Akina mama/dada muogopeni muumba jamani

Elli

Platinum Member
Mar 17, 2008
55,499
86,035
Sina tabia wala mazoea ya kuanzisha thread za mahusiano lakini kwa hili hapana; Mimi kama Mwanamme ambaye nitabaki kuwa mkweli kwa kuwa kweli hukuweka HURU, nasema hivi; tangu kubalehe hadi sasa ni kweli tupu kuwa nimeshakuwa na mahusiano na baadhi ya wanawake ( number doesnt matter).
Wapo ambao tulipendana kwa dhati ila kwa sababu ya mambo mbalimbali ilibidi relation zetu zi-break. Wapo ambao waliniacha bila sababu za msingi ( kwa upande wangu), wapo ambao kwa sababu kipindi kile tulikuwa labda "watoto" ( maana watoto hawafanyi) basi hao nao tuli-break ila kuna hawa ambao tuliachana kwa amani sana. Tulipatana kuwa sasa imetosha, nao pia nawashukuru sana ( usikimbilie kujumlisha idadi p utapotosha somo).

Nachukua nafasi hii kwa uchungu sana kwa wale akina dada wenye tabia za kuwaacha wanaume bila sababu na when things turns out worse wanaanza kukusumbua. Wamekua wakinisumbua sana ila sasa huyu wa juzi aliniiacha miaka kama kumi iliopita kwasababu nilimwambia asubiri nimalize kale ka-degree kangu, akaona anachelewa sasa eti ananisumbua na sms na simu kila saa kuwa bado anani-feel sana!!

Jana nikamtumia sms kuwa, yeye ameolewa, ana mume na watoto wawili, namheshimu mumewe na pia naiheshimu ndoa yao lakini pia nisingependa nijiingize kwenye mahusiano ambayo si sahihi ukizingatia na mimi sasa niko na my wife.....analalamika na kuniomba nikutane naye japo mara moja. Nimeamua ku-generalize kuwa labda ni akina dada wote ( including my wife maybe) kwa sababu huyu si wa kwanza wala awa pili na hata pia the same stories nimeshazisikia kwa marafiki zangu.

Hivyo nasema kwamba, kwa akina kaka na akina dada hasa akina dada, hebu tuache hizi tabia chafu tutunze ndoa na watoto wetu, ngono hazina mwisho, mimi ni sawa na huyo ulienae tuuuu, tuacheni tamaa tumrudie MUUMBA. Sorry kama nitawakera baadhi yenu.
 
Umenikera kwa kujumuisha wadada/wanawake wote!!

Nwy cha kufanya we ondoa mawasiliano naye tu basi.Tulia kwao nae kama hawezi kufanya hivyo atafute anaefanana nae wavunje viapo vyao pamoja!
 
Ni sahihi kabisa ulichosema,wapo wanawake wa aina hiyo, nafikiri ungesema kwa wenye tabia hiyo au mawazo ya aina hiyo wamuogope muumba.....na zaidi, hili ni suala la pande zote,hakuna viumbe dhaifu na waharibu ndoa na mahusiano kama wanaume....so, Michelle nasema wanaume wasio heshimu ndoa na commitment zao hata kabla ya ndoa na wanaoumiza na kutesa nafsi za watu na pengine kuziangamiza kabisa,MUOGOPENI MUNGU......last but not least......dhambi si uzinzi tu....TUMUOGOPE MUNGU SOTE,KUNA MAISHA BAADA YA HII DUNIA!!
 
Umenikera kwa kujumuisha wadada/wanawake wote!!

Nwy cha kufanya we ondoa mawasiliano naye tu basi.Tulia kwao nae kama hawezi kufanya hivyo atafute anaefanana nae wavunje viapo vyao pamoja!

Nami nimeliona hilo, si suala la wanawake wote,kwa wenye hizo tabia waache.....!!! Halafu ishu nyingine si ngumu hivyo kuzi- handle dearest,sijui kwanini watu wana complicate issues? mtu humtaki,unajibu sms zake au kupokea simu zake za nini????:confused2:
 
i think ingekuwa beta if u would say 'SOME OF GIRLS'...leaving behind dat,tc true dat there are ppo kama hao,thoz ppo dnt knw da real meaning of ndoa datc y they go on blving dat they can go back to their x-guys...
 
Samahanini ile ukisoma vizuri kuna sehemu nimetumia neno" kwa wale akina dada" nadhani ni sawa na neno "baadhi" pia katika hitimisho langu nimetaja tena kwa kuanza na akina "kaka na akina dada". Haya asanteni na mnisamehe kama mmenielewa ndivyo sivyo ila jamani huo ndio ukweli, usikimbilie kuoa/kuolewa kama hujamaliza baadhi ya mambo yako. Asanteni kwa kujaribu kunielewa.
 
ukiona vyaelea vimeumbwa labda ulikuwa huwezi kuumba by that time so ............
 
Nimeshawataka radhi, back to the point then; naombeni muwe haya tuseme tuwe (both males and females wenye tabia hizo) watulivu. Hope it is clear now. Muungwana haogopi kusema Samahani.
 
Yaani hiyo story kama ulivyoitoa, nami I encountered the same shit sometimes 2 years back. Kuna time ilibidi nimwambie yule dada namwambia mumewe ndio akatulia! And seriously nilikua tayari kumtafuta na kumwambia mumewe, maana najua anapofanya kazi. Viumbe wanawake acha waitwe wanawake.........
 
Nami nimeliona hilo, si suala la wanawake wote,kwa wenye hizo tabia waache.....!!! Halafu ishu nyingine si ngumu hivyo kuzi- handle dearest,sijui kwanini watu wana complicate issues? mtu humtaki,unajibu sms zake au kupokea simu zake za nini????:confused2:

Kweli dearest...utashangaa watu wanavyolalamika ohhh haishi kupiga ..mara text nazo haziishi kuingia.Hii yote ni kwasababu wao wenyewe wanaendekeza kinachoendelea...kwanza ukimwambia mtu aache usumbufu wake na hauko interested na anachotaka huku ukimaanisha utaona kama atakusumbua tena.Sasa kama wewe unamchekea chekea na kujibu usianze kulalamika pembeni kwamba anakusumbia....mfikishie mhusika ujumbe ili aache!
 
ukiona vyaelea vimeumbwa labda ulikuwa huwezi kuumba by that time so ............
Ni kweli kabisa nakubaliana na wewe, so why coming back to me then??? Ugomvi wangu ni mtu anaporudia matapishi yake.....kuweni nakajimsimamo kidogo, haya
 
Samahanini ile ukisoma vizuri kuna sehemu nimetumia neno" kwa wale akina dada" nadhani ni sawa na neno "baadhi" pia katika hitimisho langu nimetaja tena kwa kuanza na akina "kaka na akina dada". Haya asanteni na mnisamehe kama mmenielewa ndivyo sivyo ila jamani huo ndio ukweli, usikimbilie kuoa/kuolewa kama hujamaliza baadhi ya mambo yako. Asanteni kwa kujaribu kunielewa.

Huo ndo ukweli hakuna asiyejua kuwa kuna baadhi ya wasichana wenye tabia hizo......na sisi hatujajaribu kukuelewa.....TUMEKUELEWA,hakuna kitu kigumu ulichoongea kisichoeleweka....!!!
 
Kweli dearest...utashangaa watu wanavyolalamika ohhh haishi kupiga ..mara text nazo haziishi kuingia.Hii yote ni kwasababu wao wenyewe wanaendekeza kinachoendelea...kwanza ukimwambia mtu aache usumbufu wake na hauko interested na anachotaka huku ukimaanisha utaona kama atakusumbua tena.Sasa kama wewe unamchekea chekea na kujibu usianze kulalamika pembeni kwamba anakusumbia....mfikishie mhusika ujumbe ili aache!
Ni kweli kabisa ila mimi sina lugha ya matusi kumjibu mtu, huwa mara nyingi natumia hekima zaidi, na wala sijalalamika Dada, nimewaomba tu mjaribu kutulia, hilo tu ndio ombi langu, sina nyongeza dada.
 
Huo ndo ukweli hakuna asiyejua kuwa kuna baadhi ya wasichana wenye tabia hizo......na sisi hatujajaribu kukuelewa.....TUMEKUELEWA,hakuna kitu kigumu ulichoongea kisichoeleweka....!!!
Asante sana, nilitaka nikugongee thanks ila kitufe sijui kimeyeyukia wapi hukooo, so somo limeleweka teach others too.
 
Yaani hiyo story kama ulivyoitoa, nami I encountered the same shit sometimes 2 years back. Kuna time ilibidi nimwambie yule dada namwambia mumewe ndio akatulia! And seriously nilikua tayari kumtafuta na kumwambia mumewe, maana najua anapofanya kazi. Viumbe wanawake acha waitwe wanawake.........
Hahahaaaa, imebidi nikumbuke wimbo wa Prof J..... they are more of material motivated than loving!!
 
Kweli dearest...utashangaa watu wanavyolalamika ohhh haishi kupiga ..mara text nazo haziishi kuingia.Hii yote ni kwasababu wao wenyewe wanaendekeza kinachoendelea...kwanza ukimwambia mtu aache usumbufu wake na hauko interested na anachotaka huku ukimaanisha utaona kama atakusumbua tena.Sasa kama wewe unamchekea chekea na kujibu usianze kulalamika pembeni kwamba anakusumbia....mfikishie mhusika ujumbe ili aache!

Halafu dearest,huyu mwanamke kwa tabia hizi kuna uwezekano amekuwa na wanaume tofauti tofauti,kwanini specifically amsumbue Elli?
Nayeye kama mwanaume YAWEZEKANA ana udhaifu fulani au ni mwepesi sana, so kaona of all the men,this is the easiest dude to pursue....l.o.l
Manake wanaume wanaonaga wanawake cheap,ila ukweli ni kuwa hata sisi kuna wanaume tunawaona cheap,na wepesi kuwapata kwa shida ndogo ndogo!!! No offense,just thinking loud!!
 
Ni kweli kabisa ila mimi sina lugha ya matusi kumjibu mtu, huwa mara nyingi natumia hekima zaidi, na wala sijalalamika Dada, nimewaomba tu mjaribu kutulia, hilo tu ndio ombi langu, sina nyongeza dada.

Wapi nimesema umtukane!??Kama kumweleza mtu hufurahii tabia yake kwa kumaanisha ni sawa na kutukana basi bila shaka ntaungua motoni.
 
Ni kweli kabisa nakubaliana na wewe, so why coming back to me then??? Ugomvi wangu ni mtu anaporudia matapishi yake.....kuweni nakajimsimamo kidogo, haya

kazi kweli kweli......nilijua ugomvi ni kwa huyu dada mwenye ndoa na watoto kutoka nje ya ndoa...kumbe ugomvi ni kukurudia wewe aliyekutapika zamani? sasa,em tuweke hivi,ungekuwa ulimtapika wewe,akolewa,lakini akataka ku-spend muda na wewe,ungempokea kwa mikono miwili sio? kuweni na msimamo pia wanaume,you are the weakest creatures......!!!
 
Halafu dearest,huyu mwanamke kwa tabia hizi kuna uwezekano amekuwa na wanaume tofauti tofauti,kwanini specifically amsumbue Elli?
Nayeye kama mwanaume YAWEZEKANA ana udhaifu fulani au ni mwepesi sana, so kaona of all the men,this is the easiest dude to pursue....l.o.l
Manake wanaume wanaonaga wanawake cheap,ila ukweli ni kuwa hata sisi kuna wanaume tunawaona cheap,na wepesi kuwapata kwa shida ndogo ndogo!!! No offense,just thinking loud!!

Hahahhhaaha dearest umeniacha hoi!Ila ukweli ni ukweli tu hata kama unafurahisha...we unadhani kuna mwanamke anajipendekeza kwa mwanaume kichwa kichwa kweli?!Wanawake hua wanajua kabisa fulani nikimsumbua mara mbili tatu tu ataingia line....wakati wanaune hua wanatumaini wataweza!!

Elli kwa mara nyingine nakwambia kama kweli huna mpango na huyo dada mweleze na umaanishe.Kama bado anaendelea kukupigia na kukutext basi una udhaifu hata kama hutaki kukubali.... it‘s just a matter of time before you fall into her hands.
 
Halafu dearest,huyu mwanamke kwa tabia hizi kuna uwezekano amekuwa na wanaume tofauti tofauti,kwanini specifically amsumbue Elli?
Nayeye kama mwanaume YAWEZEKANA ana udhaifu fulani au ni mwepesi sana, so kaona of all the men,this is the easiest dude to pursue....l.o.l
Manake wanaume wanaonaga wanawake cheap,ila ukweli ni kuwa hata sisi kuna wanaume tunawaona cheap,na wepesi kuwapata kwa shida ndogo ndogo!!! No offense,just thinking loud!!

Hahhaaaa, dada zangu nyie mnanifanya nifurahi hapa ofisini peke yangu, Mimi sio Pleaser kiasi hicho, hahaaaa, mie bana hua najitahidi kupunguza maadui zaidi na kuongeza marafiki zaidi.....nawaheshimu wanawake sana sijawahi kuwaona cheap or harlots, ninawachukulia kama mama yangu that;s why simuiiti mwanamke yoyote "Demu" naweza muita Dada au Mama...they are so special creatures to me si katika maswala ya ngono. Thanks
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom