Alwaz
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,118
- 10,822
Vidio inayotajwa kuwa ni ya Ayman Aldhawaahir imetolewa.Vidio hiyo inayoelezwa kuwa ni ya nusu saa kiongozi huyo aliyekuwa ati chini ya Osama ameitoa akiomboleza kifo cha bosi wake.
Imeelezwa amemsifu Osama na kwamba ataendeleza vita dhidi ya Marekani na kwamba amelaumu kitendo cha kuzikwa Osama baharini kwamba si cha kiislamu.
Ajabu ya vidio hiyo ni kuwa zaidi ya picha ya Aldhawaahir wazungumzaji wote ni watu wa CIA halafu imeunganishwa na maelezo mengi kuhusiana na matatizo yanayoendelea katika nchi za kiislamu.Katika Aljazeera wakielezea vidio hiyo mchambuzi wao anayeitwa Marwan Albishara amembeza Aldhawaahir na kwamba nchi hizo sasa zina harakati mbadala kutokana na zile za Alqaeda.
Jamani yupo aliyeiona vidiio hiyo nje ya mitandao ya CNN na Aljazeera?.Kwanini Aldhawaahir haachiwi akazungumza mwenyewe angalau dakika moja?.Binafsi nimesikia neno moja tu kwenye sekunde za mwanzo lenye kuashiria kufa kwa Osama .... ilaa rabih (...kwa Mola wake).
Kama yupo mwenye uwezo wa kueleza usahihi wa kituko hiki,naomba aingie ukumbini ili heshima za binadamu ziendelee kuwa juu kuliko wanyama wa kufugwa.
Imeelezwa amemsifu Osama na kwamba ataendeleza vita dhidi ya Marekani na kwamba amelaumu kitendo cha kuzikwa Osama baharini kwamba si cha kiislamu.
Ajabu ya vidio hiyo ni kuwa zaidi ya picha ya Aldhawaahir wazungumzaji wote ni watu wa CIA halafu imeunganishwa na maelezo mengi kuhusiana na matatizo yanayoendelea katika nchi za kiislamu.Katika Aljazeera wakielezea vidio hiyo mchambuzi wao anayeitwa Marwan Albishara amembeza Aldhawaahir na kwamba nchi hizo sasa zina harakati mbadala kutokana na zile za Alqaeda.
Jamani yupo aliyeiona vidiio hiyo nje ya mitandao ya CNN na Aljazeera?.Kwanini Aldhawaahir haachiwi akazungumza mwenyewe angalau dakika moja?.Binafsi nimesikia neno moja tu kwenye sekunde za mwanzo lenye kuashiria kufa kwa Osama .... ilaa rabih (...kwa Mola wake).
Kama yupo mwenye uwezo wa kueleza usahihi wa kituko hiki,naomba aingie ukumbini ili heshima za binadamu ziendelee kuwa juu kuliko wanyama wa kufugwa.