Al-Kaaba: Urithi wa Kipagani na Ibada ya Siri

Al-Kaaba: Urithi wa Kipagani na Ibada ya Siri

Naomba rejea ya kauli yako kutoka kwenye Biblia ili tulinganishe ulichosema na kilichoandikwa kama vinafanana.

Tatizo hata Biblia hauijui halafu unakuja kupambana na WAISLAM- Shame on you!
Watu wa kizazi hiki wanasoma Agano jipya wanafikiri ndio Biblia....
Kasome Mwanzo 21 utapata hizo habari
 
HUYU HAMISS77, NI KATI YA WAPOTOSHAJI WAKUBWA.....
Ni sawa na kuambia watu kuwa; CCM maana yake ni Chama Cha Mambuzi na sio CHAMA CHA MAPINDUZI au kusema FFU ni fanya fujo Uone na sio Field Force Unit nk nk
yaani anachukua habari sahihi; anaifanyia tafsiri anayotaka....AKIJUA WATU WOTE NI WAJINGA WA KUMUAMINI......Shame on him!!!

HUYU; KAMA AMESOMA BIBLIA/AGANO LA KALE, IWEJE HAJUI HABARI ZA ISHMAEL NA MAMA YAKE AMBAZO ZIME ELEZWA VIZURI, SAWA SAWA NA KWA WAISLAM? ANAKUJA HAPA KUTULETEA HADITHI FEKI ZA KITAPELI eti Ishmael alipeleka mjini Maka kukiwa na msikiti, Wakati Biblia inatuambia kabisa, kuwa waliachwa jangwani na hapakuwa na kitu chochote..... Shame on him!!!
UTAONA KABISA ANAKWEPA HIZI HABARI KWA SABABU NDIPO MSINGI WA UISLAM ULIPO (AL-KAABA nk nk)

NAAMINI HATA YESU HAWEZI KUKUBALI WAPOTOSHAJI KAMA HAWA, ETI NI WAFUASI WAKE?
AENDELEE TU NA HUU UPOTOSHAJI SIKU ZA MWISHO, YESU AMKATAE NDIO ATAJUA HAJUI!!!
Wewe Bado mdogo sana kwa hii mijadala ,kwanza hujui historia,hujui uislamu,hujui biblia

Hujui Geography location ya mashariki ya kati

Kwanza kabisa, tulia.

Hakuna anayekwepa habari za Ishmael na Hajar.

Sisi tunasoma maandiko yalivyo, si kuyaongeza wala kuyapunguza.
Biblia inasema wazi

“akapotea katika jangwa la Beer-sheba.”
(Mwanzo 21:14)


Hapo ndipo Hajar na Ishmael walienda. Si Mecca. Si Saudi Arabia. Ni Beer-sheba eneo la kusini mwa Kanaani.

Biblia pia inasema

Mungu akafungua macho yake, akaona kisima cha maji.”
(Mwanzo 21:19)


Biblia haisemi
Zamzam
Mecca
Kaaba
Msikiti
Hija
Jiwe jeusi


Sasa swali la msingi ni hili

Kama hadithi ni “sawa sawa” kwa Wakristo na Waislamu, kwa nini vitu hivi vyote havipo kabisa kwenye Agano la Kale?

Hapo ndipo tatizo linaanza.


Wewe unasema

“Biblia inasema waliwekwa jangwani na hapakuwa na kitu.”
Ndiyo, ni kweli. Lakini jangwani la wapi?

Biblia imeweka jina,Beer-sheba.
Kwa nini unakataa jina hilo halafu unataka kulibadilisha kuwa Mecca?


Ukisoma Mwanzo 16 na 21 kwa uangalifu utaona

Ishmael alizaliwa Kanaani
Alikulia Kanaani

Alifukuzwa akiwa kijana (si mtoto anayenyonya)

Akaenda jangwa la Beer-sheba
Akaishi “jangwa la Parani” (Mwanzo 21:21)

Parani ipo Sinai / Negev, si Mecca.


Sasa hoja yako inajikanganya. Unasema hakuna msikiti wala kitu chochote sawa kabisa.

Lakini hadithi ya Bukhari ndiyo inayotaja

“mahali pa juu kabisa kwenye msikiti karibu na Kaaba”

Swali

Msikiti gani wakati Uislamu haukuwepo?😂😂

Kaaba gani wakati hakuna ushahidi wa kihistoria wa karne ya Ibrahimu huko Mecca?😂😂


Hapa ndipo unaona wazi kuwa hizo ni simulizi za baadaye, si historia ya karne ya Ibrahimu.

Na kuhusu kusema

“Ndipo msingi wa Uislamu ulipo”

Hapo umesema ukweli bila kujua.

Ndiyo, msingi wa Uislamu umefungwa kwenye hadithi ya kuhusisha Kaaba na Ibrahimu.

Lakini tatizo ni hili
Hakuna maandiko ya Kiyahudi.
Hakuna maandiko ya Kikristo.
Hakuna ushahidi wa akiolojia.


Hakuna rekodi ya kale ya Kiarabu ya kabla ya Uislamu
inayosema Ibrahimu alifika Mecca.


Historia ya Ibrahimu imeandikwa na Wayahudi karne nyingi kabla ya Muhammad.

Kama kweli alifika Mecca, kwa nini hakuna hata mstari mmoja katika Torati?

Hapa si suala la kupiga kelele au kusema “Yesu atamkataa fulani.”

Yesu mwenyewe alisema:
“Utaijua kweli, nayo kweli itawaweka huru.” (Yohana 8:32)

Kweli haiogopi uchunguzi.


Na ukweli ni huu, Biblia inamuweka Ibrahimu Kanaani.

Uislamu unampeleka Mecca. Moja lazima iwe sahihi na maandiko ya kale ndiyo yana uzito wa kihistoria.


Sasa swali ni hili

Ni nani aliyekuja kwanza kihistoria?
Torati au Muhammad?
 
Tatizo hata Biblia hauijui halafu unakuja kupambana na WAISLAM- Shame on you!
Watu wa kizazi hiki wanasoma Agano jipya wanafikiri ndio Biblia....
Kasome Mwanzo 21 utapata hizo habari
😂😂😂😂😂Acha UPOTOSHAJI wewe
 
1770788917377.jpeg
1770788917377.jpeg

MKINIKERA MI,NABWATUKA...!!
 
Wewe Bado mdogo sana kwa hii mijadala ,kwanza hujui historia,hujui uislamu,hujui biblia

Hujui Geography location ya mashariki ya kati

Kwanza kabisa, tulia.

Hakuna anayekwepa habari za Ishmael na Hajar.

Sisi tunasoma maandiko yalivyo, si kuyaongeza wala kuyapunguza.
Biblia inasema wazi

“akapotea katika jangwa la Beer-sheba.”
(Mwanzo 21:14)


Hapo ndipo Hajar na Ishmael walienda. Si Mecca. Si Saudi Arabia. Ni Beer-sheba eneo la kusini mwa Kanaani.

Biblia pia inasema

Mungu akafungua macho yake, akaona kisima cha maji.”
(Mwanzo 21:19)


Biblia haisemi
Zamzam
Mecca
Kaaba
Msikiti
Hija
Jiwe jeusi


Sasa swali la msingi ni hili

Kama hadithi ni “sawa sawa” kwa Wakristo na Waislamu, kwa nini vitu hivi vyote havipo kabisa kwenye Agano la Kale?

Hapo ndipo tatizo linaanza.


Wewe unasema

“Biblia inasema waliwekwa jangwani na hapakuwa na kitu.”
Ndiyo, ni kweli. Lakini jangwani la wapi?

Biblia imeweka jina,Beer-sheba.
Kwa nini unakataa jina hilo halafu unataka kulibadilisha kuwa Mecca?


Ukisoma Mwanzo 16 na 21 kwa uangalifu utaona

Ishmael alizaliwa Kanaani
Alikulia Kanaani

Alifukuzwa akiwa kijana (si mtoto anayenyonya)

Akaenda jangwa la Beer-sheba
Akaishi “jangwa la Parani” (Mwanzo 21:21)

Parani ipo Sinai / Negev, si Mecca.


Sasa hoja yako inajikanganya. Unasema hakuna msikiti wala kitu chochote sawa kabisa.

Lakini hadithi ya Bukhari ndiyo inayotaja

“mahali pa juu kabisa kwenye msikiti karibu na Kaaba”

Swali

Msikiti gani wakati Uislamu haukuwepo?😂😂

Kaaba gani wakati hakuna ushahidi wa kihistoria wa karne ya Ibrahimu huko Mecca?😂😂


Hapa ndipo unaona wazi kuwa hizo ni simulizi za baadaye, si historia ya karne ya Ibrahimu.

Na kuhusu kusema

“Ndipo msingi wa Uislamu ulipo”

Hapo umesema ukweli bila kujua.

Ndiyo, msingi wa Uislamu umefungwa kwenye hadithi ya kuhusisha Kaaba na Ibrahimu.

Lakini tatizo ni hili
Hakuna maandiko ya Kiyahudi.
Hakuna maandiko ya Kikristo.
Hakuna ushahidi wa akiolojia.


Hakuna rekodi ya kale ya Kiarabu ya kabla ya Uislamu
inayosema Ibrahimu alifika Mecca.


Historia ya Ibrahimu imeandikwa na Wayahudi karne nyingi kabla ya Muhammad.

Kama kweli alifika Mecca, kwa nini hakuna hata mstari mmoja katika Torati?

Hapa si suala la kupiga kelele au kusema “Yesu atamkataa fulani.”

Yesu mwenyewe alisema:
“Utaijua kweli, nayo kweli itawaweka huru.” (Yohana 8:32)

Kweli haiogopi uchunguzi.


Na ukweli ni huu, Biblia inamuweka Ibrahimu Kanaani.

Uislamu unampeleka Mecca. Moja lazima iwe sahihi na maandiko ya kale ndiyo yana uzito wa kihistoria.


Sasa swali ni hili

Ni nani aliyekuja kwanza kihistoria?
Torati au Muhammad?

Umeandika “Torati ilikuja kwanza kuliko Muhammad” – HILI HALIPINGWI​


Hakuna Mwislamu anayepinga hilo.
Ndiyo: Torati iliandikwa karne nyingi kabla ya Qur’an. Biblia ndiyo chanzo cha kale zaidi tulichonacho kuhusu Ibrahim katika mapokeo ya Kiyahudi.

Lakini hoja ya kihistoria si nani aliandika kwanza, bali: Je, maandiko ya kwanza yanasema kila kitu alichokifanya Ibrahim, au yanasema sehemu tu?

Kutokutajwa si sawa na kutokuwepo.




Beer-sheba si mwisho wa safari ya Ishmael​


Biblia inasema:
“Akapotea katika jangwa la Beer-sheba.”
(Mwanzo 21:14) Ndiyo. Lakini soma aya zinazofuata kwa uaminifu wa kitaaluma.

Mwanzo 21:21 “Akaishi katika jangwa la Parani.”

Swali la kihistoria:

Beer-sheba si Parani
Beer-sheba ni mahali
Parani ni eneo pana la jangwani

Wanahistoria wa Biblia (hata Wakristo na Wayahudi) wanakubali:


  • Parani ni eneo kubwa, si mji mmoja
  • Halikuwekewa mipaka kamili katika Torati
Qur’an haisemi Ishmael alibaki Beer-sheba milele.

Parani iko wapi kihistoria?​


Hoja kwamba Parani ni Sinai/Negev si msimamo wa mwisho wa kielimu, bali ni nadharia moja.

Ushahidi: Kumbukumbu la Torati halitoi ramani

Zaburi 84:5–6 inazungumzia “bonde la Baka” (linganisha na Bakkah – Qur’an 3:96)

Wanazuoni wa kale wa Kiyahudi walijua Parani ni kusini mashariki ya Kanaani, kuelekea Uarabuni

Kwa historia ya kale, jangwa la Arabia halikuwa “nje ya dunia” kama watu wanavyodhani leo.

“Kwa nini Kaaba, Zamzam havipo kwenye Torati?”​


Hili ni kosa la kimantiki (argument from silence).

Torati: Haitaji Roma wala Haitaji China wala Haitaji Marekani , Lakini maeneo hayo yalikuwepo.

Pia: Torati haitaji mahali Ishmael alikufa , Haitaji alipozikwa, wala Haitaji watoto wake wote

Torati haikuwa historia ya dunia, bali historia ya Israeli.

Ishmael alikatwa nje ya simulizi kuu, si kwa sababu hakuhusika, bali kwa sababu hakuwa sehemu ya agano la Israeli.

“Msikiti gani kabla ya Uislamu?”​

Huku ni kutoelewa lugha ya hadith.

Neno “masjid”: Kiarabu: mahali pa kusujudu na Si lazima jengo la Kiislamu

Qur’an inasema: “Msikiti wa kwanza uliowekwa kwa watu ni ule wa Bakkah.” (Qur’an 3:96)

Haimaanishi: kulikuwa na minara kulikuwa na Uislamu wa Nabii Muhammad SAW

Inamaanisha mahali pa ibada ya Mungu Mmoja, kama madhabahu za kale.


Biblia pia inazungumzia: Madhabahu kabla ya Musa na pia Ibada kabla ya Torati


“Hakuna ushahidi wa akiolojia wa Ibrahim Mecca”​


Hili ni nusu-ukweli.

Ukweli kamili:

Hakuna ushahidi wa akiolojia wa Ibrahim popote, hata Kanaani , Wala Hakuna jiwe linalosema “Abraham was here” Israel pia Ibrahim ni mtu wa zama za kabla ya uandishi mkubwa Karibu 2000 BCE

Arabia haikuwa na maandishi yaliyohifadhiwa kama Mesopotamia

Kukosa ushahidi si sawa na ushahidi wa kukosa.

Historia ya Ibrahim haikuwa miliki ya Wayahudi pekee​


Kabla ya Torati: Kulikuwa na mapokeo ya mdomo, Makabila mengi yaliihifadhi historia kwa njia zao

Uislamu unasema: Qur’an inarudisha mapokeo ya kale ya Kiarabu na Sio kunakili Torati, bali kurekebisha simulizi lililopungua upande mmoja

“Moja lazima iwe sahihi”​

Hili ni wazo la kisasa, si la kihistoria. Inawezekana: Ibrahim aliishi Kanaani (ndiyo) , Ishmael alihamia kusini (ndiyo)
Mapokeo mawili yakahifadhi sehemu tofauti za historia moja . Kijana uelewe Historia ya kale haifanyi kazi kama mahakama ya leo.

Hoja ya mwisho – “Kweli haiogopi uchunguzi”​

Hili ni kweli kabisa. Na kwa uchunguzi: Biblia haikanushi wazi safari ya Ishmael kwenda mbali zaidi , Qur’an haikanushi Ibrahim kuishi Kanaani , Kinachotofautiana ni nukta ya simulizi, si uwepo wa mtu.
 
CCM maana yake ni CHAMA CHA MAJAMBAZI siyo Mambuzi. NIKUREKEBISHE HAPO.

Huyu hamis anatuweka wazi sana mambo anayoandika hayakupaswa kujulishwa kwa watu. Anauweka wazi uislamu kiasi inakuwa ngumu sasa kuwashawishi watu kujiunga na uislam. Haya mambo anayaandika nshamwambia mimi si matangazo. Maana waislamu wengi maamuma huwa hatuangalii hayo. Yeye anayaleta. Wallah ataenda motoni kwa kuandika haya. Na namwambia siku nikionana naye... Tutagawana majengo ya serikali
Acha ulimbukeni wa kujifanya wewe ni Muislam;
Kadanganye wajinga wenzako!
Shame on you!!!
 
Acha ulimbukeni wa kujifanya wewe ni Muislam;
Kadanganye wajinga wenzako!
Shame on you!!!
 
Ibrahimu alifika Meka alikuta hakuna watu
akaukuta
Msikiti
Al-Kaaba
Kisima cha maji ya Zamzam

halafu hapohapo wanasema hiyo Al-Kaaba alijenga Ibrahimu:
Sasa alijengaje hiyo
Al-Kaaba wakati aliikuta:

Labda yule Ibrahimu mtoto wa Al-Ezar anayetajwa na Qurani
Na sio Ibrahimu mtoto Tera anayetajwa kwenye Biblia

Ibrahimu huyu wa Qurani ndiye aliyejenga hiyo
Al-Kaaba huko mecca

6:74 - Na pale Ibrahim alipo mwambia baba yake, Azar: Unayafanya masanamu kuwa ni miungu? Hakika mimi nakuona wewe na watu wako mmo katika opotofu ulio wazi.

Ibrahimu wa Biblia baba yake ni Tera na hakuwahi kumwambia baba yake kuwa anayayafanya masanamu kuwa miungu:
kama Aya ya hapo Juu inavyodai:

Huyo ni Ibrahimu wa Muhamadi:
Kama alivyo Isa wa Muhamadi
 
Ibrahimu alifika Meka alikuta hakuna watu
akaukuta
Msikiti
Al-Kaaba
Kisima cha maji ya Zamzam

halafu hapohapo wanasema hiyo Al-Kaaba alijenga Ibrahimu:
Sasa alijengaje hiyo
Al-Kaaba wakati aliikuta:

Labda yule Ibrahimu mtoto wa Al-Ezar anayetajwa na Qurani
Na sio Ibrahimu mtoto Tera anayetajwa kwenye Biblia

Ibrahimu huyu wa Qurani ndiye aliyejenga hiyo
Al-Kaaba huko mecca

6:74 - Na pale Ibrahim alipo mwambia baba yake, Azar: Unayafanya masanamu kuwa ni miungu? Hakika mimi nakuona wewe na watu wako mmo katika opotofu ulio wazi.

Ibrahimu wa Biblia baba yake ni Tera na hakuwahi kumwambia baba yake kuwa anayayafanya masanamu kuwa miungu:
kama Aya ya hapo Juu inavyodai:

Huyo ni Ibrahimu wa Muhamadi:
Kama alivyo Isa wa Muhamadi

Biblia yako yenyewe inathibitisha kuwa baba wa Ibrahimu alikuwa anaabudu sanamu.

Book of Joshua 24:2

“Tera baba yake Ibrahimu… waliabudu miungu mingine.”

Hivyo si ajabu Qurani kusema Ibrahimu alimkemea baba yake.


Pia Qurani haisemi Ibrahimu aliikuta Kaaba imejengwa tayari, bali yeye na mwanawe waliinua misingi yake:

Quran 2:127“Ibrahim na Ismail walipoinyanyua misingi ya Nyumba.”

hoja yako imejengwa juu ya kuchanganya mambo.
 
Back
Top Bottom