Alichosema Pengo kuhusu kura ya maoni

Alichosema Pengo kuhusu kura ya maoni

East African Eagle

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2013
Posts
3,759
Reaction score
2,209
Wale ambao hamkumsikia live Mzee wa Hekima Mwanademokrasia wa kweli Kadrinali Pengo alichosema kuhusu wananchi kuachwa huru waamue kidemokrasia watapiga kura ya ndiyo au hapana bila kushinikzwa msikilize mwenyewe hapa

 
Last edited by a moderator:
Sawa...lakini kwa nini apingane na TEC?! Element za unafiki zinajionyesha.
 
Sawa...lakini kwa nini apingane na TEC?! Element za unafiki zinajionyesha.

Kwa hiyo ulitaka aunge mkono kitu kisicho sahihi kidemokrasia? Ambacho ukikiweka kwenye Mizani ya ukweli wa kidemokrasia hakina uzito? TEC Si mwenyezi mungu asiyekosea.
 
Sawa...lakini kwa nini apingane na TEC?! Element za unafiki zinajionyesha.

Kwa hiyo ulitaka aunge mkono kitu kisicho sahihi kidemokrasia? Ambacho ukikiweka kwenye Mizani ya ukweli wa kidemokrasia hakina uzito?

Kwa bahati mbaya sijaweza kusikiliza hiyo clip, imegoma. Ila Pengo ana uhuru na haki ya kutoa maoni yake binafsi kama raia wengine kuhusu katiba, sipingi hilo.

Tatizo ni pale kama na yeye ni miongoni mwa hao TEC na alikuwepo wakiweka msimamo wao na mbaya zaidi kama hauongelea mtazamo wake huko kwenye TEC hadi walipotoa tamko na yeye akaja kutoa toleo tofauti na wenzake patakua na tatizo.

Narudia tena, sijasikiliza hiyo clip huenda ni tatizo la kiufundi kwenye PC yangu, ila kwa mantiki wananchi inabidi waeleweshwe kuhusu katiba pendekezwa kisha wao waamue wanachotaka.
 
Wale ambao hamkumsikia live Mzee wa Hekima Mwanademokrasia wa kweli Kadrinali Pengo alichosema kuhusu wananchi kuachwa huru waamue kidemokrasia watapiga kura ya ndiyo au hapana bila kushinikzwa msikilize mwenyewe hapa

[video=youtube;2Z18]https://www.youtube.com/watch?v=2Z18[/video]

Hili jambo limeisha siku nyingi. Hata hiyo kura ya maoni itabaki kuwa historia kwa utawala wa Kikwete.
 
butiku sio dhambi kupiga kura ya hapana;baregu hiyo kura yenyewe haipo tena
 
Tatizo ni pale kama na yeye ni miongoni mwa hao TEC na alikuwepo wakiweka msimamo wao na mbaya zaidi kama hauongelea mtazamo wake huko kwenye TEC hadi walipotoa tamko na yeye akaja kutoa toleo tofauti na wenzake patakua na tatizo.

Kwenye dini kuna kitu cha kumrudia mwenyezi Mungu na kuomba msamaha pale ulipokosea na kugeuka na kuacha yale mabaya uliyokuwemo ndani yake au uliyokuwa na msimamo ambao haukuwa sahihi..Tamko lile hata kama aliliona baya baadaye na akaamua kujirudi kidini inaruhusiwa.Na yuko sahihi kugeuka toka ubaya uwe ubaya aliokubaliana na wengine au wa peke yake.Ukigundua kosa badilika kuanzia hapo ulipogundua.Hutakiwi kubaki kosani ETI KISA TULIKUBALIANA!!!!!!!!!!
 
Kwenye dini kuna kitu cha kumrudia mwenyezi Mungu na kuomba msamaha pale ulipokosea na kugeuka na kuacha yale mabaya uliyokuwemo ndani yake au uliyokuwa na msimamo ambao haukuwa sahihi..Tamko lile hata kama aliliona baya baadaye na akaamua kujirudi kidini inaruhusiwa.Na yuko sahihi kugeuka toka ubaya uwe ubaya aliokubaliana na wengine au wa peke yake.Ukigundua kosa badilika kuanzia hapo ulipogundua.Hutakiwi kubaki kosani ETI KISA TULIKUBALIANA!!!!!!!!!!

Ndio maana nikasema ana haki na ana uhuru wa kuongea chochote. Kama amegundua alikosea akajirudi nako sio mbaya, je, amelisema hilo kwamba alikosea na amejirudi na kuona kwamba alikosea mwanzo na anaamini kwamba hiki anachokisema sasa hivi ndio sahihi?
 
Ndio maana nikasema ana haki na ana uhuru wa kuongea chochote. Kama amegundua alikosea akajirudi nako sio mbaya, je, amelisema hilo kwamba alikosea na amejirudi na kuona kwamba alikosea mwanzo na anaamini kwamba hiki anachokisema sasa hivi ndio sahihi?

Si lazima awe alikosea.Naamini katika tamko lile kuna waliosaini lakini waliokuwa hawakubaliani na lile tamko.Ila kwa kuwa maamuzi huamriwa kwa kura basi yawezekana walipiga kura walikokubali wakashinda kwa kura na baada ya kushinda kwa kura wakamtaka kila mtu asaini naye akasaini lakini moyo wake ukiwa na msimamo ule ule alikokuwa nao kwenye upigaji kura.Na naamini kuna wengine walisaini pia ila hawakuunga mkono lile tamko wakati wa kulipigia kura.Ni woga tu utakuwa unawasumbua kutoa misimamo yao.Pengo jasiri namsifu haogopi kusema kile anakiamini.

Pia Mtu akibadilika si lazima asimame apige tarumbeta kuwa jamani eee nilikosea! Anachosema sasa ndio kichukuliwe.Mwizi ambaye alikuwa hakanyagi msikitini ukiona kashika msahafu anaswali swala tano na kabadilika maneno na matendo huna haja ya kumwuliza kuwa ulishasimama kutubu mbele za watu kuwa wewe si mwizi tena? Maneno yake ya sasa ndio msimamo sahihi.
 
Si lazima awe alikosea.Naamini katika tamko lile kuna waliosaini lakini waliokuwa hawakubaliani na lile tamko.Ila kwa kuwa maamuzi huamriwa kwa kura basi yawezekana walipiga kura walikokubali wakashinda kwa kura na baada ya kushinda kwa kura wakamtaka kila mtu asaini naye akasaini lakini moyo wake ukiwa na msimamo ule ule alikokuwa nao kwenye upigaji kura.Na naamini kuna wengine walisaini pia ila hawakuunga mkono lile tamko wakati wa kulipigia kura.Ni woga tu utakuwa unawasumbua kutoa misimamo yao.Pengo jasiri namsifu haogopi kusema kile anakiamini............

Sina swali la nyongeza mkuu! Pengo ni jasiri
 
Democrasia Maana yake nini ?

Kwa kupiga kura demokrasia ni Uhuru wa mpiga kura mwenyewekuielewa katiba na kujiamulia apige kura ya ndiyo au hapana pasipo kushawishiwa au kushinikizwa na mtu yeyote awe padri,askofu au machinga muuza sakramenti kariakoo.
 
Kwa hiyo ulitaka aunge mkono kitu kisicho sahihi kidemokrasia? Ambacho ukikiweka kwenye Mizani ya ukweli wa kidemokrasia hakina uzito? TEC Si mwenyezi mungu asiyekosea.
Sema neno lolote juu ya hao wanao himiza kuipitisha, kuikubali, kuiunga mkono.................
 
Kwa bahati mbaya sijaweza kusikiliza hiyo clip, imegoma. Ila Pengo ana uhuru na haki ya kutoa maoni yake binafsi kama raia wengine kuhusu katiba, sipingi hilo.

Tatizo ni pale kama na yeye ni miongoni mwa hao TEC na alikuwepo wakiweka msimamo wao na mbaya zaidi kama hauongelea mtazamo wake huko kwenye TEC hadi walipotoa tamko na yeye akaja kutoa toleo tofauti na wenzake patakua na tatizo.

Narudia tena, sijasikiliza hiyo clip huenda ni tatizo la kiufundi kwenye PC yangu, ila kwa mantiki wananchi inabidi waeleweshwe kuhusu katiba pendekezwa kisha wao waamue wanachotaka.

Mimi naona maaskofu walikuwa sahihi na Pengo hakuwa sahihi kwa sababu zifuatazo:
1. Maaskofu waliandika waraka wao katika mazingira ambayo kila kiongozi wa serikali alikuwa akisisitiza kura ya maoni itapigwa Aprili 30 wakati mchakato wa uandishwaji kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ulikuwa unaendelea kwa kusuasua, muda wa kutoa elimu ya uraia na kampeni vilikuwa bado vinazua maswali mengi kwa mujibu wa sheria na pia nakala za katiba hazikuwa zimewafikia wananchi wengi ambao wangeshiriki kupiga kura.
2. Kama wadau wengine walivyokuwa wameishaishauri serikali kuahirisha mchakato, maaskofu nao walitaka mchakato uahirishwe ili uandishwaji wa wapiga kura kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ufanyike vizuri na pia kuwe na nafasi ya kutosha ya kutoa elimu ya uraia na kampeni.
3. Pamoja na haya, serikali ilisisitza kura iko palepale!
4. Katika mazingira haya, maaskofu waliona kama serikali itaendelea kusisitiza "kura ya maoni iko palepale" wakati kuna hizo kasoro basi ni heri waumini washiriki kujiandikisha na waipigie kura ya hapana katiba inayopendekezwa.
5. Wanaoona kuwa maaskofu walikosea wanataka kusema kwamba mchakato wa kujiandisha, kutoa elimu ya uraia na kampeni na usomaji wa katiba na kuelewa maudhui yake kungewezekana tu by Aprili 30.
6. Sasa tujiulize hii ilikuwa kwa maslahi ya nani ikiwa hadi sasa watu wengi hawajajiandikisha na hawajaisoma hiyo katiba?
7. Katika mazingira haya kweli Pengo na wanaomwuunga mkono wanaona serikali ilikuwa sahihi tu kulazimisha kura ya maoni ifanyike Aprili 30?
8. Kitu kingine mbona serikali inawasihi wananchi kuipigia kura ya ndiyo katiba inayopendekezwa na hakuna anayeona ni kuingilia uhuru wa wananchi wa kuchagua (mfano ujumbe kuhusu katiba inayopendekezwa unaosomwa kila siku TBC)?
 
Sema neno lolote juu ya hao wanao himiza kuipitisha, kuikubali, kuiunga mkono.................

Kama wanaoongea ni wanasiasa.Wana haki zote sababu kazi ya mwanasiasa ni kuwa na upande wa wazi katika siasa.Mfano UKAWA wakisema pigeni kura ya hapana wako sahihi ndiyo sera za vyama vyao kwenye hilo la kura ya maoni.Na CCM wanachama wake na viongozi wake kuanzia chini hadi juu wakisema pigeni kura ya NDIYO wako sahihi sababu kisiasa ndio sera yake kwenye hilo la kura ya maoni.

Lakini inapokuja kiongozi wa dini ambaye ndani ya dini yake ana waumini wa UKAWA na CCM kuelekeza kuwa pigeni kura ya ndiyo au hapana anakuwa hajitambui kama kiongozi wa dini anajitambua kama UKAWA au CCM zaidi kuliko kiongozi wa dini.

Askofu pengo anajitambua kuwa yeye ni kiongozi wa dini si wa kisiasa hivyo kuwaelekeza waumini wapige kura kadri ya dhamiri zao.Kwa kusema hivyo kawatendea haki wote UKAWA na CCM na kajionyesha kuwa yeye ni mtu wa dini asiye na upande kama ambavyo wanasiasa wana upande.Kiongozi wa dini kabeba wanasiasa na wasio wanasiasa.Kuna wataka kupiga kura ya ndiyo,kuna wataka kupiga kura ya hapana.Kujipambanua na kundi fulani tamko lile la maaskofu halikuwa sahihi.Pengo yuko sahihi kama kiongozi wa dini.

Ina maana hata kama tamko lao lingesema watu wapige kura ya ndiyo bado wasingekuwa sahihi sababu kuna waumini wao wengine wataka kupiga kura ya hapana.
 
Kwa kupiga kura demokrasia ni Uhuru wa mpiga kura mwenyewekuielewa katiba na kujiamulia apige kura ya ndiyo au hapana pasipo kushawishiwa au kushinikizwa na mtu yeyote awe padri,askofu au machinga muuza sakramenti kariakoo.

Kwa hiyo CCM wanavyotuambia tupige kura ya Ndio wao Demokrasi hawaijui sio ?
 
Askofu pengo anajitambua kuwa yeye ni kiongozi wa dini si wa kisiasa hivyo kuwaelekeza waumini wapige kura kadri ya dhamiri zao.Kwa kusema hivyo kawatendea haki wote UKAWA na CCM na kajionyesha kuwa yeye ni mtu wa dini asiye na upande kama ambavyo wanasiasa wana upande.Kiongozi wa dini kabeba wanasiasa na wasio wanasiasa.Kuna wataka kupiga kura ya ndiyo,kuna wataka kupiga kura ya hapana.Kujipambanua na kundi fulani tamko lile la maaskofu halikuwa sahihi.Pengo yuko sahihi kama kiongozi wa dini.

Kama Pengo ni kiongozi wa dini na ana watu wa aina zote na kwa mtazamo wako, hakutakiwa kabisa kuongelea suala la katiba, achilia mbali kuwaambia watu aidha wapige kura ya ndio au hapana. Yeye angeendelea na mambo ya dini tu.

Kwa muktadha huo, kama aliamua kuliongelea suala la katiba, alitakiwa kwanza akemee na kuonya wale wote wanao wasisitiza wananchi (Waumini) kupiga kura ya ndio au hapana ikiwemo CCM, Taasisi zingine n.k

Kama ni shujaa na kweli aliamua kuliongelea hili la katiba alitakiwa aliongelee lote na kwa ukamilifu. Katiba pendekezwa yenyewe tumeona ilivyoshinikizwa kupita kuanzia bungeni hakuliona hilo?
 
Kwa hiyo CCM wanavyotuambia tupige kura ya Ndio wao Demokrasi hawaijui sio ?

CCM wako sahihi na UKAWA wako sahihi ila viongozi wa dini hawako sahihi.

Sababu viongozi wa dini hawatakiwi kuwa na upande (PARTISAN) sababu wao ni viongozi wa wote UKAWA na CCM

CCM na wanasiasa WENGINE WOTE haki zote sababu kazi ya mwanasiasa ni kuwa na upande fulani na kushawishi wapiga kura upande huo ndio siasa zenyewe.Mfano UKAWA wakisema pigeni kura ya hapana wako sahihi ndiyo sera za yao .Na CCM wanachama wake na viongozi wake kuanzia chini hadi juu wakisema pigeni kura ya NDIYO wako sahihi sababu kisiasa ndio sera yake kwenye hilo la kura ya maoni.

Lakini viongozi wa dini wakisema pigeni kura ya ndiyo au hapana au msiende kupiga kura hapo unajua sasa viongozi wa dini walishaacha dini wameanza kuvuta bangi.Sababu wanajipambanua kiitikadi.HILI TAMKO LA MAASKOFU LIKO CHINI YA KIWANGO NA NI AIBU KULIITA TAMKO LA MAASKOFU LOOOOOO!!!! AIBU TUPU UTAFIKIRI HATA KUSOMA HAWAKUSOMA
 
Back
Top Bottom