Aliyenizidi umri anapokataa salamu ya shikamoo nimpe salamu gani?

Kati ya vitu ambavyo havijawahi kunifikirisha ni shikamoo.. Kwa wadogo kwangu aniamkie, asiniamkie yote saw na kwa wanaonizidi ntakuangalia kwanza kama una umri sawa na wazazi wangu ntakuamkia ila ukiwa chini ya hapo ntakwambia za hizi ukishtuka ukanambia we kijana em nipe heshima yangu mi silingani na wewe hapo ntakuamkia.. Niko hivo kwanza mi ni wale jamaa ambao utotoni tulikuwa tunasifika kwa kutosalimia wageni
 
Tumia lugha ya malkia!
 
Dar hakuna shikamoo. Mara ya mwisho kupewa shikamoo nilikua Tanga 2016. Bukoba na Mudoma hata kuijua hawaijui.
 
Kama ni Mkristo mwamkie Bwana Yesu asifiwe na kama Mwislam mwamkie Asalaam Aleykum

Sent using Jamii Forums mobile app
 


Kama mimi ndio sitaki kabisa hizo salamu za shikamoo hasa mwanamama akiwa mrembo naona kama anataka kuninyima fursa fulani fulani.
 
Sasa were ni bosi wake, labda kachelewa kidogo kufika ofisini sababu ya majukumu fulani ya lazima, unamfokea kama mtoto mbele ya wafanyakazi wenzake!! Hiyo shikamoo yako inasaund kweli?
 
Huku kenya hakuna hizo salamu
 
Point ni moja tu apo ukifikisha miaka 30 acha kusalimiana watu shkamoo

Ni mwendo wa kujuliana habari za saizi za mchana na jion
 
Hata mimi nikimhusudu mwanamke kijana, huwa sipendi shikamoo zake.

Akikuzoesha hilo 'lishikamoo', tena kila akinipiaga nalo, kabla sijamuitikia, hujitokeza neno ghafla 'hivi huyu binti anataka kuninyima nini' kisha ndiyo naitikia kwa sauti ya chini kabisa.
Maana yake utakapotaka kumbadilishia kibao na kuanza 'kumsomesha' hisia zako huwaga ni kazi ya ziada inayohitaji kutumia makuwadi.

Na mkishakuwa wapenzi kuamkiana 'shikamoo' hudhoofu na kisha kufa yenyewe pole pole.
Hilo la kwanza, la pili waTz wengi wanachukulia 'shikamoo' kama salamu ya mamlaka.

Kuna wakati nikiwa kijana na nina madaraka, hizo salamu nimezipokea sana nikawa ninashangaa.

Kuna siku nikiwa ofisink,mzee m1 aliingia akanisalimia 'shiamoo' nikamuuliza maana ya kunitukuza na hiyo salamu, wakati mimi ndiye nilistahili kumuamkia kutokana na umri wetu!

Yule mzee alinipa makavu bila ya kumumunya maneno, akaniambia 'hii siyo salamu yako, ni salamu ya ofisi na cheo ulichonacho'.
...'Siku ukiondolewa kwenye ofisi hii hautasikia salamu yangu ya namna hii'.

Nikaliacha lilivyo, sasa juzi Rais akiwa ziarani Mbeya nilishangazwa na kubakia mdomo wazi, salamu ya Igp ya shikamoo kwa rais wakati makamo yao ni yaleyale, ndiyo nikakumbuka yale ya yule mzee!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ilishanikuta sana nikiwa posta kwenye majengo makubwa huko ukisalimia mtu kwa hiyo salamu hakuna anaeitikia toka siku hizo situmii tena hiyo salamu nikiwa mjini.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…