Alichosema Putin kuhusu Afrika

Alichosema Putin kuhusu Afrika

deblabant

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2022
Posts
3,010
Reaction score
4,495
Kama ulikuwa hujui kuwa PUTIN amesema nini kuhusu AFRIKA, wacha nikufahamishe:

RAIS wa URUSI, Mheshimiwa VLADIMIR PUTIN,
Jana amelihutubia taifa na kusema kuwa:
Kuna watu wananilaumu mimi na serikali yangu kwamba,
kwanini naingilia masilahi yao kwa kuamua kumsaidia TRAORE.
Sasa leo wacha niwaambie ukweli, wazungu,
lakini pia wacha niwaambie Waafrika ukweli.
Japokuwa ukweli huu utakua mchungu kwa Waafrika, wacha niwaambie:

"Katika kipindi cha chini ya miaka 20 ijayo,
UFARANSA itakuwa koloni la makoloni yake ya zamani.
Wala sihitaji kuanzisha vita dhidi ya UFARANSA.
Kile ninachohitaji ni kuzikomboa nchi za AFRIKA,
hasa zinazozungumza lugha ya Kifaransa ambazo,
kwa muda mrefu zimekuwa makoloni ya UFARANSA.
Nikizikomboa hizi nchi zikawa na nguvu na miundombinu ya kiuchumi,
pamoja na kiteknolojia na kujisimamia wenyewe kijeshi,
lazima UFARANSA itaanguka yenyewe,
kama tunda lililooza liangukavyo kutoka kwenye mti.

Nani kati yetu sisi wa ULAYA asiyejua ukweli mchungu kuwa
ardhi ya AFRIKA ina uwezo wa kulisha ULAYA, AMERIKA, na ASIA yote?

Lakini kitu pekee ambacho AFRIKA imekosa ni viongozi wenye akili.

AFRIKA imebarikiwa rasilimali adimu duniani,
lakini shida ni viongozi waliolaaniwa, wabinafsi, hawana akili,
na wanaojali familia zao kuliko nchi zao.

AFRIKA ina utajiri mara 20 zaidi ya ULAYA,
lakini AFRIKA ni masikini—masikini takribani zaidi ya mara maelfu kimaendeleo.

Ninachoweza kuwaambia Waafrika ni kwamba,
kama viongozi wao watadhubutu kujitambua
na kuunda sarafu moja ya pamoja kwa ajili ya AFRIKA mzima,
nawahakikishia nchi nyingi za ULAYA zitakuja kuomba misaada AFRIKA.

AFRIKA inamiliki 70% ya maliasili zinazopatikana ulimwenguni,
AFRIKA inamiliki 70% ya malighafi zinazotumika kuunda silaha za nyuklia.

Na wazungu wanajua hilo, lakini kwa kejeli,
bado mpaka leo hii MAREKANI na UFARANSA
wanaujasiri wa kuiita AFRIKA kuwa ni bara masikini zaidi duniani,
kwa sababu tu wazungu hao wamefanikiwa kuwashika akili Waafrika.

Na Waafrika wenyewe walivyo kama mazezeta,
wanaamini kuwa kujipendekeza kwa wazungu ndiyo ujanja,
na wanaamini kuwa ULAYA ni sehemu bora kuishi kuliko AFRIKA,
na wanaliona bara lao kama sehemu mbaya kuliko mabara yote duniani.

Sasa nimeamua kumsapoti ndugu yangu TRAORE,
kwa sababu yeye ameonesha kuwa anajitambua.

TRAORE anajitambua sana kuliko viongozi wote wa AFRIKA na raia wao.

Mimi kama PUTIN, kama RAIS wa URUSI,
nasema hapa leo kuwa nipo tayari kumsaidia kiongozi yeyote atakaye jitambua AFRIKA
ila ujitambue kweli kweli kama TRAORE.

Lakini kama utakuja kwangu ukaniomba msaada,
na kuniambia kuwa sasa wewe na raia wako mnajitambua,
na unataka kuikomboa nchi yako kwa kunidanganya,
utajuta kuzaliwa, kwani URUSI huwa haipendi mambo ya kijinga kijinga."

— amesema PUTIN
Makala hii imeletwa kwenu na Dhulkad Madara kutoka Morogoro.
 
Ardhi ya Urusi ni zaidi. Ya 1/3 tatu ya Afrika lakini kwanini yeye hairishi ulaya na Marekani kwa pamoja
Mkuu are you insane?
Large percent ya land ya urusi sio productive land ni land yenye barafu,lakini land ya Africa at large ni productive land as in terms of ardhi Yenyewe na pia resources ambazo bara la ulaya Lina depend on those resources
 
Mkuu are you insane?
Large percent ya land ya urusi sio productive land ni land yenye barafu,lakini land ya Africa at large ni productive land as in terms of ardhi Yenyewe na pia resources ambazo bara la ulaya Lina depend on those resources
Sasa yeye mbona nchi yake inaongoza kwa rasilimali za madini na mafuta ila raia wake wanahangaika tu kuliko ulaya na Marekani ? Mwambie udikteta ndiyo mwiba mchungu kwa maendeleo
 
Kama ulikua hujui kuwa PUTIN amesema nini kuhusu AFRIKA wacha nikufahamishe;-
RAIS wa URUSI muheshimiwa VLADMIR PUTIN,
Jana amelihutubia taifa na kusema kuwa,
Kuna watu wananilaumu mimi na serikali yangu kuwa,
Kwanini naingilia masilahi yao kwa kuamua kumsaidia TRAORE,
Sasa leo wacha niwaambie ukweli wazungu,
Lakini pia wacha niwaambie waafrika ukweli,
Japokuwa ukweli huu utakua mchungu kwa waafrika lakini wacha niwaambie;-

"Katika kipindi cha chini ya miaka 20 ijayo,
UFARANSA itakuwa koloni la makoloni yake ya zamani,
Wala sihitaji kuanzisha vita dhidi ya UFARANSA,
Kile ninachohitaji ni kuzikomboa nchi za AFRIKA,
Hasa zinazo zungumza lugha ya kifaransa ambazo,
Kwa muda mrefu zimekuwa makoloni ya UFARANSA,
Nikizikomboa hizi nchi zikawa na nguvu na miundombinu ya kiuchumi,
Pamoja na kiteknolojia na kujisimamia wenyewe kijeshi,
Lazima UFARANSA itaanguka yenyewe kama tunda lililooza liangukavyo kutoka kwenye mti,
Nani kati yetu sisi wa ULAYA asiyejua ukweli mchungu kuwa,
Ardhi ya AFRIKA ina uwezo wa kulisha ULAYA, AMERIKA na ASIA yote,
Lakini kitu pekee AFRIKA ilichokosa ni viongozi wenye akili,
AFRIKA imebarikiwa rasilimali adimu duniani,
Lakini shida inaviongozi waliolaaniwa, wabinafsi,hawana akili na wanaojali familia zao kuliko nchi zao,
AFRIKA ina utajiri mara 20 zaidi ya ULAYA,
Lakini AFRIKA ni masikini ni masikini takribani zaidi ya mara maelfu kimaendeleo,
Ninachoweza kuwaambia waafrika ni kwamba,
Kama viongozi wao watadhubutu kujitambua,
Na kuunda sarafu moja ya pamoja kwa ajili ya AFRIKA mzima,
Nawahakikishia nchi nyingi za ULAYA zitakuja kuomba misaada AFRIKA,
AFRIKA inamiliki 70% ya maliasili zinazopatikana ulimwenguni,
AFRIKA inamiliki 70% ya malighafi zinazotumika kuunda silaha za nyuklia,
Na wazungu wanajua hilo lakini kwa kejeli,
Bado mpaka leo hii MAREKANI na UFARANSA,
Wanaujasiri wa kuiita AFRIKA kuwa ni bara masikini zaidi duniani,
Kwasababu tu kuwa wazungu hao wamefanikiwa kuwashika akili waafrika,
Na waafrika wenyewe walivyo kama mazezeta,
Wanaamini kuwa kujipendekeza kwa wazungu ndiyo ujanja,
Na wanaamini kuwa ULAYA ni sehemu bora kuishi kuliko AFRIKA,
Na wanaliona bara lao ni kama sehemu mbaya kuliko mabara yote duniani,
Sasa nimeamua kumsapoti ndugu yangu TRAORE,
Kwasababu yeye ameonesha kuwa anajitambua,
TRAORE anajitambua sana kuliko viongozi wote wa AFRIKA na raia wao,
Mimi kama PUTIN kama RAIS wa URUSI,
Nasema hapa leo kuwa nipo tayari kumsaidia kiongozi yeyote atakae jitambua AFRIKA,
Ila ujitambue kwelikweli kama TRAORE,
Lakini kama utakuja kwangu ukaniomba msaada,
Na kuniambia kuwa sasa wewe na raiawako munajitambua,
Na unataka kuikomboa nchi yako kwa kunidanganya,
Utajuta kuzaliwa kwani URUSI huwa haipendi mambo ya kijinga kijinga".....amesema PUTIN

Makala hii imeletwa kwenu na Dhulkad Madara kutoka Morogoro
Leo Putin ameritoti tokea Morogoro!
 
Back
Top Bottom