Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
Aliyekuwa Katibu wa Rais wa awamu ya tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Ndugu Ngussa Samike leo Jumamosi Juni 28, 2025 amechukua Fomu ya Chama Cha Mapinduzi CCM ya kuomba ridhaa ya kupeperusha bendera ya Chama hicho kwenye Kinyang'anyiro cha Ubunge, Jimbo la Sengerema Mkoani Mwanza katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025.
Kuchukua fomu kwa Bw. Ngussa Samike kumeongeza msisimko katika kinyang'anyiro cha Ubunge katika Jimbo hilo ambalo kwasasa linaongozwa na Mhe. Hamis Tabasamu kutokana na ushawishi wake kisiasa uliopanda zaidi wakati wa utawala wa Awamu ya tano na awamu hii ya sita. Bw. Ngussa amewahi kuwa Katibu tawala wa Mkoa wa Mwanza na Mkoa wa Lindi katika utawala wa awamu ya sita.
Chanzo: Jambo TV
Kuchukua fomu kwa Bw. Ngussa Samike kumeongeza msisimko katika kinyang'anyiro cha Ubunge katika Jimbo hilo ambalo kwasasa linaongozwa na Mhe. Hamis Tabasamu kutokana na ushawishi wake kisiasa uliopanda zaidi wakati wa utawala wa Awamu ya tano na awamu hii ya sita. Bw. Ngussa amewahi kuwa Katibu tawala wa Mkoa wa Mwanza na Mkoa wa Lindi katika utawala wa awamu ya sita.
Chanzo: Jambo TV