kipara kipya
JF-Expert Member
- May 2, 2016
- 14,150
- 16,139
Miezi minne iliyopita kuna mzee aliondoka hapa kijiji cha masakata wilayani tunduru kuelekea jijini dar es salaam 'jiji la maraha.
kwenda kushughulikia miamala ya pesa zake za mafao baada ya kuhudumu serikalini kwa kipindi kirefu,
Mzee aliondoka mwezi wa tano mwaka huu kwa kumuaga bi mkubwa kuwa atarejea baada ya wiki moja.
Pia kukiwa na shabaha ya kurudi na pesa za kuwekea sawa mashamba yao,
,kweli alifika mjini akakutana na mwanawe mkubwa wa kike aliyemsaidia kurahisisha shughuli zake za kibenki.
Huyo mwanawe naye kidogo alihamdulillah anahudumu kwenye wizara moja nyeti,
Baada ya kuchukua maokoto mzee aliweza kutupa kiasi cha pesa kwa bi mkubwa baada ya hapo,
mzee hakupatikana tena si kwa simu wala salamu .
Watu walihangaika vituo vya polisi na mahospitalini ,mochwari ,baa zote na vijiwe vya kahawa ,ikawa hakuna majibu.
Cha kushtusha ni jana mzee amepatikana huko mbezi kwenye nyumba moja amefungiwa na binti mmoja umri wa mwanawe ,akiwa hana hata wasiwasi na hajui kama watu wanahangaika wala kaacha bi mkubwa huko home.
Mzee amekamata remote hana hata mashaka bi mdogo amemmwagia udambwi dambwi juu ya meza,
baada ya kumkuta hapo palizuka vurumai kubwa nguo kuchanika ili kumtoa mzee pale nyumbani kwa bi mdogo.
Huku mzee akiapa kutaka kuwaachia radhi watoto wake na bi mdogo akitaka kuwafungulia mashtaka watoto wa mzee kumletea fujo nyumbani kwake!
Angalizo :wazee wasiachwe peke yao kwenda kufanya miamala wasije angukia kwenye mikono isiyo salama!
kwenda kushughulikia miamala ya pesa zake za mafao baada ya kuhudumu serikalini kwa kipindi kirefu,
Mzee aliondoka mwezi wa tano mwaka huu kwa kumuaga bi mkubwa kuwa atarejea baada ya wiki moja.
Pia kukiwa na shabaha ya kurudi na pesa za kuwekea sawa mashamba yao,
,kweli alifika mjini akakutana na mwanawe mkubwa wa kike aliyemsaidia kurahisisha shughuli zake za kibenki.
Huyo mwanawe naye kidogo alihamdulillah anahudumu kwenye wizara moja nyeti,
Baada ya kuchukua maokoto mzee aliweza kutupa kiasi cha pesa kwa bi mkubwa baada ya hapo,
mzee hakupatikana tena si kwa simu wala salamu .
Watu walihangaika vituo vya polisi na mahospitalini ,mochwari ,baa zote na vijiwe vya kahawa ,ikawa hakuna majibu.
Cha kushtusha ni jana mzee amepatikana huko mbezi kwenye nyumba moja amefungiwa na binti mmoja umri wa mwanawe ,akiwa hana hata wasiwasi na hajui kama watu wanahangaika wala kaacha bi mkubwa huko home.
Mzee amekamata remote hana hata mashaka bi mdogo amemmwagia udambwi dambwi juu ya meza,
baada ya kumkuta hapo palizuka vurumai kubwa nguo kuchanika ili kumtoa mzee pale nyumbani kwa bi mdogo.
Huku mzee akiapa kutaka kuwaachia radhi watoto wake na bi mdogo akitaka kuwafungulia mashtaka watoto wa mzee kumletea fujo nyumbani kwake!
Angalizo :wazee wasiachwe peke yao kwenda kufanya miamala wasije angukia kwenye mikono isiyo salama!