Ajira kutolewa mwakani

Ajira kutolewa mwakani

Kama huna ajira na unasubiri ajira za serikali basi nakushauri kuwa na imani.

Aliwazalo mtu ndilo alipatalo,kama unataka kusubiri hadi julai sawa waza haya.
 
Waziri wa utumishi wa umma na utawala bora Angella Kairuki amesema serikali itaanza kutoa ajira mwakani mwezi wa pili 2017 na kupandisha madaraja vyeo na kulipa stahiki mbalimbali za watumishi wa umma. Kairuki ameyasema hayo akiwa kwenye ziara ya kikazi jijini dar es salaam amesema kuwa mda huu serikali ipo kwenye hatua za mwisho za kukamilisha zoezi la uhakiki wa watumishi hewa na kubadilisha miundo ya utumishi wa umma pamoja na kupitia upya mishahara ya watumishi sekta binafsi kwa miezi iliyobaki mwaka huu.

Kairuki ameongea hayo akiwa anaulizwa swali na waandishi wa habari kuhusu Serikali itaajiri lini amewataka watanzania kuwa wavumilivu pindi zoezi la uhakiki linafanyiwa tathimini kwa mapana.
 
Kipind cha mpito,sasa ndg zangu waliokuwa wamesain mkataba na serkali tayar na wao mpaka mwakan? Na wamesimamishwa ajira zao mpaka mwakan na bila Malipo? Sheria inasemaje ktk mikataba ya kaz?
 
Mlimchagua wenyewe kwa hio hakuna namna acha awanyooshe
 
Back
Top Bottom