Huu undugu sasa umekuwa mzigo! Tatizo nna wivu na kaka zangu kuliko hata l'aziz wangu! Mmh! Shkamoo kaka. Uko zamu kwa nani leo, nataka kuja kudoea vitumbua
Nakuambia Kaizer hii kazi ni ngumu mno! Jinsi fomu za sensa zilivyoandaliwa kuna viboksi 4 tu vya kujaza status yaani unajaza kimojawapo sasa tunapokea marital status ambazo hatujawahi kuzisikia. Hebu fikiria hii ya Kongosho "Triplets" hata sijui naiweka wapi? Fomu ingekuwa ina kiboksi cha "other" labda tungejaza hapo lakini looh! zoezi gumu.
Mie raha yangu ipo kwenye hilo tabasamu lako tamu... lol. Kuna kibaridi hapa na amini usiamini nina kahawa hapa... Fanya hima msiri wa Kaizer uje upate kahawa. Ila hara hara naomba usimrushe roho mdogo wangu wala mimi hapa, naona kisha anza kuwa na wasi wasi hapo juu... Uwe unatoa taarifa mkipeana siri... lol