Albert Msando afunguka kuhusu Zitto Kabwe

Kama haya maswali yameongelewa na wakili msomi, na ikawa bahati mbaya alikuwa wakili wa Zitto, hapa lazima tu Zitto angepoteza kesi.


Wakati wanaamua kwenda mahakamani, hawakujua wanacheza kamari na kipengele cha katiba? Hiyo katiba leo inaonekana onevu na viongozi wanaonekana hawafai. Wakati inaandikwa Zito hakuwa kiongozi? Alipopitisha hicho kipengele alikuwa naibu katibu mkuu, leo kimemhukumu, anaanza kukimbia kivuli chake.

Zito amekuwa akiyumbishwa a mawazo ya watu wasiokuwa na maono sahihi na wasijali hatma yake. u
Mmeshahoji kwa ni ni Zito alianzisha ACT akiwa ndani ya CHADEMA? Halafu bado mnawalazimisha CHADEMA wamuone ni mwanachama mwadilifu na mwaminifu kwa chama chao?

Double Standards hapana. Acheni kabisa!.

BTW, huyo mheshimiwa msomi, anapaswa kuelewa kwamba Chadema ni Democrasia pevu na si "utawala holela kama anavyotaka kulazimisha".

Mchana mwama.





 
Zitto asamehewe chondechonde baba yetu mhe.Mbowe, wanachadema tusamehe na tusahau yaliyopita, zitto asamehewe bure bila masharti nawaombeni, tusimuache aende.
 
Last edited by a moderator:
Uzuri wa msando ndiyo huu yuko wazi kabisa haogopi mtu hata mmoja.
 
Kama haya maswali yameongelewa na wakili msomi, na ikawa bahati mbaya alikuwa wakili wa Zitto, hapa lazima tu Zitto angepoteza kesi.

Mkuu Tabby nakukubali sana kwenye kujenga hoja. KUDOS
 
Last edited by a moderator:
Zitto asamehewe chondechonde baba yetu mhe.Mbowe, wanachadema tusamehe na tusahau yaliyopita, zitto asamehewe bure bila masharti nawaombeni, tusimuache aende.
Mkuu umechelewa sana huu msamaha wako hilo chama lenu la kibabe kama hilo nani atakusikiliza wewe sisimizi.
 


- Mnasema haya maswali yameandikwa na Mwanasheria? Pole sana Zitto I hope now utajifunza na hawa wanasheria wa Instagram

- Le Mutuz
 
Huyu ndiyo mnamuita wakili msomi?

Kuna kipengele ndani ya katiba ya CHADEMA inasema"mtu yyt atakaye kishtaki chama mahakamani atapoteza sifa ya kuwa mwana CHADEMA"

Mapumbavu Nyie chama kisishitakiwe shauri lisipelekwe mahakamani ....acheni udikteta
 
- Mnasema haya maswali yameandikwa na Mwanasheria? Pole sana Zitto I hope now utajifunza na hawa wanasheria wa Instagram

- Le Mutuz

Tena mwanasheria msomi wa kitivo cha sheria cha UDSM anayependa ku-floss wekundu wa Msimbazi Instagram....
 
Hoja/maswali yote 9 yanajibiwa na jibu moja..Msando go back to class
 
Tena mwanasheria msomi wa kitivo cha sheria cha UDSM.

- hahahahahahaha yupo Instagram sana nilimuonya Zitto wiki Tatu zilizopita kwamba anakoelekea na huyu Mwanasheria wake siko I hope amenielewa now, hahahahaha this is a big joke!!

Le Mutuz
 
Zitto asamehewe chondechonde baba yetu mhe.Mbowe, wanachadema tusamehe na tusahau yaliyopita, zitto asamehewe bure bila masharti nawaombeni, tusimuache aende.

Wazo lako ni kama langu
Kumbuka kuwa hii kesi kushinda kwa CDM si kwamba ni kitu hakikupangwa kwasababu jambo hili kama nikweli lilivyoamulwa lilitakiwa kuisha siku nyingi, lakini ka kipindi hicho Zitto alikuwa na manufaa kwa CCM, kwa kuchochea mgogoro CDM. Taabu imekuja baada ya ESCROW, kwa kuwa amekuwa mwiba, na inasemekana kuna kashfa nyingine anataka kuibua ambazo kwa hakika zitakuwa mwiba kama zitagusa watu kama Magufuri na Mwakyembe ambao ndio wanaonekana wasafi.
Imebidi ashindwe kesi ili avuliwe uanachama na ubunge na iwe afueni kwa CCM.

Tundu Lissu nae kabla hata ya kutafakari janja hiyo kakurupuka kutaka sifa.

Walitakiwa kama chama kuangalia maslahi mapana ya nchi na UKAWA, hata kama wasimrudishe kundini wangekaa kimya.

Eti ndio wanataka kuing'oa CCM, kwa ujinga huu watasubiri sana. Hapo hawajatangaza mgombea, fikiria nini kitatokea.. Hela hazijamwagwa bado, tayari wanang'oana mno.

Mbuzi kabisa.
 
Amini usiamini Ubinafsi,Chuki,Ufisadi,mihemko,kutokupenda mawazo tofauti na ya Mwenyekiti vinaimaliza Chadema.
 
Nn maana ya demokrasia?kma swala haljapatikana muafaka ndan ya chama hachukue hatua gan?katiba ya chama ni ya kidikteta nafkria inapnga wanachama kwenda mahakaman il iwakandamize kwa maslai ya wachache.shame chadema

Zitto ameitumikia hiyo katiba ya kidikteta kwa muda gani sasa?..kama na ye alikuwa muumini wa hiyo katiba ya kidikteta basi hiyo hiyo ndo imemuhukumu
 

Bora mkuu umeliona hilo,Kwa style hii chama tawala kitatawala mpaka kitakapotokea chama mbadala.
 
haya yaliyompata zitto...ni kwa mjibu wa katiba.....sijui kama zitto alikuwa aware na hicho kipengere au la!
CHA KUJIFUNZA
kwa sasa watanzania tupo kwenye mchakato wa kupigia kura katiba mpya....chonde chonde tusije tukaipigia kura ya ndiyo kama hatujui nini tunakipa hiyo ndiyo...tusije tukawa kitimoto baadaye kwa kujikaanga kwa mafuta yake. tusome katiba tuielewe japo kidogo afu ndo tupigie kura ya kuiunga mkono. nje ya hapo bora kura ya hapana.
 
Zitto ameitumikia hiyo katiba ya kidikteta kwa muda gani sasa?..kama na ye alikuwa muumini wa hiyo katiba ya kidikteta basi hiyo hiyo ndo imemuhukumu

Nchi hii kuipata kwasasa ni ndoto.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…