia hii; Swali la kujiuliza ni je:
Swali hili ni muhimu, hasa ikizingatiwa kwamba, wananchi walio wengi hawaelewi kwamba Fedha hizi kuitwa misaada haina maana kwamba zinakuja bure, kwani ni mikopo yenye masharti na riba nafuu ambayo hulipwa na fedha za walipa kodi – wakulima, wafanyakazi, mama ntilie, machinga, n.k;
Madhara Ya Kutegemea Sana Misaada:
Yapo mengi, lakini kwa madhumuni ya mjadala huu, kwanza, Utegemezi Huu ambao sasa umekuwa ni wa Kudumu, umeua dhana ya "KUJITEGEMEA" katika nchi yetu, na badala yake, tunajulikana kama moja ya mataifa matajiri duniani ambao ni "OMBA OMBA";
Pili, kutegemea sana misaada kuna athiri BALANCE OF PAYMENTS ya nchi yetu: Maana rahisi ya kuelewa dhana ya Balance of Payments: BOP ni tofauti iliyopo baina ya MALIPO TUNAYOFANYA nje ya nchi (outflows) kama vile madeni, manunuzi ya bidhaa muhimu kwa maendeleo ya uchumi kama vile mashine, vipuri, magari ya serikali, n.k, na MALIPO TUNAYOPATA kutoka nje ya nchi (inflows), kama vile mapato yanayotokana na kuuza mazao yetu nje, madini yetu n.k;
Lakini kwa vile kwa miaka mingi tumekosa uwezo wa kuzalisha bidhaa muhimu kupitia viwanda vyetu na badala yake tunaagiza hata vitu virahisi kutengeneza nchini, na kwa kuwa kwa miaka mingi tumekuwa hatutumii vizuri mikopo kutoka nje kwa kuwekeza kwenye sekta ambazo zitatusaidia tujitegemee kama taifa, OUTFLOWS (malipo ya mikopo, manunuzi ya capital goods n.k) zinakuwa ni kubwa kuliko INFLOWS (mapato yetu kutoka kwenye biashara ya kimataifa n.k), na kupelekea Balance of Payments Deficits;
Na Kutokana na Deficit hii kuendelea kuwa mzigo – kutokana na kukopa zaidi na zaidi bila ya kujitengenezea mazingira ya kujitegemea na pia kulipa madeni yaliyopo kwa uhakika; na pia kutokana na suala ufisadi kuzidi kushika kasi, nchi nyingi wahisani zimeanza kulegeza kamba, na hatuna uhakika iwapo wahisani wataendelea kutusaidia katika bajeti zetu kwa kwa viwango vinavyohitajika; Na iwapo misaada katika bajeti itapungua, huku taifa likiwa halijajitengenezea mazingira ya kujitegemea, hii itapelekea kupungua kwa kwa huduma za kijamii kutoka serikali ya CCM, jambo ambalo linaweza kuchochoea hali ya machafuko nchini;
HITIMISHO
Tumeona kwamba virutubisho vyote sita vya machafuko katika Taifa, vipo Tanzania; Lakini pamoja na hayo, kwa kiasi kikubwa, Tanzania bado inaendelea kuwa nchi ya Amani na Utulivu, licha ya uwepo wa Volcano anayoizungumzia Mwalimu Nyerere. Maswali ya Kujadili:
Kabla ya kunyosheana vidole na kulaumiana kwa hoja nyepesi nyepesi, nadhani ni muhimu tumrejee kidogo Mwalimu Nyerere; Kuna mambo mawili makubwa ambayo sidhani kama ni ya mjadala; Kwanza, ni Ukweli kwamba Mwalimu Nyerere Kuwa ndiye Mjenzi Mkuu wa Taifa la Amani na Utulivu ambalo sote bila ya kujali itikadi za vyama, tunajivunia; Pili, ni ukweli kwamba msingi wa Ujenzi wa Taifa hilo, ilikuwa ni Azimio la Arusha;
Ebu tutazame Mwalimu ana maoni gani juu ya suala hili lililopo mbele yetu (Shivji, 2000):
["It is not that peace has come by itself. The source of peace in Tanzania is not that the Arusha Declaration has done away with poverty even a little bit. Isn't there this poverty we are still living with? This poverty is right here with us. It is not the same economy we are grappling with? The fact is not that the Arusha Declaration has banished poverty even by an iota – nor did it promise to do so. The Arusha Declaration offered hope. A promise of Justice, hopes to the many, indeed the majority of Tanzanians continue to live this hope. So long as there is this hope, you will continue to have peace. Here in Tanzania we have poverty but no ‘social cancer'. It is possible it has just begun. But otherwise we don't have a social cancer. There isn't a Volcano in the making, that one day it is bound to erupt. We have not yet reached that stage because the people still have hopes based on the stand taken by the Arusha Declaration. It did not do away with poverty but it has given you all in this hall, capitalists and socialists alike, an opportunity to build a country which holds out a future of hopes to the many.
To be sure, you few Waswahili, do you really expect to rule Tanzanians through coercion, when there is no hope? When there is no hope, and then expect that they will sit quiet in peace? Peace is born of hope, when hope is gone, there will be social upheavals. I'd be surprised if these Tanzania refuse to rebel, why?
When the majority don't have any hope you are building a volcano. It is bound to erupt one day. Unless these people are fools. Many in these countries are fools, to accept being ruled just like that. To be oppressed just like that when they have the force in numbers, they are fools. So Tanzanians would be fools, ****** (imbecile, morons, retarded/majuha), if they continued to accept to be oppressed by minority in their own country. Why?
Therefore we cannot say that we have now reached a stage when we can forget the Arusha Declaration. Don't fool yourselves. This would be like that fool who uses a ladder to climb and when he is up there kicks it away. Alright, you are up there, you have kicked away the ladder, right, so stay there because we will cut the branch. You are up there, we are down here and you have kicked away the ladder. This branch is high up, we will cut it. Your fall will be no ordinary fall either.
Let me say no more. It is sufficient to say we should accept our principles, we should continue with our principles of building peace and peace itself. Tanzanians should continue to have faith in the party, in the government and in you in positions. Tanzanians should see you as part of them not their enemies. They should trust the party, the government and you who have opportunities for there is no country where everyone is equal. These fingers of mine are not equal, and in that sense there is no such equality anywhere."]
Mwalimu Anatufunda Nini?
Kwanza: Hali aliyoinzungumzia Nyerere Miaka 25 iliyopita, inazidi kujitokeza leo Tanzania;
Pili: Mwalimu alizungumza maneno haya Wakati wa Mfumo wa Chama Kimoja Cha Siasa (CCM), na ilikuwa ni MIAKA NANE (1987) Kabla ya Kuzaliwa kwa CHADEMA (1995), Hivyo SIO SAHIHI Kuelekeza Lawama Hizi Moja Kwa Moja Kwa Chadema;
Tatu: Mwalimu alikuwa anatuonya Kwamba, Kitendo Cha Kuachana na Azimio La Arusha Bila Kwanza Ya Kuangalia Yepi Bado Yanatufaa, Kitapelekea Mmomonyoko wa Amani na Utulivu Tanzania;
Nia yangu sio kujenga hoja kwamba nani anahusika na hali ya sasa ya kutoweka kwa amani, na badala yake, kujenga mazingira ya mjadala huo kwa faida yetu sote; Nitafanya hivyo kwa kujadili nadharia za machafuko (theories of conflict and violence) katika mataifa, ili baadae tuje kuzijadili kwa mazingira ya Tanzania. Zipo nadharia kadhaa zinazoelezea vyanzo vya machafuko ndani ya taifa, na kama nilivyojadili hapo awali, kwa muumini wa nadharia hizi, Tanzania ilitakiwa iwe katika machafuko makubwa muda mrefu uliopita;
Nadharia hizi Zinaelezea Virutubisho Vikuu Vya Machafuko Katika Taifa Kama ifuatavyo:
- Ukosefu mkubwa wa ajira katika taifa;
- Idadi kubwa ya Vijana ndani ya taifa;
- Idadi kubwa ya Makabila na mgawanyiko mkubwa wa imani za Kidini;
- Machafuko ya Kisiasa Kwenye Nchi Zinazopakana na Taifa husika;
- Hali Duni (Kimapato) kwa wananchi walio wengi;
- Utegemezi (usiokwisha/chronic) wa Misaada kutoka mataifa ya nje, hasa katika kuendesha bajeti ya nchi;
Swali linalofuata ni, Je, Virutubisho Hivi Vipo Tanzania? Ufuato ni Mtazamo wangu juu ya hili:
1. Ukosefu mkubwa wa ajira katika taifa
Hiki ni kirutubisho cha kwanza cha machafuko ndani ya nchi; Mamilioni ya watanzania wanakabiliwa na tatizo la ajira, wengi wao ikiwa ni vijana walio kati ya umri wa miaka 15 na 25; Kwa mujibu wa Benki ya Dunia (2010), jumla ya watanzania 850,000 huingia katika soko la ajira kila mwaka, huku wachache wakifanikiwa kupata ajira rasmi na za kudumu; Benki ya Dunia inakadiria kwamba - ifikapo mwaka 2015, jeshi hili litaongezeka by an extra 1.3 Million; Swali linalofuatia ni je:
- Jeshi Hili Linaingia Kwenye Soko la Ajira na Ubora wa Namna Gani?
ELIMU YA MSINGI
Tukianza na vijana wanaomaliza elimu ya msingi, jumla ya wanafunzi katika mfumo wetu wa shule za msingi inakaribia MILIONI TISA; Katika hawa, inaelezwa kwamba ni 80% ndio huwa wanafanikiwa kumaliza elimu ya msingi, [sawa na karibia watoto MILIONI SABA NA LAKI MBILI], huku 20% ya wanafunzi waliobakia wakishindwa kumaliza elimu yao ya darasa la saba kwa sababu mbalimbali – [sawa na karibia watoto MILIONI MOJA NA LAKI NANE];
Kwa maana hii kila baada ya miaka michache, watoto zaidi ya Milioni Moja Wenye Umri wa Kuwa Shule, huishia mitaani wakiwa na umri chini ya miaka 15;
MUHIMU
Kati ya wanafunzi tuliobaini wanamaliza elimu ya msingi (watoto milioni saba na laki mbili), ni 20% tu ndio hufanikiwa kuendelea na elimu ya sekondari (milioni moja la laki nne), na watoto waliobakia (takribani milioni tano na laki saba), hujumuika na wale wenzao ambao hawakuweza kufika darasa la saba, hivyo kufanya Jumla ya watoto wanaoishia mitaani bila ya elimu zaidi ya darasa la Saba, katika interval ya miaka michache, kuwa takribani MILIONI SABA NA NUSU;
Hili ni sehemu ya kundi katika jamii ambalo Mwalimu Nyerere anawazungumzia kwani wanaishi katika mazingira yaliyokosa kila aina ya haki (Social injustice, Economic injustice&Political injustice); Kundi hili kwa kiasi kikubwa sana limeshakata tamaa na Utawala Wa CCM; Tukumbuke pia kwamba kabla ya kufariki dunia, Nyerere aliwahi sema maneno haya (1995):
"Watanzania wanataka Mabadiliko, na Wasipoyapata CCM, watayatafuta kupitia Chama Kingine"
Sasa, kwa bahati mbaya au nzuri, kutegemea Mtu Yupo Upande Upi wa Hoja, Chadema kinaendelea kuwa Chama Mbadala alichozungumzia Mwalimu, na isitoshe, wakati wa uhai wake, Mwalimu alitaja Chadema kwa jina - kwamba kina kila dalili ya kuja kuwa na mafanikio siku za usoni;
ELIMU YA SEKONDARI
Mbali ya tatizo lililopo kwenye elimu ya msingi, kwa mujibu wa Benki ya Dunia (2010), katika kipindi cha mwaka 2000 – 2010, jumla ya wanafunzi milioni moja la laki tatu walimaliza elimu yao ya Sekondari; Kati ya hawa:
- Waliopasi kwa Division One ilikuwa ni 3% (wanafunzi takribani 39,000)
- Division Two, 5% (takribani wanafunzi 65,000)
- Division Three, 15% (takribani wanafunzi 195,000)
- Division Four, 50% (takribani wanafunzi 650,000)
- Division Zero, 26% (takribani wanafunzi 338,000)
Kwa maana hii, iwapo tunachukulia kwamba wanafunzi waliopata madaraja ya Kwanza hadi Tatu ndio uendelea na elimu ya juu, basi ina maana kwamba kati ya wanafuzi milioni moja na laki tatu waliomaliza elimu zao za sekondari katika kipindi hicho (2000 – 2010), waliofanikiwa kuendelea na elimu ya juu ni 25% tu [sawa na wanafunzi 325,000 kati ya jumla ya wanafunzi 1,300,000]; Hivyo, katika kipindi hiki, wanafunzi wa sekondari walioishia mitaani ni karibia 975,000; Hata kwa wale wanaofanikiwa kuendelea na elimu ya juu, bado suala la ajira huko mbeleni sio la uhakika;
MUHIMU
Ni dhahiri kwamba wengi ya watoto (vijana) hawa ambao hawaendelei na elimu za juu, wanaingia kwenye soko la ajira wakiwa hawana ujuzi wa kutosha kuweza kumudu ushindani katika soko; Lakini hili lisingekuwa tatizo sana iwapo wangekuwa wanavutiwa na ajira kwenye sekta ya KILIMO; lakini kwa bahati mbaya, ni idadi ndogo sana ya vijana hawa wanavutiwa na ajira katika Sekta ya Kilimo; Hili ni tatizo, hasa ikizingatiwa kwamba bado KILIMO kinatambulika rasmi kama sekta kuu ya ajira, na pia Uti wa Mgongo wa Taifa ‘Kiuchumi';
2. Idadi kubwa ya Vijana Ndani Ya Taifa
Hiki ni kirutubisho cha pili cha machafuko ndani ya nchi; Suala hili linaenda sambamba na lile la awali – yani tatizo la ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana; Lakini kwa kuongezea tu, kwa mujibu wa African Economic Outlook (2010), zaidi ya 60% ya watanzania hawajavuka umri wa miaka 25, na inakisiwa kwamba ifikapo mwaka 2015, idadi hii itaongezeka na kufikia 75% ya jumla ya idadi ya watanzania; Kwa maana hii, ifikapo mwaka 2015, watanzania zaidi ya milioni 33 watakuwa chini ya umri wa miaka 25; Hili ndio "TIMING BOMB" ambalo wanasiasa mbalimbali wamekuwa wanajaribu kulijadili kisiasa;
3. Idadi kubwa ya Makabila na mgawanyiko mkubwa wa imani za kidini
Kirutubisho hiki kipo bayana: Inasemekana Tanzania ina makabila zaidi ya mia moja na ishirini, na pia Taifa limegawanyika karibia nusu kwa nusu kati ya Waumini wa Kislam na Waumini Wa Kikristo;
4. Machafuko ya Kisiasa Kwenye Nchi Zinazopakana na Taifa husika
Hiki ni kirutubisho cha nne; Tanzania imezungukwa na nchi ambazo - karibia zote zimepitia machafuko ya aina mbalimbali, huku nyingine zikiendelea kuwa katika hali ya machafuko; Kutokana na machafuko haya, Tanzania ilishawahi kupokea jumla ya wakimbizi karibia milioni moja kutoka nchi za maziwa makuu zilizokuwa katika mapigano ya wenyewe kwa wenyewe; Kuna wakati Tanzania ilikuwa ni moja ya mataifa yenye idadi kubwa ya wakimbizi duniani;
5. Hali duni za vipato vya wananchi walio wengi
Hiki ni kirutubisho cha tano; Kwa mujibu wa takwimu za IMF, Pato la Taifa Tanzania ni takribani Dola Bilioni 23 kwa mwaka; Vile vile, kwa miaka kumi na mbili mfululizo (2000 – 2012), uchumi wa nchi unakuwa kwa wastani wa karibia 7% kwa mwaka; Huko nyuma, Benki ya Dunia iliwahi kutamka kwamba - nchi ikiwa na kasi ya namna hii kwa miaka zaidi ya kumi mfululizo, inakuwa katika nafasi nzuri ya kufikia malengo yote ya MILLENIA, hasa kupunguza umaskini kwa 50%;
Lakini Je, Umaskini Tanzania Umepungua Kwa Kiasa Gani?
Pato la taifa la Dollar Bilioni 23 kwa mwaka, linaiweka Tanzania katika nafasi ya kumi na nne kwa ukubwa kiuchumi barani Afrika (kati ya mataifa 53), na nafasi ya ‘98' duniani kati ya jumla ya mataifa 185 yaliyomo kwenye orodha ya Benki ya Dunia (2011); Kasi yetu ya kukua kwa uchumi (takribani 7% kwa mwaka), inaiweka Tanzania kuwa nchi ya 12 Afrika na ya 43 duniani;
Hizi discrepancies hapa ni tosha kuleta mashaka kuhusu thamani ya uchumi wetu ni kwa faida ya nani; Vinginevyo, kilicho dhahiri ni kwamba - Tanzania ina rasilimali nyingi zinazovutia mitaji mingi kutoka sehemu mbalimbali za duniani (kwani uchumi wetu unaendeshwa na mitaji ya nje kwa karibia 75%), lakini mitaji hiyo haiji kwa ajili ya watanzania walio wengi, wala kwa manufaa ya watanzania walio wengi, bali inakuja kutokana na rasilimali nyingi zilizopo Tanzania na kwa manufaa ya wachache;
Swali linalofuatia ni JE:
- Who Gets the Largest Share and Who Benefits the Most?
Bila shaka jibu ni kwamba – sio watanzania walio wengi, hasa wakulima vijijini; Zipo tafiti zinaonyesha kwamba asilimia ya waanchi wanaofaidika na uchumi wa leo Tanzania, haizidi 10% ya watanzania wote, licha ya nchi kujaliwa kila aina ya rasilimali; Kwa maana nyingine, kukua kwa pato la taifa na uchumi hakupelekei Maisha Bora kwa watanzania walio wengi;
Ifuatayo ni sehemu ndogo ya ushahidi juu ya hili:
Pamoja na Tanzania kuwa ni nchi ya '98' kwa ukubwa wa uchumi duniani, na nchi ya '43' kwa kasi ya kukua kwa uchumi duniani, katika suala la GDP Per Capita, Tanzania ni nchi ya sita kutoka mwisho Duniani; Tanzania ni bora kwa nchi zisizozidi tano ambazo ni: Malawi, Madagascar, Burundi, Liberia na DRC; Kwa maana nyingine rahisi, kwenye suala la vipato kwa wananchi, Tanzania ni nchi ya sita kutoka mwisho duniani, hivyo kufanya watanzania kuwa miongoni mwa watu maskini kuliko wote duniani, huku nchi yao ikiwa ni moja ya nchi tajiri kupindukia duniani;
Wapo wanaoweza kujenga hoja kwamba GDP Per Capita sio kielelezo kizuri, hivyo tujaribu kuangalia vielelezo vingine juu ya umaskini wetu watanzania: Idadi ya Watanzania wenye $1.25 (karibia 2,000/=) au chini ya hizi mifukoni mwao kila siku ni karibia 70% (karibia watanzania milioni 30); Na Watanzania wenye $2 (takribani 3,000/=) mifukoni mwao kila siku, ni karibia 90% (sawa na watanzania takribani milioni 36);
Je: Shillingi elfu mbili au elfu tatu kwa siku inatosha kwa matumizi ya aina gani kwa mtanzania wa leo kwa mahitaji kama vile nauli, chakula cha familia, mahitaji ya watoto shule n.k? Ni dhahiri haitoshi, na kwa maana hii, zaidi ya watanzania milioni 30 wanaishi maisha ya kuunga unga, na yasio na matumaini kama alivyojadili Nyerere awali;
6. Utegemezi wa misaada usiokwisha kutoka nje, kuendesha bajeti ya nchi
Hiki ni kichecho cha mwisho cha machafuko, kukijadili; Tunafahamu kwamba Tanzania ni moja ya nchi zinazoongoza duniani kwa kutegemea misaada kutoka nje kuendesha bajeti ya nchi; Kwa miaka zaidi ya 30 sasa, Tanzania imekuwa katika kumi bora ya orodha hii kidunia; Inakadiriwa kwamba, tangia uhuru, zaidi ya dollar za Kimarekani Bilioni KUMI zimeingia Tanzania kwa njia hii; Swali la kujiuliza ni je:
- Mabilioni haya ya dollar, yamefanya kitu gani cha maana kwa watanzania walio wengi (hasa vijijini)?
Swali hili ni muhimu, hasa ikizingatiwa kwamba, wananchi walio wengi hawaelewi kwamba Fedha hizi kuitwa misaada haina maana kwamba zinakuja bure, kwani ni mikopo yenye masharti na riba nafuu ambayo hulipwa na fedha za walipa kodi – wakulima, wafanyakazi, mama ntilie, machinga, n.k;
Madhara Ya Kutegemea Sana Misaada:
Yapo mengi, lakini kwa madhumuni ya mjadala huu, kwanza, Utegemezi Huu ambao sasa umekuwa ni wa Kudumu, umeua dhana ya "KUJITEGEMEA" katika nchi yetu, na badala yake, tunajulikana kama moja ya mataifa matajiri duniani ambao ni "OMBA OMBA";
Pili, kutegemea sana misaada kuna athiri BALANCE OF PAYMENTS ya nchi yetu: Maana rahisi ya kuelewa dhana ya Balance of Payments: BOP ni tofauti iliyopo baina ya MALIPO TUNAYOFANYA nje ya nchi (outflows) kama vile madeni, manunuzi ya bidhaa muhimu kwa maendeleo ya uchumi kama vile mashine, vipuri, magari ya serikali, n.k, na MALIPO TUNAYOPATA kutoka nje ya nchi (inflows), kama vile mapato yanayotokana na kuuza mazao yetu nje, madini yetu n.k;
Lakini kwa vile kwa miaka mingi tumekosa uwezo wa kuzalisha bidhaa muhimu kupitia viwanda vyetu na badala yake tunaagiza hata vitu virahisi kutengeneza nchini, na kwa kuwa kwa miaka mingi tumekuwa hatutumii vizuri mikopo kutoka nje kwa kuwekeza kwenye sekta ambazo zitatusaidia tujitegemee kama taifa, OUTFLOWS (malipo ya mikopo, manunuzi ya capital goods n.k) zinakuwa ni kubwa kuliko INFLOWS (mapato yetu kutoka kwenye biashara ya kimataifa n.k), na kupelekea Balance of Payments Deficits;
Na Kutokana na Deficit hii kuendelea kuwa mzigo – kutokana na kukopa zaidi na zaidi bila ya kujitengenezea mazingira ya kujitegemea na pia kulipa madeni yaliyopo kwa uhakika; na pia kutokana na suala ufisadi kuzidi kushika kasi, nchi nyingi wahisani zimeanza kulegeza kamba, na hatuna uhakika iwapo wahisani wataendelea kutusaidia katika bajeti zetu kwa kwa viwango vinavyohitajika; Na iwapo misaada katika bajeti itapungua, huku taifa likiwa halijajitengenezea mazingira ya kujitegemea, hii itapelekea kupungua kwa kwa huduma za kijamii kutoka serikali ya CCM, jambo ambalo linaweza kuchochoea hali ya machafuko nchini;
HITIMISHO
Tumeona kwamba virutubisho vyote sita vya machafuko katika Taifa, vipo Tanzania; Lakini pamoja na hayo, kwa kiasi kikubwa, Tanzania bado inaendelea kuwa nchi ya Amani na Utulivu, licha ya uwepo wa Volcano anayoizungumzia Mwalimu Nyerere. Maswali ya Kujadili:
- Nini ni Chanzo Kikuu cha Mmomonyoko wa Amani na Utulivu Nchini Tanzania?
- Je, Ni Chadema? Kwa Hoja Zipi?
- Je, Ni Kweli Kwamba Mjenzi wa Taifa La Amani Na Utulivu Ni ‘Mwalimu Nyerere' Kupitia Azimio La Arusha?
- Kama Jibu Kwa Swali la Tatu ni NDIO, Kwa Vile Nyerere Hatunaye Tena na Azimio La Arusha Hatunalo Tena, JE, nini imebakia kuwa nguzo kuu ya Kulinda Amani na Utulivu Katika Nchi Yetu?
- Je, Ni CCM? Kwa Hoja Zipi?
- Kama Jibu Kwa Swali la Tatu ni HAPANA, Bila ya Kujali Itikadi Zetu Za Vyama, Nini Ni Mbadala Rasmi Wa Azimio La Arusha Ambao Unaeleweka na Unaokubaliwa na Walio Wengi Kwamba Una Manufaa Kwa Taifa, na Mbadala ambao CCM na Chadema Wote Wapo Tayari Kuufanyia Kazi, CCM ikiwa Chama Tawala au Chama Kikuu Cha Upinzani au Chadema ikiwa Chama Tawala au Chama Kikuu Cha Upinzani?