Nazjaz
JF-Expert Member
- Jan 20, 2011
- 7,802
- 9,280
Kikundi cha wapiganaji wa Kiislamu wa
Somalia, al Shabaab, kinasema kuwa
kimeondoka katika vituo vyake kadha ndani
ya mji mkuu, Mogadishu.
Wakaazi wameiambia BBC kwamba waliona
misafara ya wapiganaji ikiondoka katika mji
huo.
Kuhama huko kunafuatia mapigano makali
jana usiku.
Kikosi cha Umoja wa Mataifa kinachoisaidia
serikali ya Somalia kimekuwa kikipigana na
al Shabaab mjini Mogadishu katika siku za
karibuni; ili kuweza kufikisha msaada wa
chakula kwa wale walioathirika na ukame
nchini Somalia.
Haijulikani kama wapiganaji hao
wameondoka kabisa.
Msemaji wa serikali alielezea huo kuwa
"ushindi wa dhahabu" kwa watu wa
Somalia.
Lakini al Shabaab, ambayo inadhibiti
sehemu kubwa ya kusini mwa nchi, ilisema
wameondoka kufwatana na mikakati yao na
iliahidi kufanya shambulio la kulipiza.
Baadhi ya wadadisi wanafikiri al Shabaab
imepungukiwa na fedha kwa sababu
wafadhili wao wa Arabuni
wamewapunguzia msaada tangu al
Shabaab kudhoofika kijeshi.
Wadadisi wanasema al Shabaab imewahi
kuwahamisha wapiganaji wake mjini
Mogadishu siku za nyuma, lakini safari hii
inaonesha kuondoka kwao ni ushindi
mkubwa kwa serikali.
Somalia, al Shabaab, kinasema kuwa
kimeondoka katika vituo vyake kadha ndani
ya mji mkuu, Mogadishu.
Wakaazi wameiambia BBC kwamba waliona
misafara ya wapiganaji ikiondoka katika mji
huo.
Kuhama huko kunafuatia mapigano makali
jana usiku.
Kikosi cha Umoja wa Mataifa kinachoisaidia
serikali ya Somalia kimekuwa kikipigana na
al Shabaab mjini Mogadishu katika siku za
karibuni; ili kuweza kufikisha msaada wa
chakula kwa wale walioathirika na ukame
nchini Somalia.
Haijulikani kama wapiganaji hao
wameondoka kabisa.
Msemaji wa serikali alielezea huo kuwa
"ushindi wa dhahabu" kwa watu wa
Somalia.
Lakini al Shabaab, ambayo inadhibiti
sehemu kubwa ya kusini mwa nchi, ilisema
wameondoka kufwatana na mikakati yao na
iliahidi kufanya shambulio la kulipiza.
Baadhi ya wadadisi wanafikiri al Shabaab
imepungukiwa na fedha kwa sababu
wafadhili wao wa Arabuni
wamewapunguzia msaada tangu al
Shabaab kudhoofika kijeshi.
Wadadisi wanasema al Shabaab imewahi
kuwahamisha wapiganaji wake mjini
Mogadishu siku za nyuma, lakini safari hii
inaonesha kuondoka kwao ni ushindi
mkubwa kwa serikali.