Aliyefukuzwa TRC kubadilishiwa Mashtaka?

Aliyefukuzwa TRC kubadilishiwa Mashtaka?

mirindimo

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2009
Posts
1,041
Reaction score
2,141
7BD33599-9A96-41BC-828F-BE8EC3206328.jpeg
God is us again 😄 ili ionekane Kadogosa ako sahihi kwa habari za chini huyu bwana anapangiwa zengwe apewe mashtaka tofauti ikiwezekana hata ya Uhujumu Uchumi ama matumizi mabaya ya nafasi. Mama anaupiga mwingi mnooo kazi iendelee
 
Nchi yetu Ili mambo yaende ni kuwa mnaa Tu ukijifanya activist unatetea wengine utajijua na mkeo na wanao watakapoanza kukusumbua. Mf. Mzuri Mimi mikelele ya harakati ni humu JF kitaa nipo kama nimekunywa maji ya bendera alafu Kuna kamanda wa CHADEMA aje kunishawishi Amadala ajilipue thubutuuu!!
 
View attachment 2335717God is us again ili ionekane Kadogosa ako sahihi kwa habari za chini huyu bwana anapangiwa zengwe apewe mashtaka tofauti ikiwezekana hata ya Uhujumu Uchumi ama matumizi mabaya ya nafasi. Mama anaupiga mwingi mnooo kazi iendelee
Mmesahau DCI ni nani??
Kwa kuwa kumbusha tuu Dci ni Kingai. Mtaalamu wa kesi za kubumba.
 
High degree or level of understanding, reasoning, inteliigence, having foresight, etc, are qualities that could put you in trouble if you have those qualities and you use them when arguing with politicians especially those found in Africa.
 
Nchi yetu Ili mambo yaende ni kuwa mnaa Tu ukijifanya activist unatetea wengine utajijua na mkeo na wanao watakapoanza kukusumbua. Mf. Mzuri Mimi mikelele ya harakati ni humu JF kitaa nipo kama nimekunywa maji ya bendera alafu Kuna kamanda wa CHADEMA aje kunishawishi Amadala ajilipue thubutuuu!!
Nyie mnadhani akina Nape na yule dogo wa umoja wa vijana wa CCM wajinga, kuwa chawa kunalipa kuliko kujifanya kifaru hasa kwenye nchi zetu hizi za Kiafrika. Mwisho wa yote wale mabingwa wa vishkwambi hawatakusaidia kuweka ugali mezani baada ya kukuta yale uliyoyataka yakukute/
 
Hapa duniani inatakiwa uwe mnafiki, ukiwa mkweli tayari unaliwa.
Watu hawataki kusikia ukweli hata kidogo,
Siyo kweli, kila mtu anapenda UKWELI.
Na yuko tayari kutafuta documents na watu wathibitishe huo UKWELI( hasa ikiwa ameonewa).
Mfano: Viongozi wetu wa kitaifa wakiambiwa kuwa wao ni RAIA wa Uganda Unadhani watakubali?,wataleta documents na watu mbalimbali kuthibitisha uraia wao. Hii inamaana kuwa wanaupenda UKWELI.
ILA kama UKWELI huo utakuwa chanzo cha matatizo ( hakuna binadamu anayeutaka), hilo siyo kwa viongozi tu, bali ni sisi wote.
MFANO: Unampenda sana mwanamke X(mke wako) lakini una uhusiano na mwanamke Y(kimada). Lakini huyu X, akijua uhusiano wako na Y ataachana na wewe.( Ukweli huu hutautaka ufahamike kwa X. Hivyo utauchukia).
Pia, nakubaliana na wewe kuwa ili uishi vizuri na watu ni vizuri ukawa mnafiki(Hii inasababishwa na mapungufu tuliyo nayo).
 
Mwenyewe anapenda kusifiwa niambie wapi alikataza asisifiwe na ndio maana alimuita jukwaani JAH PEOPLE amsifie... Viongozi wengi wa afrika wanapenda sifa kuliko kuambiwa ukweli, ndio maana ukienda kwenye mitandao ya kijamii wanamtag ili wapate teuzi
 
Kesha kamatwa kwa kosa la kimtandao na Kibatala anahangaika kujua yupo kituo gani
Uzoefu unatuonyesha kuwa utambiwa yupo Mbweni kumbe yupo Stakishari au Tazara
 
Uyo jamaa amejitakia mwenyewe yaliyomkuta hakutumia busara kabisa maana yeye ni mtumishi wa Serikali sasa inakuaje anaanza kuikosoa tena ngoja apate adabu iwe fundisho
 
Uyo jamaa amejitakia mwenyewe yaliyomkuta hakutumia busara kabisa maana yeye ni mtumishi wa Serikali sasa inakuaje anaanza kuikosoa tena ngoja apate adabu iwe fundisho
Ndio ubaya wa kufanya mambo Bila kufikiria hatima yake.....kabla ya kufanya Jambo unatakiwa unaliangalia ktk engo tofauti....
 
Kesha kamatwa kwa kosa la kimtandao na Kibatala anahangaika kujua yupo kituo gani
Uzoefu unatuonyesha kuwa utambiwa yupo Mbweni kumbe yupo Stakishari au Tazara
Huyo atakua mwigulu anataka amkomoe, unajua kabla ya magufuli kuwa kiongozi mwenye roho mbaya kuwahi kutokea nchoni alikuwepo mwigulu ambaye alitengeneza mtandao wa utekaji, utesaji na kubambika kesi watu.
 
Back
Top Bottom