Endelea kushabikia Moto kwa Jirani huku kwako nako kunafuka MOSHI. Unaingiza propaganda za Jukwaa la Siasa kwenye maisha ya Watu na Msiba mkubwa kama huu?
Wakuu nimestaajabishwa sana na hili hasa kwa upande wa TV stations ikiwa za nje zimeweza kuujuza ulimwengu kwanini TV stations zetu hawana updates/wamechelewa kutuletea updates zaidi ya kutuonyesha cartoons na maandishi kupita kwa chini? Au wapo busy na Miss Tanzania? Inasikitisha sana.
duh kugumu hapa
duh....edit basi post yako kidogoZanzibar ni majiran wa tanganyika kama ilivyo rwanda, kenya na uganda. 2004 abanyagwanda walichinjana na kilisha samaki wetu wa mto kagera na watanzania waliendelea kucheza kiduku. Kenya-after erection riots zilizalisha maiti nyingi wakati wa TZ wakiendelea kunya kahawa-zanzibar siyo tanzania.
Baada ya Tukio la MV Bukoba katika ziwa VICTORIA na kama idadi ya watu wanaohofiwa kupoteza maisha ikawa hiyo inayodhaniwa kati ya 1500 - 2000 itakuwa ni ajali ya majini kubwa kuliko zote katika historia ya Taifa hili. Huu ni msiba usioelezeka (endapo idadi itakuwa hiyo ama kuvuka)
Kwa mintarafu hiyo Uncle Lundenga na Ndugu yangu George Rwehumbiza hamna sababu yoyote ya kuwaweka Watanzania pale Mlimani City wakimkufuru Mungu huku wengine wanaomboleza. Najua mnaweza kutia pamba masikio na mkaamua kuobserve silence kwa dakika 1, lakini dhambi hii haitawatoka kamwe kama mtapuuza maono haya.
Kama kawaida yetu tutasema unajua tumekodi na kulipa gharama kubwa kwa wataalam kutoka maeneo mbalimbali ndani na Nje ya Tanzania kwa hiyo hatuwezi kupoteza fedha hizi na hakuna wa kuzilipa tena kuandaa Tamasha, Aaah nyie watu hizi fedha za nani kama si wauza vitumbua na karanga wa msata hadi mahenge ambao hawalali wakikesha kutuma meseji na kushiriki bahati nasibu wasiyoshinda hata siku moja huku shilingi zao zikiteketea kama fupa katika domo la fisi.
Ndugu zetu wapendwa wa VODACOM na LINO AGENCY INTERNATIONAL kaeni meza moja na mtafakari hili msiba huu leo ni mkubwa kwa Taifa, hatuna haja ya kusherekea kupitia matangazo ya LIVE katika Luninga kwa mabinti zetu kupita wakiwa Nusu Uchi huku mamia ya ndugu zao bado wapo majini miili yao ikiwa inasakwa na huzuni kubwa imeligubika Taifa.
Kila jambo ni mapenzi ya Mungu na kwa moyo wa Unyenyekevu kabisa natoa pole kwa familia zilizoguswa na msiba huu kwa niaba ya wana JF wenzangu.
Bwana Alitoa, Bwana Ametwaa...Jina lake lihimidiwe
Ina lilah waina ilaih rajuun