Mgirik
JF-Expert Member
- Apr 27, 2013
- 13,204
- 13,182
Mmmhhhh!!!! Dunia hii ina viumbe hatar sana ..Kila jambo lina wakati wake... Na hakuna kitu kinnatokea bila sababu.... Kuna wakati wa kulia na kuna wakati wa kucheka...
Mmmhhhh!!!! Dunia hii ina viumbe hatar sana ..Kila jambo lina wakati wake... Na hakuna kitu kinnatokea bila sababu.... Kuna wakati wa kulia na kuna wakati wa kucheka...
@rrondo hakuna niliposema nawachukia matajiri ama nauchukia utajiri... Bali nimeelezea njia ya kupita... Hata mimi naupenda utajiri... Anayechekia utajiri au matajiri....! ni mtazamo wake usimhukumu.... Nimependa leo kuweka kumbukumbu sawa... Wakati wengine wakifurahi leo... Wengine wanatoneshwa makovu ya vidonda vilivyosababishwa na matokeo ya ubinafsi choyo na udhalimuMshana Jr na wewe unawachukia matajiri? Huo mchezo wa vyakula vibovu bado unaendelea na wanaojaribu kupambana nao wanaitwa maadui wa uchumi na watu wachukiao matajiri.
Niko pamoja nawe. Kuna watu hawakuelewi na hawatakuekewa kwao matajiri ni kama mungu.@rrondo hakuna niliposema nawachukia matajiri ama nauchukia utajiri... Bali nimeelezea njia ya kupita... Hata mimi naupenda utajiri... Anayechekia utajiri au matajiri....! ni mtazamo wake usimhukumu.... Nimependa leo kuweka kumbukumbu sawa... Wakati wengine wakifurahi leo... Wengine wanatoneshwa makovu ya vidonda vilivyosababishwa na matokeo ya ubinafsi choyo na udhalimu
Nakumbuka ilikuwa miaka ya tisini na kampuni husika ndio huyu alipatikana bila mikwaruzo tena walidondoka karibu watu wanne wa ofisi ya mkemia.Alfajiri ya leo tarehe 20.10.2018 imepokelewa na watu wengi kwa furaha kubwa baada ya kuenea taarifa za kupatikana salama mfanyabiashara kijana bilionea Mohammed Dewji... Ni furaha kwa familia, ndugu jamaa na marafiki na wale wote wasioamini katika udhalimu.....
Mwishoni mwa utawala wa rais Ali Hassan Mwinyi (CCM) mwaka 1989-90... Lilitokea jambo baya sana lililoitia nchi yetu DOA kubwa sana... Mauaji ya kutisha ya Dr. Fupi aliyekuwa mkemia mkuu wa serikali kipindi hicho... Uzalendo wa nchi yake... Utu wema wake, uamunifu na chuki dhidi ya rushwa vilisababisha maisha yake yakatishwe... Akiacha mjane na watoto wawili
Udhalimu, uchoyo, ubinafsi kukosa huruma, hamu kubwa ya kupata kuliwafanya watu wanaojifanya watu Mungu sana kusahau utu wao na kufanya ukatili mkubwa kwa mtu aso hatia! Wakaichukua roho yake mchana kweupe, na kuiachia familia yake majonzi makubwa na machozi ya milele!
Nini kilitokea!?
Kulikuwa na kampuni moja iliyokuwa inajishughulisha na uuzaji wa nafaka... Kampuni hii ilikuwa na mabohari makubwa hapa DSM... Basi kukawa na uhitaji mkubwa wa mchele na ngano kipindi hicho, na kampuni husika ikaingiza tani za kutosha ili wananchi wapate chakula na kampuni ipate pesa
Mchele ule uliingizwa toka uarabuni kupitia Zanzibar nadhani.. Habari zikavuja kwamba mchele ule haukufaa kwa matumizi ya binadamu, ulikuwa umeshaharibika... Kuthibitisha tuhuma hizi ikabidi mkemia mkuu wa serikali aitwe kuupima...!
Mkemia akafanya kazi yake kwa uaminifu na weledi mkubwa akishirikiana na senior lab technician mmoja... Hawa wawili wakaheshimu kiapo chao cha kazi.. KUTENDA KWA WELEDI NA UAMINIFU... Dr Fupi akatoa majibu yake kuwa mchele ule haufai kwa matumizi ya binadamu, yoyote ayakayeutia atapata madhara makubwa ya kiafya yajayo taratibu....
Wenye mali wakapingana na majibu ya mkemia mkuu wa serikali... Malumbano yakaanzia hapo, vitisho nk... Lakini Dr Fupi akashikilia msimamo wake!
Mwishoni mwa wiki ile ya malumbano Dr Fupi akiwa nyumbani kwake akapata ugeni.. Kuchungulia getini akaona hawa si watu wema kwakuwa walikuwa wanaparamia ukuta... Dr kwa haraka akaomba msaada wa polisi wa vituo mbalimbali (alikuwa anaishi Oysterbay)
. Kituo no moja simu ilikuwa busy
. Kituo no mbili gari haikuwa na mafuta
. Kituo no tatu kilipokea wito lakini wakafika kwa kuchelewa kidogo...
Watu wale wabaya waliingia ndani kwake kwa kuvunja mageti na milango na wakamkuta Dr akiendelea kuomba msaada.. Walimkatakata mpaka akakata roho.... Wakaondoka bila kuchukua kitu chochote...
Wiki iliyofuata msaidizi wake akakaimu nafasi yake na kutoa haraka cheti cha ubora wa mchele husika na bidhaa husika ikaingizwa sokoni, huku familia ya Dr Fupi ndugu na jamaa wakiwa kwenye majonzi makubwa ya kumpoteza baba yao... Yule senior lab technician pia alikufa inasemekana kwa sumu....
Kampuni husika ilituhumiwa sana kwenye hili lakini wakati huo Mzee Malecela akiwa mwenye nguvu kubwa akalimaliza ajuavyo yeye....
Maneno ya Mungu yanasema ni rahisi kwa ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuurithi ufalme wa mbinguni.. (Ngamia sio mnyama ni lile kamba kubwa la kushikilia chombo kinapoweka nanga ufukweni ama baharini)
Mbele ya nuru ya mafanikio ya matajiri nyuma yake kuna giza lililojaa udhalimu tupu.....
Ngazi za kuwafikisha watu wengi kwenye kilele cha mafanikio ya kibiashara zimeshikiliwa na mafuvu na mifupa ya wahanga wengi sana!
Ni weekend ya furaha MO kapatikana.... Ni weekend nyingine ya huzuni kubwa kwa familia ile ya Dr Fupi iliyopokwa mpendwa wao hali wakiwa bado wanamhitaji sana... Nitamlilia daima shujaa huyu wa uzalendo asiyekumbukwa popote!
Kusoma hujui, hata picha huoni?Mkuu Mshana Jr hebu weka wazi kidogo..
Kwann umeandika maada hii Leo baada ya kupatkana kwa Mo?
Je hyo kampuni iliyokuwa imeagiza Michele ni kampuni gani?
Mmiliki wake ni nani?
Hizo kelele zisaidie pia kupatikana kwa Ben Saanane.Acha ujinga tena muda si mrefu mtasema ile gari ni ya mbowe. Kapatikana kwa sababu ya kelele za dunia nzima. Pia mlitaka kuaminisha dunia kuwa si chadema tu watekwao hata wanaccm. Sasa movie imebuma. Angalia kama MO anawatazama usoni hao jamaa.
Watakuelewa wachache sana. RIP Dr. Fupi mzalendo uliyepotezwa na walafi.
Kampuni husika wakati huo iliwapoteza wafanyakazi wake wengi tu, wengine walifanyiwa unyama na ukatili wa kutisha na kutosha...Niko pamoja nawe. Kuna watu hawakuelewi na hawatakuekewa kwao matajiri ni kama mungu.