Maarifa
JF-Expert Member
- Nov 23, 2006
- 4,568
- 2,911
Nkapa
Ni nani aliyemjua John Pombe Magufuli kabla ya mwaka 1995?
Hili ni swali muhimu sana kwa wale wanaofikiria na kufuatilia siasa za Tanzania toka enzi na enzi.
Ilikuwaje Mkapa akamteua kuwa mmoja wa askari wa miamvuli just from nowhere?
Ilikuwaje kamati ya maadili ya CCM ikakubaliana kuja na jina la Magufuli kwenye tano bora ya CCM mwaka 2015 bila kujali mbwembwe za watia nia wakongwe na wakiojinadi kwa mbwembwe kwa miaka zaidi ya sita?
Ilikuwaje Magufuli akaweza kuepuka scandals za kumuangusha kama Waziri katika kipindi kilichokumbwa na scandals nyingi?
Inakuwaje au ilikuwaje Magufuli ameweza kuhimili mikikimikiki ya wizara zote alizopelekwa na kuibuka hero?
Unapojiuliza maswali haya ni lazima ujiulize ni nani hasa aliyemuibua John Pombe Joseph Magufuli.
Pia ni lazima umuheshimu aliyemuibua the coming president of URT.
Isitoshe ni muhimi kumuheshimu au kuheshimu chombo kinachoibua watu wa namna hii!