Akili za namna hii nilikuja kuzikuta huku Tanzania tu. Nilisikitika sana na kutokwa na machozi

Bill Lugano

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
1,186
6,403
Habarini ndugu zanguni.naamini maisha yanaenda mbele kiulaini kama kawaida.kuna jambo nimeli observe mara kadhaa limekuwa likinisikitisha sana.

Hii kauli "Billman ngekuwa kama wewe ningewabandua sana mademu" au "Billman ningekuwa kama wewe ningewatafuna sana mademu"

Mi nilimuuliza jamaa mmoja ungewabandua kitu gani kilichobandikwa kwao mpaka ukafikia hatua ukajiona umewaweza? Ni upuuzi tu.

Wengi wanaamini ukiwa na vidollar kidogo kama mimi kisha una mvuto basi wewe kazi yako inakuwa ni kudate tu.mimi huwa nasema ungekuwa kama mimi usingewaza kama mimi.

Mimi kuwa na magari ya kifahari tena toka Ulaya ambayo hayajapita muda wake wa ku expire.(mimi gari zangu toka itengenezwe hamna iliyofika miaka 5) haimaanishi ndo kigezo cha kuwa natembea tu na kila mary,jane and jack.hapana.

Hili jambo limesababisha hata siku moja nigombane na jamaa yangu mmoja tupo bar moja huko mikocheni anamshika makalio mhudumu.nikamuuliza why unamkosea heshima dada wa watu...akawa tu anacheka.alinikwaza sana yaani siku ile kaja ile sehemu ana 600,000 tu anaamini inampa kibali cha kushika watu makalio hovyo hovyo. Je angegundua mimi kwenye gari nilikuwa nina tsh 27,000,000. Si angetaka kushika mpaka moyo,maini na firigisi/figo kabisa?maana angeona vya nje tu havitoshi.

Nilimdharau sana jamaa na mapombe yake ya namna hiyo.nakumbuka nilimpa yule dada tsh 100,000 tu kumwomba msamaha kwa niaba ya jamaa yangu.

Watu wengine wamekuwa na mawazo potofu kuwa kwa sisi wenye vijihela basi tunatoa tu pesa.hivyo hata ukikutana naye anakuwa na maneno mengi akiamini hutamwacha hivi hivi.mimi huwa silewi sifa za kijinga.kuwa napendeza nina hela naonekana kama black american.hayo nayajua why should i pay you for that?

Jamaa namfahamu huwa anafuta futa magari pale napopark siku hiyo kaniona nipo na sister flani basi kanianzishia sifa kibao.eti mi sikustahili kabisa kuzaliwa tz.(by the way mimi ....) Mwishon naondoka ananiuliza ntamwachaje?nlimwambia tu ntamwacha kama nilivyomkuta

Sijumpa hata ndululu moja.akashangaa naenda mpa mama mmoja msafisha barabara tsh 50,000.

Mimi siamini katika kujenga mahusiano kwa pesa....mwanamke mpumbavu ni mzigo mkubwa sana kwa mwanaume wake.

Mimi nmekutana na watu wenye pesa hapa africa na nje akina bill gate n.k si kwamba wanapita tu wagawa pesa kama karanga.wana mipango.

Akili za kwamba upate pesa ukawanyanyase wanawake ni za kipumbavu.mbona mi nmeshawahi tumia pesa yangu mara kadhaa na sikuwahi ku sex nawahusika.

Ombea kupata akili halafu upate pesa.wengine wengi wapuuzi wangekuwa na pesa kama mimi wangepata maradhi meng sana na pengine kufirisika.

Na si kweli kuwa ukiomba tu nakupa.sijaona mimi akina mo dewj wakifanya hivgo. Akili hizi naziona tu afrika.
 
"Nlimdharau sana jamaa na mapombe yake ya namna hiyo.nakumbuka nilimpa yule dada tsh 100,000 tu kumwomba msamaha kwa niaba ya jamaa yangu."
 
Here We Go!

Je
angegundua mimi kwenye gari nlikuwa nina tsh
27,000,000. Si angetaka kushika mpaka
moyo,maini na firigisi/figo kabisa?maana
angeona vya nje tu havitoshi.
Kiduku ana ujumbe mzuri kiujumla (bila kujali kama story yake ni kweli ama la, kuna la kujifunza), lakini kutembea na pesa kama hizo kwenye gari ni risk kubwa sana, watu wabaya wakijua ni rahisi kumdhuru mtu.

Kuhusu kusaidia watu bila kutaka malipo, hili ni jambo gumu. Maana mara nyingine mtu unasaidia kwa moyo mkunjufu, halafu anayesaidiwa ndiye anaona kwamba anawajibika kurudisha fadhila kwa namna anayoweza yeye.
 
Mkuu Kidukuuuu ktk ubora wako, nilivyosoma title ya thread tu nikajua utakuwa ni wewe.

Wacha niende nikapumzike getho nisome thread yako niongeze siku za kuishi.
 
Kiduku lilo member anayeondoa stress humu jf japo wengine nahisi hawajamuelewa jamaa maana wanatokwa na povu kwenye nyuzi zake
 
Back
Top Bottom