Ama kweli Lowassa amekwaa kisiki hatari!

Ama kweli Lowassa amekwaa kisiki hatari!

idawa

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2012
Posts
25,298
Reaction score
38,438
Pamoja na Kujiandaa Kuchukua nchi kwa zaidi ya miaka 25.

Pamoja na kuwanunua aslimia kubwa ya wahariri na waandishi wa kawaida wa vyombo vya habari

Pamoja na kuwanunua robo tatu ya wajumbe wa kamati kuu hadi kufikia hatua ya kumzomea Mwenyekiti.

Pamoja na kuvinunua vyama vikubwa vinne vya upinzani na yeye akiwa ndio mgombea pekee.

Pamoja na kumiliki mtandao mpana zaidi na wa hatari nchini Mafioso & Mafisadi Unity (MMU)

Lakini bado anaonekana kupwaya kwa Magufuli,alieanza harakati za urais juzi ,tena hana mtandao ,hana vyombo vya habari vya kueleweka hata ule mtandao hatari Mafioso & Mafisadi Unity (MMU) unamwogopa na kumwangalia kwa jicho la tatu.!

Magufuli usikate tamaa ,watanzania wachache wenye uelewa na nchi yao wanatambua juhudi zako.!
 
..........................
Magufuli usikate tamaa ,watanzania wachache wenye uelewa na nchi yao wanatambua juhudi zako.!

Hapo kijani hapo: Mwili wako i radhi lakini moyo ni dhaifu!
 
Umesema wananchi wachache wanatambua juhudi za magufuli hujui kuwa kura zinatakiwa za wananchi wengi. Asante kwa kukubali wananchi wengi wako kwa lowassa. Twende na lowassa
 
Kule Seif kawabana mbavu kweli kabomoa ngome ya CCM Unguja lakini CCM tangia enzi za mwalimu walishindwa kabisa kutoboa ngome nzito ya CUF Pemba (since 1995 election )Huku nako Lowassa !!matezi lazima yawashuke...CCM OUT
 
Kwenye mikutano yenu fanyeni haya halafu urudi tena hapa JF:

1. Msitumie malori kusafirisha watu
2. Msiwatangulize jukwaani akina daimond na ze komedi!
Mkuu hoja sio wasanii,Mbona na nyie mnatumia Chopa Kama kivutio.

Ukweli ni kwamba Lowassa anapwaya kwa Magufuli Pamoja na mtandao hatari alionao.!
 
Umesema wananchi wachache wanatambua juhudi za magufuli hujui kuwa kura zinatakiwa za wananchi wengi. Asante kwa kukubali wananchi wengi wako kwa lowassa. Twende na lowassa
Na siku zote wanaookoa sio wengi Bali wachache kwa faida ya wengi.!
 
Unaposema watanzania wachache.....je, hao wachache watampa kura za ushindi!

Kubali kataa Lowassa rais 2015!

Hvo Ndivo Unavoamini,namim Naamini Kuwa Vyovyote Vile Ukubali Ukatae Magufuli Ndio Rais Wa Jmt Awamu Ya 5...
 
Star tv imenunuliwa na chama gani. Channel ten inemunuliwa na chama gani. Tbc imenunuliwa na chama gani na vingine vingi
 
Kwenye mikutano yenu fanyeni haya halafu urudi tena hapa JF:

1. Msitumie malori kusafirisha watu
2. Msiwatangulize jukwaani akina daimond na ze komedi!
1. Kwani CHADEMA hawatumii malori/hawabebi watu?
2. Kwani CHADEMA/UKAWA hawatumii wasanii?....Hawa akina Ney wa Mitego...Bob Junior...Wolper..Shamsa Ford sio wasanii?...
 
Ingekuwa urais unapatikana kwenye mitandao basi Lowasa angekuwa rais,lakini bahati nzuri wapiga kura asilimia kubwa ni wale ambao hawajawahi kutumia mtandao
 
Ingekuwa urais unapatikana kwenye mitandao basi Lowasa angekuwa rais,lakini bahati nzuri wapiga kura asilimia kubwa ni wale ambao hawajawahi kutumia mtandao
2010 Dr.Slaa angekua Rais wa Tanzania, na kwenye mitandao ccm haijawai kushinda ila Mwisho Siku wengi wetu huduwaa.!
 
Mkuu hoja sio wasanii,Mbona na nyie mnatumia Chopa Kama kivutio.

Ukweli ni kwamba Lowassa anapwaya kwa Magufuli Pamoja na mtandao hatari alionao.!

Chopa usafiri sio kivutio! Nyie mbona chopa kwan mnatumia kama kivutio? Miaka 2 ya uwaziri mkuu wa Lowassa ni kama miaka 20 ya Magufuli wizarani!
 
Back
Top Bottom