Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 7,206
- 12,702
Nitaweka hapa hadithi zote, kutoka vitabu vyote(vinne ) vya Alfu lela ulela. Fuatana nami kwenye safari hii ndefu. Pia vyote unaweza kuvisoma bure ndani ya maktaba app.
Tuanze na kitabu cha nne.
Utangulizi
Kisa cha Baba-Abdalla kipofu
Kisa cha Sidi-Nouman
Kisa cha Ali Kogia, Mfanyi biashara wa Baghdadi
Farasi wa uchawi
Kisa cha ndugu wawili wanawake waliomwonea kijicho dada yao mdogo
HADITHI zinazohadithiwa, zimekuwa kama zile zinazotolewa na wazee wanawake wa nchi mbali mbali wakiwahadithia wajukuu zao. Hapana mtu anayejua ni za tangu lini, au ni nani aliyezitoa kwanza. Labda watoto wa Ham, na Shem, na Japhet (Jaffari) walizisikia katika Safina, siku za Gharika!
Watu wa nchi zingine huzihadithia kwa njia mbali mbali lakini
hadithi ni zile zile moja, hata kwa watoto wadogo wa Kizulu walio Cape, au kwa watoto wadogo wa Kieskimo walio pwani ya kaskazini mwa nchi ya Amerika. Kubadilika huku kumetokea kwa ajili ya tabia na desturi za nchi, kama vile kuvaa au kutovaa nguo.
Katika hiadithi hizi mna wafalme wengi na malkia wengi, kwa sababu hapo zamani kulikuwa na wafalme wengi katika nchi, na yule mtu ambaye sasa ana heshima kwa watu, hapo zamani za kale alikuwa namna ya mfalme. Hadithi hizi za kale haziwezi kusahauliwa kabisa kwa maana ziliandikwa kwa miaka mbali mbali, lakini nyingi ni za karne hii ya sassa ambazo ziliandikwa kwa lugha za kila namna.
Hadithi hizi za "Alfu-lela-ulela," ambazo zingine, ingawa si zote, zimo katika kitabu hiki, ni hadithi za Mashariki. Wahindi na Waarabu na Waajemi, huzitoa kwa namna zao wenyewe, Lakini si kwa watoto, ila kwa watu wazima. Ni kweli kuwa hapo zamani kulikuwa hakuna vitabu vya hadithi, wala vitabu vilivyopigwa chapa, lakini kulikuwa na watu maalum ambao kazi zao zilikuwa ni kuwafurahisha wanawake na wanaume kwa kuwatolea hadithi, nao walikuwa wakiwatolea hadithi kwa kuwasifia vema Waislamu wanaokaa Baghdadi au Bara ya Hindi. Na mara kwa mara hudhaniwa kuwa mambo hayo yote yalitokea zamani za enzi ya Khalifa Mkuu, au Mtawala wa Uaminifu, Harun Rashid, aliyekaa Baghdadi tangu mwaka 786 hata 808, na huyo waziri wake aliyekuwa akia- ndamana naye vile vile alikuwa mtu wa kweli, katika ukoo mkubwa wa Mabamiside. Naye aliuawa na Khalifa kwa ukatili sana, wala hapana mtu ajuaye sababu yake. Katika kulikumbuka deni la mapenzi niliokopeshwa ambalo siwczi kulilipa nafurahi kumsheheneza shukurani za kweli Bwana A. A. M. Isherwood, O.B.E., M.A., Deputy Director of Education Bwana F. Johnson, Esq., Chairman of Publication Committee na mabwana wengine wote walio wanachama wa Publication Committee, na mwenyewe Bwana S. Rivers-Smith, C.B.E, M.A., The Hon'ble the Director of Education, kwa jinsi walivyokuwa radhi kunisaidia kwa mapenzi, katika kukisifia kitabu hiki changu hata kikapatikana kupigwa chapa.
Na hivi natumaini kwamba wasomaji wote watakaokipenda
kitabu hiki, wataungana nami katika kulishuhudia deni langu.
DAR ES SALAAM,
1st January, 1928.
Tuanze na kitabu cha nne.
MAZUNGUMZO YA ALFU LELA ULELA
AU
SIKU ELFU NA MOJA
KIMEFASIRIWA KWA KISWAHILI NA
EDWIN W. BRENN
KITABU CHA NNE
YALIYOMO
AU
SIKU ELFU NA MOJA
KIMEFASIRIWA KWA KISWAHILI NA
EDWIN W. BRENN
KITABU CHA NNE
YALIYOMO
Utangulizi
Kisa cha Baba-Abdalla kipofu
Kisa cha Sidi-Nouman
Kisa cha Ali Kogia, Mfanyi biashara wa Baghdadi
Farasi wa uchawi
Kisa cha ndugu wawili wanawake waliomwonea kijicho dada yao mdogo
UTANGULIZI
HADITHI zinazohadithiwa, zimekuwa kama zile zinazotolewa na wazee wanawake wa nchi mbali mbali wakiwahadithia wajukuu zao. Hapana mtu anayejua ni za tangu lini, au ni nani aliyezitoa kwanza. Labda watoto wa Ham, na Shem, na Japhet (Jaffari) walizisikia katika Safina, siku za Gharika!
Watu wa nchi zingine huzihadithia kwa njia mbali mbali lakini
hadithi ni zile zile moja, hata kwa watoto wadogo wa Kizulu walio Cape, au kwa watoto wadogo wa Kieskimo walio pwani ya kaskazini mwa nchi ya Amerika. Kubadilika huku kumetokea kwa ajili ya tabia na desturi za nchi, kama vile kuvaa au kutovaa nguo.
Katika hiadithi hizi mna wafalme wengi na malkia wengi, kwa sababu hapo zamani kulikuwa na wafalme wengi katika nchi, na yule mtu ambaye sasa ana heshima kwa watu, hapo zamani za kale alikuwa namna ya mfalme. Hadithi hizi za kale haziwezi kusahauliwa kabisa kwa maana ziliandikwa kwa miaka mbali mbali, lakini nyingi ni za karne hii ya sassa ambazo ziliandikwa kwa lugha za kila namna.
Hadithi hizi za "Alfu-lela-ulela," ambazo zingine, ingawa si zote, zimo katika kitabu hiki, ni hadithi za Mashariki. Wahindi na Waarabu na Waajemi, huzitoa kwa namna zao wenyewe, Lakini si kwa watoto, ila kwa watu wazima. Ni kweli kuwa hapo zamani kulikuwa hakuna vitabu vya hadithi, wala vitabu vilivyopigwa chapa, lakini kulikuwa na watu maalum ambao kazi zao zilikuwa ni kuwafurahisha wanawake na wanaume kwa kuwatolea hadithi, nao walikuwa wakiwatolea hadithi kwa kuwasifia vema Waislamu wanaokaa Baghdadi au Bara ya Hindi. Na mara kwa mara hudhaniwa kuwa mambo hayo yote yalitokea zamani za enzi ya Khalifa Mkuu, au Mtawala wa Uaminifu, Harun Rashid, aliyekaa Baghdadi tangu mwaka 786 hata 808, na huyo waziri wake aliyekuwa akia- ndamana naye vile vile alikuwa mtu wa kweli, katika ukoo mkubwa wa Mabamiside. Naye aliuawa na Khalifa kwa ukatili sana, wala hapana mtu ajuaye sababu yake. Katika kulikumbuka deni la mapenzi niliokopeshwa ambalo siwczi kulilipa nafurahi kumsheheneza shukurani za kweli Bwana A. A. M. Isherwood, O.B.E., M.A., Deputy Director of Education Bwana F. Johnson, Esq., Chairman of Publication Committee na mabwana wengine wote walio wanachama wa Publication Committee, na mwenyewe Bwana S. Rivers-Smith, C.B.E, M.A., The Hon'ble the Director of Education, kwa jinsi walivyokuwa radhi kunisaidia kwa mapenzi, katika kukisifia kitabu hiki changu hata kikapatikana kupigwa chapa.
Na hivi natumaini kwamba wasomaji wote watakaokipenda
kitabu hiki, wataungana nami katika kulishuhudia deni langu.
E. W. BRENN
DAR ES SALAAM,
1st January, 1928.