Amakweli CHADEMA inabeba watu. Huu ndio ukweli.

Amakweli CHADEMA inabeba watu. Huu ndio ukweli.

Chadema haina watu ila inabeba kikundi furani cha walaghai kinachofanya biashara ya kisiasa na kulaghai watu.
Naona umetoka kabisa kwenye mada tatizo lako unatumika katika ile kitu iliyopigwa marufuku kule uganda na inashabikiwa na Obama
 
Hivi Mageti sita amepotelea wapi mbona humu ndani simwoni? LB7 yeyote atakayemwona amsalimie sana.
 
:israel::lock1::director::director::violin::majani7::msela::horn::lalala::clap2::clap2:
 
Wakati ulifika tukabeba kila mtu lkn wengi hawakidhi viwango vya kuwa viongozi na ndio hayo makapi yanapepetwa
 
Hukuwa na haja ya kufanya utafiti. Ni sawa na mtu aliyezaliwa me aende kufanya utafiti kama ye ni me. Samahanini kwa huo mfano wangu, lakini namaanisha kuwa, CDM ndiyo Maarufu si mtu. Ukijiondoa au kuondolewa kwenye ule umaarufu anabaki debe tupu lenye lebo tu. Mali ni cdm. Ndo maana watu wanatofautishwa na hivyo vyama vingine. Chadema imo mioyoni mwa watu. Hata wanaojaribu kuiudhi CDM wanafika mahali mioyo inawasuta wana changanyikiwa.

Chama hakiwezi kumfanya mtu kuwa maarufu bt umaarufu mtu ujitengenezea kutokana haiba na kaliba yake. Kujidanganya cdm inawafanya kuwa maarufu ni upungufu na uelewa Mdogo mlionayo mbona wewe siyo maarufu kuliko James Mbatia?au hamad rashid au ht wema sepetu?
 
Mtei alisema kuwa zitto kama anataka kubakia na uanachama wa Mahakama wao hawana shida... “Lakini huwezi kuwapeleka viongozi wako kortini na bado ukaendelea kubaki kuwa mwanachama wetu.”
Alimtuhumu kwa kuwagonganisha viongozi mbalimbali ndani ya Chadema na hata kuzua mitafaruku ya hapa na pale huku akisema kwamba uamuzi wa Kamati Kuu ndiyo wa mwisho.
 
ni kweli , cdm imekuwa kama wavuvi haramu , inasomba hata matakataka ! ujinga uwe wakati wa kwenda tu , SAFARI HII HATUTAFANYA UJINGA TENA , HAKUNA NAFASI KWA WASALITI .
 
Chadema haina watu ila inabeba kikundi furani cha walaghai kinachofanya biashara ya kisiasa na kulaghai watu.

Isisahahu na kile chama chenye kundi la wauza unga,pembe za ndovu na wabakaji sawa eee!!
 
Samahani ndugu Yericko hivi ule utafiti wako ulioufanya kuhusu dhana ya "UGAIDI " na ukaleta uzi hapa kwamba unataka kuchapisha kitabu umeishia wapi...nilisikia eti ulisahau kuchange ID yako ukajikuta unajijibu mwenyewe..ni kweli mkuu..??

Ha ha ha kumbe wale walosemwa na Max wanalipwa mpk wanakuwa na ID zaidi ya moja njaa bhana
 
Soma umaamuma wa zito alivyopayuka
Taarifa ya Chadema inasema kwamba chama hicho (chama changu) kilikuwa kimechunguza mwenendo wangu tangu mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini kuwa mimi napokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga Chadema.

Ripoti hiyo ilinihusisha pia na mwananchi raia wa Ujerumani, Andrea Cordes ambaye, kwa mujibu wa ripoti hiyo, alinisaidia kupokea na kuhifadhi kiasi cha dola 250,000 za Marekani kupitia kwenye akaunti yake binafsi.

Taarifa hii ya kutunga na iliyojaa uongo wa kiwango cha kutisha, imenifadhaisha, kunisikitisha na kunikasirisha.
 
Chama hakiwezi kumfanya mtu kuwa maarufu bt umaarufu mtu ujitengenezea kutokana haiba na kaliba yake. Kujidanganya cdm inawafanya kuwa maarufu ni upungufu na uelewa Mdogo mlionayo mbona wewe siyo maarufu kuliko James Mbatia?au hamad rashid au ht wema sepetu?

sasa mbona wakitimuliwa umaarufu wao unapukutika ? MFANO MCHUKUE JULIANA SHONZA LEO HALAFU MWAMBIE AITISHE MKUTANO HATA SOKONI KARIAKOO , TANGAZA KWENYE MEDIA ZOTE HATA KWA MWEZI MZIMA , WACHUKUE HATA FM ACADEMIA WATUMBUIZE ( MAANA TOT IMEKUFA ) HALAFU UONE KAMA KUNA ATAKAYEKUJA KUMSIKILIZA !
 
sasa mbona wakitimuliwa umaarufu wao unapukutika ? MFANO MCHUKUE JULIANA SHONZA LEO HALAFU MWAMBIE AITISHE MKUTANO HATA SOKONI KARIAKOO , TANGAZA KWENYE MEDIA ZOTE HATA KWA MWEZI MZIMA , WACHUKUE HATA FM ACADEMIA WATUMBUIZE ( MAANA TOT IMEKUFA ) HALAFU UONE KAMA KUNA ATAKAYEKUJA KUMSIKILIZA !

Kwani shonza ninani katika siasa za nchi hii? Ndo maana nasema uelewa Mdogo au ushabiki tu mwafanya km mfanyavo kwenye soka jmn siasa ni maisha huyu unayemdharau leo kesho Rais wako tuwe na upeo na akili ya uchambuzi kwenye siasa hakuna Rafiki au adui Wa kudumu tuwaheshimu wenzetu tubishane kwa hoja na Sera si matusi na kejeli
 
Chadema mmekuja na style mpya ya kujiliwaza ili muiaminishe jamii kwamba bado mpo kumbe mmeshajifia.
 
Chama hakiwezi kumfanya mtu kuwa maarufu bt umaarufu mtu ujitengenezea kutokana haiba na kaliba yake. Kujidanganya cdm inawafanya kuwa maarufu ni upungufu na uelewa Mdogo mlionayo mbona wewe siyo maarufu kuliko James Mbatia?au hamad rashid au ht wema sepetu?

Kweli weye ndo hamnazo kabisa, Unasema ati Chama hakiwezi kumpa mtu umaarufu? Unajua unalolisema au is it for the sake of arguing?? Mi sipendi kubishana kwani mwisho wa mabishano ni kutukanana.
Kama chama hakimpi mtu umaarufu, jiulize hao waliofukuzwa CCM wakaja CDM mbona walipita kwa kura nyingi tu? Mbona Shibuda hakuenda NCCR? Bila chama, pesa ndio itakupa umaarufu.
Ngoja kidogo uone visa vya kutangatanga wanasiasa wakitafuta chama maarufu apart from ccm
 
UMEONA MKUU,ila mda ukifika watajua tu,wakamuulize NAJIB BALALA wa ODM,alijitoa ODM akidhani atashinda kwa urais useneta wa mombasa,ila kilichotokea kijana mdogo chipukizi wa siasa kutoka Mombasa alimuangusha mapema.
ndio hao jamaa wanaotoka na matusi yatawakuta
 
Hiki chama bado sijajua malengo ya kuanzishwa kwake ni kushindana na Chadema au nini, maana naona mtaji wao ni kuisakama Chadema, sijui ndio upinzani wao huo, tangazeni sera zenu ni zipi ili wananchi wawapime kama mnajipya, ukiona chama kimeanzishwa halafu kinajenga bifu na Chadema, jua kabisa hiyo ni plani ya ccm kuendelea kuihujumu Chadema kama chama kikuu cha upinzani.
 
Kiukweli wanajamvi nimetamani kushare nanyi jambo ili,ambalo nimelifanyia utafiti mdogo nanikafanikiwa kubaini kitu.
Mimi nimesema na nafsi yangu na wewe sema na nafsi yako kwanza kisha changia.
Ndugu zangu kiukweli nimewafatilia kwa ukaribu karibu wote waliojitoa na kufukuzwa uwanachama ndani ya chadema,kiukweli wanakuwa kama weu alafu wanapungukiwa vitu vifuatavyo kama vile kukosa tena mvuto katika jamii,pia hawana hoja wanapokua wanaongea mbele ya watu. Kutokana na machache niliyoyabaini,nalazimika kusema ya kwamba;chadema inawabeba wanachama wake tofauti na tunavyo aminishwa na wasaliti wetu eti bila mimi chadema(samanini nimebana pua na kubinjua midomo kuonyesha nijinsi gani walivyokua wananichefua). Ila kama unabisha wafatari kwa ukaribu karibu wote walio tumuliwa na wale wote walio iama chadema. Lazima utawaona wanaongea pumba.

Mkuu kuhalalisha ulicho kisema ni sawa na kusema hakuna aliyemkubwa kuliko CHADEMA kama taasisi.

Soma hapa..

Haya aliyanena Zitto Z. Kabwe miaka miwili iliyopita:


"Tumegundua kuwepo kwa juhudi za makusudi kutugombanisha CHADEMA.
Hiki ni chama makini, kimezibaini njia hizo na kwa hakika hakiwezi kusambaratishwa.
CHADEMA ndiyo imenipa Umaarufu mimi. Mimi si maarufu kuliko Chama, CHADEMA ni taasisi.
CHADEMA ni chama ambacho kina misingi katika uanzishwaji wake.


Wanasema eti nilishinda kwa umaarufu wangu binafsi. SI KWELI. Niligombea ubunge nikitokea shule. Sikuwa najulikana. Niliikuta 'grassroot network' ya Chama.


Hakikujengwa na mimi. CHADEMA ilijengwa na uongozi uliokuwepo. Nilikuta uongozi intact ( imara). Katika kila kijiji kulikuwa na uongozi na hata katika vitongoji vyote.

Wakati naingia kugombea ubunge kulikuwa na wanachama wa CHADEMA wenye kadi wanaofika 10,800 katika jimbo zima.
Hawa sikuwatafuta mimi, niliwakuta na ndio waliofanikisha ushindi wangu.


Katika mazingira kama haya utasemaje kuwa mimi ni maarufu kuliko chama wakati chama ndicho kimenipa umaarufu?.

CHADEMA ni Chama ambacho wenyeviti wake wastaafu wanaendelea kuenziwa na kuhudhuria vikao vyote vya Chama. Institutional memory ipo kuliko katika vyama vyote vya upinzani.

Alipohama Dr Aman Walid Kabourou, wengi walidhani ndiyo mwisho wa CHADEMA Kigoma, lakini leo hii CHADEMA ni moto Kigoma kuliko ilivyokuwa awali".


Chanzo: Chadema ni msingi.
 
Watakuja kutukana hapa watoto wa Lumumba ilhali uzi unahusu Wana CHADEMA, we subiri uone wanavyoanza kutiririka mapovu kama wamechomolewa vichwa.

nani alikuwa anamjua lema kabla ya kudandia chadema???!!!
 
Back
Top Bottom