kisugujira
JF-Expert Member
- Aug 13, 2012
- 774
- 196
Kutokana na uhaba wa ajira uliopo sasa hivi nchini, vijana tunaotafuta ajira tunatakiwa kuwa makini na taasisi za nje zinazotoa matangazo ya kuwepo nafasi za kazi kwa niaba ya makampuni yanayotaka au tayari yanafanya kazi hapa nchini.
Vijana wengi tusio na ajira tumekuwa tukituma maombi ya kazi kwenye makampuni mbalimbali kupitia taasisi hizi bila mafanikio yoyote! Taasisi hizo au mawakala hao wa kazi toka nje kama My Jobs Eye na Prime Time Personnel Africa ya nchini Kenya yanafanya kazi kibaguzi. Wanatoa matangazo ya nafasi za ajira kwa watanzania lakini wanaopata kazi ni wakenya!
Mara nyingi utakuta wanataka mtu awe na elimu ya sekondari ya KCSE yenye C tupu (with C plain), kibali cha kufanyia kazi,pasipoti,leseni ya gari daraja BCDE na kadhalika. Kwa hiyo utaona mahitaji yote hayo huwa ni kwa mtu asiye raia wa hapa nchini. Wanakuwa wameisha waandaa watu wao toka Kenya kuja kufanya kazi hapa nchini.
WanaJF nini kifanyike kuondoa ukilitimba huu?
Nawakilisha.
Vijana wengi tusio na ajira tumekuwa tukituma maombi ya kazi kwenye makampuni mbalimbali kupitia taasisi hizi bila mafanikio yoyote! Taasisi hizo au mawakala hao wa kazi toka nje kama My Jobs Eye na Prime Time Personnel Africa ya nchini Kenya yanafanya kazi kibaguzi. Wanatoa matangazo ya nafasi za ajira kwa watanzania lakini wanaopata kazi ni wakenya!
Mara nyingi utakuta wanataka mtu awe na elimu ya sekondari ya KCSE yenye C tupu (with C plain), kibali cha kufanyia kazi,pasipoti,leseni ya gari daraja BCDE na kadhalika. Kwa hiyo utaona mahitaji yote hayo huwa ni kwa mtu asiye raia wa hapa nchini. Wanakuwa wameisha waandaa watu wao toka Kenya kuja kufanya kazi hapa nchini.
WanaJF nini kifanyike kuondoa ukilitimba huu?
Nawakilisha.