Albadir iliyosomwa Tanga

Albadir iliyosomwa Tanga

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
361,112
Reaction score
831,778
Inasemekana ndio albadir mbaya zaidi kuwahi kusomwa, maana madhara yake yalikumba hata wasiohusika. Ilisomwa kwa niaba ya Mzee mmoja wa kidigo baada ya kuchoka kuibiwa nazi zake na vijana wa Tanga mjini, na alifikia maamuzi hayo baada ya kutoa onyo na tahadhari!

Albadir ile ilikausha majani ya njia walimopita wezi, visu vilivyotumika vilikatikakatika, punda aliyebeba alikufa, gari ya punda ikiharibika vibaya, wezi wote walikufa wameachama huku nguo za siku ya tukio zikiwa kama zimemwagiwa tindikali, miili yao ilioza kwa kasi ya ajabu hata kabla ya kuzikwa, yeyote alinunua ama kuhusika na zile nazi alipata madhara ya ugonjwa na kifo.....

Inasemekana makaburi ya wale wezi vijana wane, hayakuota majani kwa miaka mingi. Tukio la kushambuliwa TL liliwaumiza na kuwasononesha watu wengi, ndani na nje ya nchi.. Wengi walilichukulia kama uonevu mkubwa

Kitu hicho kikapelekea kuja na wazo la kusoma kisomo cha albadir kwakuwa kulikuwa na hisia kwamba haki haitatendeka...
Visomo husika vilisomwa japo si kwa mafanikio sana kwakuwa zilitumika nguvu kubwa sana kuvizuia lakini vilisomwa kwa siri kwenye baadhi ya maeneo...

Lakini hata kama visingesomwa ile hali tu ya kusononeka kwa watu wengi kwa pamoja na kutajataja visomo, kiroho hali hiyo ilileta athari kwa wahusika (hapa nitapingwa na baadhi ya watu)

Baada ya hapo yameanza kutokea mambo ambayo ukiyatazama kwa jicho la kiroho kisha ukaunganisha dots ni kama vile kuna uhalisia unaoshabihiana na visomo vilivyosomwa....

Athari za visomo vya albadir wakati mwingine si lazima afe mtu, bali hata kuchanganyikiwa na kuharibikiwa kwa mambo pia yaweza kuwa ni matokeo ya kisomo

Visomo vimepingwa na kukosolewa kwa maelezo marefu mengine yakiwa hayaeleweki lakini asikudanganye mtu kisomo ni kisomo tuu. Usijaribu kabisa kukidharau

Jerry Muro kijana aliyechipukia kwenye uandishi wa habari hata kufikia kupata tuzo, ni muwewesekaji namba moja.. Achana na yaliyowahi kumkuta huko nyuma bado alikuwa anaweza kuandika hoja na ikaeleweka....

Lakini sasa inafika mahali unamuonea imani... Haeleweki anaandika nini na kila anachoandika kinakuwa na mapungufu mengi kuliko ya goma langu cocochanel

Najiuliza Jerry anayejivunia kupata degree moja nchi tatu tofauti ana nini na CHADEMA? Ana nini na TL!? Ana nini na akina Nasari na Lema? Ni kisomo kimempata ama kuna asili yenye mizizi mirefu iliyokuja kuzaa chuki kubwa namna hii? Je kuna wakati pengine alitaka kuingia CHADEMA na kutegemea apate nafasi halafu akakosa?

Vyovyote iwavyo Jerry ni mhanga mkubwa wa yanayotokea sasa na yamemjeruhi kwa namna ya kipekee kabisa na ni katikati ya kiwewe hicho anakaribia kuwehuka kabisa na kuropoka hata ambayo hakupaswa kuyasema... Kuna faida katika kuweweseka kwake!

Kuna faida kwenye kuropoka kwake! Anatufunulia mengi ambayo tungetumia muda mwingi na nguvu pia kuyajua. Ni wakati wetu sasa tuvute viti, tukae kimya tuli kabisa tutege masikio, wanaoweweseka wanazidi kuongezeka... Visomo haviendagi bure
 
Mshana Jr Mimi sio muislam ila hivi vitu ni common sana kwa wale wanaotoka sehemu zenye Muslim wengi si kitu cha kushangaa
Kwetu kule kondoa kunavijana waliiba mazulia ya msikitini kikapigwa hicho kinachoitwa kisomo mkuu watu walioza kabla hawajafa nikasema kwa kweli hii kitu hii ni hatari
 
Aah tujadilini mambo ya maana bwn, huyu Muro acha apambane na hali yake. Zama zimemuishia na hakuna alichofanya, amejaribu kutafuta bahati yake huku na huko wap, sasa kaparamia siasa, anajenga hoja kama za soka ufungwe au ufunge mshindi unabaki kuwa wewe tu
 
Mshana Jr Mimi sio muislam ila hivi vitu ni common sana kwa wale wanaotoka sehemu zenye Muslim wengi si kitu cha kushangaa
Kwetu kule kondoa kunavijana waliiba mazulia ya msikitini kikapigwa hicho kinachoitwa kisomo mkuu watu walioza kabla hawajafa nikasema kwa kweli hii kitu hii ni hatari
Inaitwa tindikali ya kiroho kuna wengine huanza kufa kwa kunyonyoka nywele kucha ngozi hatimaye nyama.. Ni vifo vya mateso mno
 
Duuu imekuwaje huyu
embe dodo hilo ukishindwa kulila bichi na pilipili subiria liive!
huyu ni mpunga nahisi ile albadir ya naz huko tanga ilimpitia na huyu baada ya kuokota kifuu tuu na kujipikilisha
 
embe dodo hilo ukishindwa kulila bichi na pilipili subiria liive!
huyu ni mpunga nahisi ile albadir ya naz huko tanga ilimpitia na huyu baada ya kuokota kifuu tuu na kujipikilisha
Mungu bado sijaelewa nakiri wazi kabisa sijaelewa
 
IMG-20171003-WA0054.jpg
 
Back
Top Bottom