Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Priscus Tarimo, ameibuka mshindi katika kura za maoni za chama hicho kwa kupata kura 1,539 kati ya kura halali 3,288 zilizopigwa, na hivyo kutetea nafasi yake ya kuwania tena ubunge.
Matokeo hayo yametangazwa leo, Agosti 4, 2025, na Msimamizi wa Uchaguzi wa CCM Jimbo la Moshi Mjini, Ndg. Ivan Moshi, ambaye alisema kura 10 kati ya zilizopigwa zilihesabiwa kuwa batili.
Tarimo amewazidi washindani wake wakiwemo Ibrahim Shayo aliyeshika nafasi ya pili kwa kupata kura 1,495, Amini Twaha (143), Samwel Ngowi (67), Theresia Komba (36), na Neema Kumburu (8).
Zoezi hilo la kupiga kura limefanyika mapema leo katika kata zote 21 za Jimbo la Moshi Mjini na limeshirikisha wagombea sita waliowania tiketi ya CCM kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.
Matokeo hayo yametangazwa leo, Agosti 4, 2025, na Msimamizi wa Uchaguzi wa CCM Jimbo la Moshi Mjini, Ndg. Ivan Moshi, ambaye alisema kura 10 kati ya zilizopigwa zilihesabiwa kuwa batili.
Tarimo amewazidi washindani wake wakiwemo Ibrahim Shayo aliyeshika nafasi ya pili kwa kupata kura 1,495, Amini Twaha (143), Samwel Ngowi (67), Theresia Komba (36), na Neema Kumburu (8).
Zoezi hilo la kupiga kura limefanyika mapema leo katika kata zote 21 za Jimbo la Moshi Mjini na limeshirikisha wagombea sita waliowania tiketi ya CCM kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.