Ajira ni ngumu jamani

Ajira ni ngumu jamani

dah bora ww umeitwa kwenye kujitolea mm hata kujitolea nanyimwa naambiwa niandike barua kwa mkulugenzi then nikifuatilia majibu yangu naambiwa nafasi za kujitolea hakuna saizi serikalini hapa halmashauri ya jiji lambeya
huenda makosa yaliyopo hapa ndo unayafanya na huko wanakuona sio mtu makini pole sana
 
Hili nalo neno....ndo maana nime post uzi mwingine ktk forum ya biashara.... nataka kwenda singida nikanunue mayai ya kienyeji.....bt kuna mambo kadhaa yananitatiza nimeomba ushauri huko
Bora hiyo biashara unayoifikiria kuliko kuuza duka la wachina lakini kama unaona utapata experience yoyote kulingana na ulichosomea fine, binafsi naona bora ufanye biashara unayoifikiria.
 
Ndugu mm nimeambiwa nikajitolee kwenye duka la wachina sasa cjui kwa experience hapo napatana nn..... labda kwenye connection ndo naamini nitapata
unataka kuajiriwa au unataka kufanya biashara?
huko dukani pia si utapata experience za biashara?halafu huwezi jua huko vichenji chenji huwa havikosekani waweza shangaa ukawa unarudi nyumbani kila siku na elf kumi, ungekaa nyumbani ungeipata?
pia ukiona huiwezi, haikusaidii si unaacha mama
 
Hiyo hela ya nauli mwezi mzima plus hela ya chakula mchana mara miezi utakayofanya kazi bora ukaziweka ukafungua biashara ya karanga kwa mwezi unajua umeingiza faida kiasi kuliko kumfaidisha mtu bila malipo, fanya marketing for your own business
Good advice
 
Kwa dunia ya sasa ni kazi kupata kazi. Inakuhitaji uwe na moja kati ya vitu vifuatavyo ili uweze kuipata;

1. Wealth (ambayo huna)

2. Family background (kwa wenzangu na Mimi hii pia hatuna background nzuri)

3. Connection

4. Reputation

5. Knowledge and experience.

Kuanzia namba 3-5 Unaweza ukazitengeneza kupitia nafasi hiyo uliyoipata. Kama sio mbali sana na unakoishi ni vizur ukajitolea maana kupitia hapo utapata vyote. Kila la kheri na Mungu akujalia mema.
 
Hili nalo neno....ndo maana nime post uzi mwingine ktk forum ya biashara.... nataka kwenda singida nikanunue mayai ya kienyeji.....bt kuna mambo kadhaa yananitatiza nimeomba ushauri huko

Mayai ya kienyeji kuwa nayo makini sana,yakilowana tu au kupatwa na maji ni hasara tayar yanaharibika
 
Mimi nilishafanya internship ofc flan nilijigharamia kila kitu. Hta photocopy na print sikutumia,walikuwa wanachukuwa namba ya photocopier ya mwisho asubh na jioni. Mpaka leo sijawahi kusahau ile hali,nilijiona inferior sana but nilipata uzoefu. Nenda kafanye ili upate uzoefu
 
Nenda kafanye mkuu ukiwa kazini kazi zitakuja lakini ukikaa home mhh mi nilipata kazi kabisa na makubaliano kila kitu ni company ya MTU ila ilikuwa ikifika mwisho wa mwezi dah hadi kichwa kinauma naenda dai pesa yangu kama naomba msaada ila sikuacha pale pale nikatengeneza connection na watu nikapata kazi nyingine nikaondoka ila cha moto nilikuwa nakiona hivo usikate tamaa nenda
Hongera mkuu kwa ushauri mzuri na wa hekima.
 
Huku wanalilia kazi,huku voda,airtel wanapunguza wafanyakazi sababu ya mtikisiko wa uchumi.

DUNIA UWANJA WA FUJO.
 
Kuna ofisi nyingine wanaojitolea wanapewa pesa ya usafiri na kula mchana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom