Akina baba msiwachokoze watoto wenu

Akina baba msiwachokoze watoto wenu

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
19,395
Reaction score
40,222
Waefeso 6:4
"Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana".

Kabla ya yote niweke wazi kwamba ninaamini biblia ni kitabu kitakatifu chenye mafundisho yote muhimu kwa binadamu. Pia ni kitabu chenye kuburudisha na kusisimu sana. Kimsingi biblia ni kitabu chenye kila kitu na kamwe hutajutia kukisoma kila siku. Kwa wale wasio na imani kama yangu pia wako sahihi maana nao wana wanachoamini.

Tukirudi kwenye nia nzima ya uzi ni kwamba biblia kupitia Waefeso ina maonyo kwa kina baba dhidi ya watoto wao. Ukisoma imeandikwa straight kwamba kina baba tusiwachokoze watoto bali tuwalee katika maadili mema. Kwanini imeandikwa hivi? Jibu ni kwamba hata Mungu mwenyewe alishaona upuuzi wa wakina baba wengi kuendekeza ubabe usio na tija kwa watoto wao kiasi kwamba wakati mwingine inakuwa kama uchokozi. Hivyo kupitia neno lake akatoa mwongozo.

Nikiangalia makuzi ya wengi wetu nazidi kuamini hayo maneno ya Waefeso 6:4. Wengi wetu tumekuzwa katika namna ambayo baba huwa ni kama adui yaani HAZOELEKI. Madhara yake ni kwamba huku ukubwani automatically baba anakuwa kama ametengwa. Watoto wengi wakishakuwa watu wazima huelekeza mapenzi kwa mama huku baba akipambana kivyake. Hali huwa mbaya kwa familia za vipato vya chini kwasababu watoto humjali zaidi mama kwa kumtumia pesa mara kwa mara. Baba hufanywa kama ziada tu. Kimsingi uzee wa wa kina baba wengi huwa na changamoto sana.

Ninawasihi sana kina baba wenzangu tusibaki kwenye yale maandiko ya kumbana mtoto aheshimu huku tukikazia na ule mstari usemao USIMNYIME MTOTO MAPIGO. Tukumbuke pia hatutakiwi KUWACHOKOZA WATOTO. Mtoto kukuogopa sana utajutia sana uzeeni. Utaanza kuwalaumu watoto kumjali mama yao zaidi wakati wewe ndo ulijichagulia mwenyewe mwisho wako.

Nawapongeza sana single mothers kwenye malezi ya watoto wao hasa wa kiume. Hawa single mama huwa wanacheza vizuri nafasi zao kwenye kuwakuza watoto wa kiume. Wengi wa watoto wa single mama huja kuwa masupastaa wakubwa na mzazi kuishia kula bata.
 
Nyinyi ndio aina ya Wazazi wenye kizazi cha namna hii.

Screenshot_20220901-132339_1.jpg
Screenshot_20220901-132349_1.jpg
Screenshot_20220901-132519_1.jpg
Screenshot_20220901-132539_1.jpg
 
Nyinyi ndio aina ya Wazazi wenye kizazi cha namna hii.
We mzee unataka tu kuleta ligi isiyo na maana yoyote. Kama ni ushoga kuna watu wako straight kabisa na wanapiga chuma gym ila mashoga. Kuna mambo mengine inafika point mzazi hawezi ku-control ni Mungu tu aamue.
 
Sisi katika tuliyofundishwa ni haya hapa:

17_23.gif

23. Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa hishima.


17_24.gif

24. Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wangu Mlezi! Warehemu kama walivyo nilea utotoni.


17_25.gif

25. Mola wenu anajua kabisa yaliyo nyoyoni mwenu. Ikiwa nyinyi mtakuwa wema, basi hakika Yeye ni Mwenye kuwaghufiria wanao tubia kwake.


(Qur'an 17:23-25)
 
Nawapongeza sana single mothers kwenye malezi ya watoto wao hasa wa kiume. Hawa single mama huwa wanacheza vizuri nafasi zao kwenye kuwakuza watoto wa kiume. Wengi wa watoto wa single mama huja kuwa masupastaa wakubwa na mzazi kuishia kula bata.
Yaan huo mstari uliouweka na ulivyomalizia vinapingana kabisa yaan in short umepuyanga

Mada inahusu akina baba ila hitimisho unaweka akina mama ambao kwa kiburi chao wenyewe wamebaki kua single mothers

Efeso 6 inazungumzia watoto na wazazi wao sio watoto na mzazi wao, Efeso 6 inaelezea kuhusu malezi ya kifamilia ya baba na mama na sio malezi ya pande moja, Efeso 6 inasimamia amri ya 4 ya Mungu waheshimu baba na mama, upate miaka mingi na kheri duniani

Efeso 6 haizungumzii single mother's na hakuna mstari kwenye biblia unazungumzia single mothers km upo uweke hapa na mimi niupitie

Efeso 6 inaelezea misingi ya familia na nguzo za familia jinsi gani wazazi wote wawili na sio mmoja wanatakiwa kuishi na watoto wao na kuwalea katika malezi yanayompendeza Mungu,

Efeso 6 inawahimiza watoto na wazazi kutimiza hitaji la Mungu, kwa kuwahimiza wababa wasikasirishe watoto wao na watoto wawatii na kuwaheshimu wazazi wao

Efeso 6 inawahimiza wazazi wawakuze watoto wao katika hekima na kimo, wakue kwa kuenenda na kutenda mambo mazuri yanayompendeza Mungu kwa kuwatii na kuwaheshimu wazazi wao wote wawili yaan baba na mama

Biblia katika Efeso 6 inazungumzia malezi ya pande mbili yaan baba na mama na sio pande moja yaan single mother au single father

Napita...
 
Yaan huo mstari uliouweka na ulivyomalizia vinapingana kabisa yaan in short umepuyanga

Mada inahusu akina baba ila hitimisho unaweka akina mama ambao kwa kiburi chao wenyewe wamebaki kua single mothers

Efeso 6 inazungumzia watoto na wazazi wao sio watoto na mzazi wao, Efeso 6 inaelezea kuhusu malezi ya kifamilia ya baba na mama na sio malezi ya pande moja, Efeso 6 inasimamia amri ya 4 ya Mungu waheshimu baba na mama, upate miaka mingi na kheri duniani

Efeso 6 haizungumzii single mother's na hakuna mstari kwenye biblia unazungumzia single mothers km upo uweke hapa na mimi niupitie

Efeso 6 inaelezea misingi ya familia na nguzo za familia jinsi gani wazazi wote wawili na sio mmoja wanatakiwa kuishi na watoto wao na kuwalea katika malezi yanayompendeza Mungu,

Efeso 6 inawahimiza watoto na wazazi kutimiza hitaji la Mungu, kwa kuwahimiza wababa wasikasirishe watoto wao na watoto wawatii na kuwaheshimu wazazi wao

Efeso 6 inawahimiza wazazi wawakuze watoto wao katika hekima na kimo, wakue kwa kuenenda na kutenda mambo mazuri yanayompendeza Mungu kwa kuwatii na kuwaheshimu wazazi wao wote wawili yaan baba na mama

Biblia katika Efeso 6 inazungumzia malezi ya pande mbili yaan baba na mama na sio pande moja yaan single mother au single father

Napita...
Ume-comment ushuzi mtupu pia hujaelewa kabisa nilichoandika.
 
Umeandika ujinga kujifariji kutokana na kuzalishwa zalishwa na kuachwa unaona ni fahari...mbwa wewe...🤣
Wewe chizi elewa kwamba humu hatujuani na ID zetu ni feki... utajisikiaje kujua mimi unaniyenitukana ndo nilikutoa marinda?
 
Binafsi nawapongeza sana
Single Mothers.

Wanafanya kazi ya Mungu kulea watoto wa Mungu waliotelekezwa.

Tatizo lao sasa.
Ukimpokea Single Mother kutaka kuhusiana naye na kuendelea kumlea mtoto wake.

Kila siku habari ni kumlaumu mtalaka wake.
Kwa sasa niongelee mimi tuendeleze maisha mtoto akikua mpeleke kwa baba yake au tumpe elimu ya kumfaa.

Ushauri kwa Single Mothers.
Ukimpata mwenza mpya anza kuishi maisha mapya ya kusikilizana wewe na mwenzako.

Kumbuka hapo Mungu amakuongezea nguvu ya kumlea mtoto na kukurudisha kwenye mahusiano ya Ki- Mungu.

Achana kabisa na habari, mawasiliano, kumbukumbu, na masimulizi ya uhusiano wako ulio pita.

Wanaume hatutaki kabisa kusikia habari za mme mwenza hata za sifa njema au sifa mbaya.
Zitakusabishia kuachwa tena.

Nawasilisha.
 
Waefeso 6:4
"Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana".

Kabla ya yote niweke wazi kwamba ninaamini biblia ni kitabu kitakatifu chenye mafundisho yote muhimu kwa binadamu. Pia ni kitabu chenye kuburudisha na kusisimu sana. Kimsingi biblia ni kitabu chenye kila kitu na kamwe hutajutia kukisoma kila siku. Kwa wale wasio na imani kama yangu pia wako sahihi maana nao wana wanachoamini.

Tukirudi kwenye nia nzima ya uzi ni kwamba biblia kupitia Waefeso ina maonyo kwa kina baba dhidi ya watoto wao. Ukisoma imeandikwa straight kwamba kina baba tusiwachokoze watoto bali tuwalee katika maadili mema. Kwanini imeandikwa hivi? Jibu ni kwamba hata Mungu mwenyewe alishaona upuuzi wa wakina baba wengi kuendekeza ubabe usio na tija kwa watoto wao kiasi kwamba wakati mwingine inakuwa kama uchokozi. Hivyo kupitia neno lake akatoa mwongozo.

Nikiangalia makuzi ya wengi wetu nazidi kuamini hayo maneno ya Waefeso 6:4. Wengi wetu tumekuzwa katika namna ambayo baba huwa ni kama adui yaani HAZOELEKI. Madhara yake ni kwamba huku ukubwani automatically baba anakuwa kama ametengwa. Watoto wengi wakishakuwa watu wazima huelekeza mapenzi kwa mama huku baba akipambana kivyake. Hali huwa mbaya kwa familia za vipato vya chini kwasababu watoto humjali zaidi mama kwa kumtumia pesa mara kwa mara. Baba hufanywa kama ziada tu. Kimsingi uzee wa wa kina baba wengi huwa na changamoto sana.

Ninawasihi sana kina baba wenzangu tusibaki kwenye yale maandiko ya kumbana mtoto aheshimu huku tukikazia na ule mstari usemao USIMNYIME MTOTO MAPIGO. Tukumbuke pia hatutakiwi KUWACHOKOZA WATOTO. Mtoto kukuogopa sana utajutia sana uzeeni. Utaanza kuwalaumu watoto kumjali mama yao zaidi wakati wewe ndo ulijichagulia mwenyewe mwisho wako.

Nawapongeza sana single mothers kwenye malezi ya watoto wao hasa wa kiume. Hawa single mama huwa wanacheza vizuri nafasi zao kwenye kuwakuza watoto wa kiume. Wengi wa watoto wa single mama huja kuwa masupastaa wakubwa na mzazi kuishia kula bata.
Eti watoto wa single maza huishia kuwa masupastaa huo utafiti sample ni diamond sio
 
Waefeso 6:4
"Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana".

Kabla ya yote niweke wazi kwamba ninaamini biblia ni kitabu kitakatifu chenye mafundisho yote muhimu kwa binadamu. Pia ni kitabu chenye kuburudisha na kusisimu sana. Kimsingi biblia ni kitabu chenye kila kitu na kamwe hutajutia kukisoma kila siku. Kwa wale wasio na imani kama yangu pia wako sahihi maana nao wana wanachoamini.

Tukirudi kwenye nia nzima ya uzi ni kwamba biblia kupitia Waefeso ina maonyo kwa kina baba dhidi ya watoto wao. Ukisoma imeandikwa straight kwamba kina baba tusiwachokoze watoto bali tuwalee katika maadili mema. Kwanini imeandikwa hivi? Jibu ni kwamba hata Mungu mwenyewe alishaona upuuzi wa wakina baba wengi kuendekeza ubabe usio na tija kwa watoto wao kiasi kwamba wakati mwingine inakuwa kama uchokozi. Hivyo kupitia neno lake akatoa mwongozo.

Nikiangalia makuzi ya wengi wetu nazidi kuamini hayo maneno ya Waefeso 6:4. Wengi wetu tumekuzwa katika namna ambayo baba huwa ni kama adui yaani HAZOELEKI. Madhara yake ni kwamba huku ukubwani automatically baba anakuwa kama ametengwa. Watoto wengi wakishakuwa watu wazima huelekeza mapenzi kwa mama huku baba akipambana kivyake. Hali huwa mbaya kwa familia za vipato vya chini kwasababu watoto humjali zaidi mama kwa kumtumia pesa mara kwa mara. Baba hufanywa kama ziada tu. Kimsingi uzee wa wa kina baba wengi huwa na changamoto sana.

Ninawasihi sana kina baba wenzangu tusibaki kwenye yale maandiko ya kumbana mtoto aheshimu huku tukikazia na ule mstari usemao USIMNYIME MTOTO MAPIGO. Tukumbuke pia hatutakiwi KUWACHOKOZA WATOTO. Mtoto kukuogopa sana utajutia sana uzeeni. Utaanza kuwalaumu watoto kumjali mama yao zaidi wakati wewe ndo ulijichagulia mwenyewe mwisho wako.

Nawapongeza sana single mothers kwenye malezi ya watoto wao hasa wa kiume. Hawa single mama huwa wanacheza vizuri nafasi zao kwenye kuwakuza watoto wa kiume. Wengi wa watoto wa single mama huja kuwa masupastaa wakubwa na mzazi kuishia kula bata.

1.Wazazi ni MUNGU wa Pili
2.Waheshimu Baba na Mama upate Miaka Mingi na Heri Duniani
3.Utapewa Laana wewe….Unatakiwa kuwaheshimu wazazi Mpaka Wawe hawapo duniani.
Hata Kama wakikosea wewe sio wa Kuwaambia wamekosea.
Mzazi hakosei.
Mtoto/watoto Lazima wawatii na Kuwahudumia wazazi.
4.Mtoto hachokozwi bali anafundishwa…
5.Mtoto hakua kwa Mzazi….
6.Siko halizidi Kichwa…
Hivi unaweza kwenda kwa watu ukawaeleza kuwa Baba yako anakuchokoza???
7.Laana ya Mzazi akikutamkia au Akisononeka tuu Hutopata Baraka katika Maisha.
Unatakiwa Uyaishi hayo yooote.
Ni wapi wamewasema sana wazazi dhidi ya watoto??? Jibu ni HAKUNA.
Mkuu nimechokoza tuu Mada daa
 
1.Wazazi ni MUNGU wa Pili
2.Waheshimu Baba na Mama upate Miaka Mingi na Heri Duniani
3.Utapewa Laana wewe….Unatakiwa kuwaheshimu wazazi Mpaka Wawe hawapo duniani.
Hata Kama wakikosea wewe sio wa Kuwaambia wamekosea.
Mzazi hakosei.
Mtoto/watoto Lazima wawatii na Kuwahudumia wazazi.
4.Mtoto hachokozwi bali anafundishwa…
5.Mtoto hakua kwa Mzazi….
6.Siko halizidi Kichwa…
Hivi unaweza kwenda kwa watu ukawaeleza kuwa Baba yako anakuchokoza???
7.Laana ya Mzazi akikutamkia au Akisononeka tuu Hutopata Baraka katika Maisha.
Unatakiwa Uyaishi hayo yooote.
Ni wapi wamewasema sana wazazi dhidi ya watoto??? Jibu ni HAKUNA.
Mkuu nimechokoza tuu Mada daa
Biblia ilivyoandika enyi kina baba msiwachokoze watoto wenu ilikuwa na maana gani?
 
Back
Top Bottom