Noel france
JF-Expert Member
- Oct 8, 2012
- 1,159
- 1,054
- Thread starter
- #61
Mkuu kuhalalisha ulicho kisema ni sawa na kusema hakuna aliyemkubwa kuliko CHADEMA kama taasisi.
Soma hapa..
Haya aliyanena Zitto Z. Kabwe miaka miwili iliyopita:
"Tumegundua kuwepo kwa juhudi za makusudi kutugombanisha CHADEMA.
Hiki ni chama makini, kimezibaini njia hizo na kwa hakika hakiwezi kusambaratishwa.
CHADEMA ndiyo imenipa Umaarufu mimi. Mimi si maarufu kuliko Chama, CHADEMA ni taasisi.
CHADEMA ni chama ambacho kina misingi katika uanzishwaji wake.
Wanasema eti nilishinda kwa umaarufu wangu binafsi. SI KWELI. Niligombea ubunge nikitokea shule. Sikuwa najulikana. Niliikuta 'grassroot network' ya Chama.
Hakikujengwa na mimi. CHADEMA ilijengwa na uongozi uliokuwepo. Nilikuta uongozi intact ( imara). Katika kila kijiji kulikuwa na uongozi na hata katika vitongoji vyote.
Wakati naingia kugombea ubunge kulikuwa na wanachama wa CHADEMA wenye kadi wanaofika 10,800 katika jimbo zima.
Hawa sikuwatafuta mimi, niliwakuta na ndio waliofanikisha ushindi wangu.
Katika mazingira kama haya utasemaje kuwa mimi ni maarufu kuliko chama wakati chama ndicho kimenipa umaarufu?.
CHADEMA ni Chama ambacho wenyeviti wake wastaafu wanaendelea kuenziwa na kuhudhuria vikao vyote vya Chama. Institutional memory ipo kuliko katika vyama vyote vya upinzani.
Alipohama Dr Aman Walid Kabourou, wengi walidhani ndiyo mwisho wa CHADEMA Kigoma, lakini leo hii CHADEMA ni moto Kigoma kuliko ilivyokuwa awali".
Chanzo: Chadema ni msingi.
pamoja sana kamanda kwa kutuletea nukuu zenye ushahidi tosherezi. Kazi ni kwao vibaraka wanao jaribu kuzuia upepo kwa kutumia viganja vya mkono. Ukweli utabaki ukweli hata kama watabisha.