Ajira kwa misingi ya vyama italivuruga Taifa

Ajira kwa misingi ya vyama italivuruga Taifa

Molembe

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
9,933
Reaction score
11,863
Hivi karibuni umekuwepo utaratibu wa kuajiri vijana wanaotokana na chama, ajira hizo zilianzia kitengo na hivi karibuni wameajiriwa watendaji wa kata zaidi ya 300 na ajira zao zilitangazwa ndani ya chama tu, na vijana hao wameanza kazi mwezi wa 8.

Ajira za namna hii zitaligharimu taifa, mchakato wa ajira unapaswa kuwa wazi kwa kila mtu na sio kuangalia makada na wakereketwa wa chama, tukumbuke kuwa watendaji hawa wanakuja kuhudumia watu wasio na vyama na wenye vyama, tuache kuingiza iguana kwenye utumishi wa umma.
 
Kwamba matangazo ya kazi yalibandikwa kwenye mbao za matangazo za ofisi za CCM tu.
 
Huku Zanzibar huajiri kama familiya yenu siyo ccm na kama huna kadi ya ccm ndio ajira utaisikia tuu nahata uwe na vyeti umejaza kabati kama huko chama cha ccm sahau kuajiriwa
Pole sana mkuu. CCM wanatumia mbinu nyingi sana kuongoza nchi.
 
Unaajiri watu wakiwa ofisiani kila kitu kupinga tu ,ofisi zinajaa migogoro na masiasa yasiyoisha

Mara kila siri za ofisi unazikuta mitandaoni kila siku.mtakaa sana nyumbani hadi muitwe baba wa nyumbani


Nashauri usaili uangalie background za kisiasa watu wawe eliminated mapema .


State agent
 
Mm mwenyewe nilifanya intaview ya civil engineering office ya manispaa huku kwetu Zanzibar tunaita baraza La mji walihitaji MTU aliyena digree ya civil engineering ili wapate mtu wa kuwarekebishia mipango miji pamoja na siter plan tulienda kufanya inteview ile ktk shule ya Fidel Castro iliyopo vitongoji Chake Chake tulikuwa watu watatu mm na wenzangu wawili wote tulikua wanaume.

Kwa bahati mzuri ile nafasi nikabahatika kupita jina langu na jina lango likaenda ktk office flani nyeti na jina lile wakaagizwa vijana watatu ktk office ile wanifuatilie nyendo zangu ndio wakafika mpaka kwa sheha kwajina huko bongo munamwita mwenyekiti wa mtaa basi walupo fika walisalimiana vizuri na wakamuliza yule sheha jee hili jina hili unalijua naakapewa na picha ya passport size sheha akajibu nalijua na akauliza ananini akaambiwa huyu ameomba ajira na amefanikiwa lkn tumekuja kwako utupe sifa zake sheha akawambia wale vijana huyu MTU hafai kumpa kazi na wala hafai kufanya kazi ktk serekali hii mmoja wa wale vijana akauliza kwanini sheha akajibu huyu kijana wazazi wake ni wa vyama pinzani na yy mwenyewe ni mpinzani kwahiyo bora hata mutafute MTU kutoka sehemu yoyote lkn huyu hafai

Basi jamaa wakaenda zao na wakapeleka maelezo Yale Yale waliyopewa .sasa kuna msemo ambao wahenga husema kwenye wabaya na mwema hakosi siku hiyo nimo ktk uwanja wa gombani uliopo chake chake Pemba ilikua nikiangalia mechi kati ya timu ya jamhuri na jangombe boys kuna yule kijana aliyetoka ktk office nyeti akaja kuniambia umemkosea nini sheha wako nikamwambia mm sija mkosea akanimbia mbona anakuchukia na anazizuia rizki zako nikamwambia mm sina ugomvi mbona akaniambia basi kama ww huna ugomvinae lkn jina lako ilikua lishapita lk. Sheha wako kalizuia kasema ww hufai kupewa kazi ile kwa sababu wazaziwako ni chama cha upinzani

naombeni muniamini kwa haya maneno niliondika mm sikusingizia wala sikuandika kwa chuki Bali huo ndio ukweli na mpaka barua nilizoomba ninazo nilizotoa kopy
 
Unaajiri watu wakiwa ofisiani kila kitu kupinga tu ,ofisi zinajaa migogoro na masiasa yasiyoisha

Mara kila siri za ofisi unazikuta mitandaoni kila siku.mtakaa sana nyumbani hadi muitwe baba wa nyumbani


Nashauri usaili uangalie background za kisiasa watu wawe eliminated mapema .


State agent
Nakuhakikishia mm binafsi na ni mtoto wa kislam aje mtu na panga anambie chagua kuuliwa au chagua ccm naona bora aniuwe naongea kwa machungu kwani ccm iliniulia wazazi wangu wawili akiwemo baba angu mzazi na mjomba wangu mwaka 2001 ktk maandamano hao ilikua wanatoka nyumbani wanaenda mskitini wakapigwa risasi njee ya nyumba yetu na kama wataka ushahidi mulize Benjamin William mkapa ktk kitabu chake anachosema anajutia kitendo kile cha watu 22
 
Abdalla mpemba,

Sheha ni sawa na balozi wa nyimba kumi? Kama ni kweli basi ninaamini miaka mia moja ijayo wajukuu na vitukuu vyetu vitakuwa vinaulizana kwanini nchi yetu ndiyo nchi maskini kuliko nchi zote alizoziumba Mwenyezi Mungu? Na hata wakiambiwa kuna chama cha siasa kiliamua msiendelee na muishi kama maskini na madhalili wa ulimwengu huu hawataamini.

Njia pekee kwa sasa kwa wenye akili ni kuhamasisha watoto na wajukuu kukimbilia nje, hasa kwa wazungu. Miaka hiyo angalau watapatikana watakaochanganya damu hii na nyingine. Damu ya mtanzania kwa mtanzania haitaweza kuishi katika dunia ya miaka michache ijayo.

Utanzania utaweza kufikia kuwa kiashiria cha kushindwa, umaskini, uduni wa fikra, uduni wa elimu, ubabaishaji, wizi, ufisadi, unafiki nk. Binafsi nitafanya karakati za aina zote nipeleke kizazi huko nje kwa rangi nyingine na binadamu wenye utamaduni mwingine. Labda itasaidia.
 
Ndiyo maana ni halali kutowapa ushirikiano watendaji wa namna hiyo. Do the minimum to keep things going.
 
Abdalla mpemba,
Kwa aliyeishi Zanzibar hilo jambo atakuwa anajua vizur sana, kwenye ajira za serikali Zanzibar ni kichefuchefu.
Nina rafiki yangu alipelekwa kusoma nje na chuo cha SUZA karudi wamemzungusha mwaka wa 2 sasa wakiamini yeye ni mfuasi wa CUF.

Pia yupo bint naye kaepelekwa India anarudi aanze ajira akaolewa na mtoto wa kiongozi wa CUF basi walimwambia live kuwa hakuna ajira na nafasi ipo wazi wanaitafutia mtu mwaka sasa wakati serikali imetumia pesa nyingi kumsomesha nje.
 
Unaajiri watu wakiwa ofisiani kila kitu kupinga tu ,ofisi zinajaa migogoro na masiasa yasiyoisha

Mara kila siri za ofisi unazikuta mitandaoni kila siku.mtakaa sana nyumbani hadi muitwe baba wa nyumbani


Nashauri usaili uangalie background za kisiasa watu wawe eliminated mapema .


State agent
Unaona ni sifa kuandika haya lakini siku hicho unachoshabikia kikafitinika utajutia mengi mno.
Mtabaki wenyewe kwenye ajira zote za serikali na hapo ndio mtaanza kuulizana maswali mbona kanda ile wapo wengi sisi wa kanda hii tupo wachache?

Hakuna dhulma na usaliti ushawahi kudumu au kuleta furaha ya milele amini hivyo.

Furaha mnayoipata sasa hivi baada ya kugawiana vyeo mtaikosa muda si mrefu, mkumbuke kila mtu atakuja kuwa mwanachama wa CCM na kwakuwa serikai yenu haina uwezo wa kuajiri watu wote na kibaya zaid mmejaza vijana kwenye makambi yenu mkiwaahidi ajira kama wataendelea kumshangilia Mtukufu wenu, sasa upinzani na fujo za kukosekana kwa ajira zitaanzia CCM, na kama huamin nitajie kijana mmoja tu aliyetoka Upinzani anayependwa na vijana wa CCM?
 
Kwamba matangazo ya kazi yalibandikwa kwenye mbao za matangazo za ofisi za CCM tu.
Jua kwamba namba ya kadi ya chama inahitajika kwenye application!!!lazima uandike mimi comrade jiwe bashite kadi namba 554000 chama cha mapinduzi!ndio unapata ajira!kama una mdogo wako yupo chuo mwambie atafute kadi ya ccm namba yake itatumika kwenye application!!!
 
Back
Top Bottom