kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,252
- 16,171
Mkuu wa Mkoa ni kiongozi wa watu wote, taasisi zote na vikundi vyote. Anapokuwa anatumia pesa ya watu wote kuwapa Tabora United inayoshiriki ligi kuu sawa na timu nyingine sio sawa. Hii ni tofauti na goli la mama ambalo linatolewa kwa timu yoyote inayoshiriki mashindano makubwa. Mkuu wa mkoa anapofanya mambo kama kiongozi wa Tabora uninted atafanyiwa kama kiongozi wa mpira badala ya kiongozi wa Mkoa wa Tabora.
Mkuu wa Mkoa anapodai na kuhoji wanaoipokea Yanga Tabora aliongea kama Mkuu wa Mkoa, kiongozi wa timu ya Tabora United au kama shabiki wa Simba? Kwanini anataka watu wa mpira wamtendee kama mkuu wa Mkoa wakati yeye ametenda kama kiongozi wa timu na shabiki wa simba?
Kumkamata Ally Kama kwa mambo ya mpira amevuka mipaka na kuichonganisha CCM na wananchi bila sababu. Mkuu wa Mkoa ameichafua Yanga kwa kudai wanataka kuwahonga wachezaji wa Tabora na walimroga; huku ni kuvuka mipaka ya kimamlaka. tabora ni ya watanzania kwanini anahoji watu wanaoipokea Yanga?
Nadhani Rais anapaswa kuwakemea wateule kama hawa,
Mkuu wa Mkoa anapodai na kuhoji wanaoipokea Yanga Tabora aliongea kama Mkuu wa Mkoa, kiongozi wa timu ya Tabora United au kama shabiki wa Simba? Kwanini anataka watu wa mpira wamtendee kama mkuu wa Mkoa wakati yeye ametenda kama kiongozi wa timu na shabiki wa simba?
Kumkamata Ally Kama kwa mambo ya mpira amevuka mipaka na kuichonganisha CCM na wananchi bila sababu. Mkuu wa Mkoa ameichafua Yanga kwa kudai wanataka kuwahonga wachezaji wa Tabora na walimroga; huku ni kuvuka mipaka ya kimamlaka. tabora ni ya watanzania kwanini anahoji watu wanaoipokea Yanga?
Nadhani Rais anapaswa kuwakemea wateule kama hawa,