Ajali ya Dr. Mwakyembe na yatokanayo

Mwakyembe kaka yangu mpiganaji, tumekusikia. Amini Mungu atakushindia kama alivyokushindia katika ajali ile, gari iliumia na ukatoka ndani bila hata mchubuko wa kutoa damu. Jua Mungu ni mwema na anakupigania kila mahali. Kama kuna waliokuwa wanasubiri kujipongeza baada ya ajali basi wameshindwa na walegee kabisa. We tulia endelea na kazi zako vyema hasa kujipanga kujiandaa vema kwa uchaguzi ujao. Jimbo ni lako.
 
Ukweli plain truth ni short, simple na clear na direct to the point, kama Masia alivyosulubishwa bila kosa lolote
Hakuwa na maelezo mengi zaidi ya kusema 'wewe wasema'.
Dr ambaye yu mgonjwa, hakuhitaji kujisafisha kwa maelezo yote hayo na kuingia kwenye technicalities
Za kisheria kwa andiko safi la kiuandishi wa habari.
Angetulia tuu kwanza apone ndipo alonge.

Mengi alipowatukana mafisadi papa, kuna wenye busara walimuona ni mjinga fulani, Rostam alipomjibibisha na kumuita fisadi nyangumi, wale wenye busara wanamuona RA ndio mjinga wa wajinga. Jeethu pamoja na ufisadi wake, hajajibu, hajaitisha press conference, hajatoa statement yoyote na hatajibu chochote, huyo ndio wakumuogopa.
Ili Dr alinde heshima yake, hana haja ya kusema saana na andiko refu. Yeye tayari ni mheshimiwa na anaheshimiwa hata akikaa kimya.

Mbona Dr Mwakyembe ameshasema ni kwa nini ameandika!

Pamoja na kwamba bado naumwa na niko nyumbani nikipumzika kwa ushauri wa madaktari, nimelazimika kuvunja ukimya na kutoa taarifa hii fupi kuzuia upotoshaji wa makusudi unaofanywa na magazeti, hususan gazeti la Tanzania Daima, na baadhi ya viongozi wa Jeshi la Polisi kwa sababu wanazozijua wenyewe kuhusu suala hili.
 
''ni nani katika kamati hiyo ana utaalamu kunipita mimi?''

hakya mungu nchi hii!!!!!?

we acha tu.

Mkuu, habari yote ile umeona kakipande hako tu kweli......?kwa maneno mengine, ujumbe uliopata kny press release ya Dr. Upo hapo kny quatation yako tu?....try to be objectively jamani.....khaa!

Hizi tabia za kukatakata maneno ilikupata tafsiri tofauti ni tabia za kishetani!

Shangaa saa.....yaani wana mcho lakini hayaoni.....wana masikio lakini hayasikii kabisa!
 
Mmh! Hapa panafuka moshi na nafkiri utawaka tuu, na maji waliyotaka kumwagia yamekuwa kama mafuta wanashikwa na butwaa au walichanganya dumu wakaacha la mafuta wakabeba maji, na wakirudi kwenye hifadhi yao wanakuta dumu la mafuta bado lipo na limejaa telee! Aah! Wanaanza kumsaka mchawi eti kuna mtu kahujumu mbinu yao,japo aliyepewa pesa ya maji ya kuzimia moto ni mwanamtandao asiye na doa na mkomavu, ama kweli siku ya kufa mafuta maji hutumika!oh
 
Ushabiki aside, kwa hili conduct ya Geshi letu la polisi inashangaza na hili inawezekana linasababishwa na incompetency au pure cover-up. Verdict ya kuwa Mwakyembe alikuwa amelala inashangaza haswaa kwa kuwa hakuna ushahidi wa observer yeyote unaothibitisha hilo. Hivi polisi wanaweza wakatunga kitu cheap kama hicho??

Watu kusingiziwa makosa hasa kwenye kesi za trafic ni jambo la kila siku. Ukipata ajali hasa hizi ndogo ndogo za kukwatuliwa na dala dala usipoangalia vizuri, unagongwa na unatiwa hatiani wewe. Hilo ni jambo la kila siku. Ile michoro wanayojifanya kuchora usipoangalia vizuri au kama huelewi utashangaa kweli kweli. Sheria za bara barani ziko wazi lakini wanapochora wakikuona ni unsuspecting, umeliwa.

Watu kubambikiziwa kesi ni jambo la kawaida. Ukishafikishwa kituoni, unaweza kubebeshwa misokoto ya bangi au kete za madawa ya kulevya. Lengo lao huwa ni moja tu, utoe rushwa. Haya huwa wanayatumia kutisha watu, 90% of the cases watu hutoa rushwa yakaishia huko huko. Sasa hii imeshakuwa ndo 'modus operandi' ya polisi wetu.

Sasa kwa hili, sijui kama kuna motive ya kukatiwa kitu kidogo, ukizingatia kesi yenyewe ni high profile. Motive ya polisi hapa itakuwa nini?? Shimo ni kweli watu walioliona hilo shimo walikubali haliwezi kusababisha ajali kwa gari ile. Lakini kauli ya shimo ilitoka kwa mkuu wa polisi wa mkoa, RPC!!! Ghafla kamati inakuja na new theory baada ya kuona theory ya RPC haina mshiko. Sasa kama hawa watu waliona RPC wao alichemsha kwa kutoa kauli mapema, suluhu yake ni hii??

Ni kweli ndani ya jeshi la polisi kuna matatizo makubwa. Kuna incompetence. Kuna kutojali. Kuna rushwa na mengine machafu mengi. Sugarcoat iliyofanyika pale juu alipoingia Kikwete haijasaidia sana kulifanya jeshi hili liaminike. Mojawapo ya vitu vinavyofanya watu tufikirie mara mbili ni pamoja na huku kujichanganya na kukosekana kwa coherence katika statement zao.
 
Naomba kuulizwa swali? Ajali ya Chenge iliundiwa Tume? majibu yametoka Kwa nini kwa mwakyembe ripoti imekuwa haraka sana? Nafikiri tume zote zingekuwa haraka hivi hata hela za wananchi zisingepotea hivyo.
 
Swali: Mbona Chenge alipogonga na kuuwa watu wawili alitokea kwenye TV na magazeti yakaandika na ni mwaka huu huu akielezea ilivyokuwa na tena akisindikizwa na polisi wengi. Au sheria na makatazo hayo ya polisi yamepitishwa lini au polisi wamesahau. Chenge ni Mbunge na Mwanasheria kama mwakyembe? Polisi wakitoa ufafanuzi na tofauti ya matukio haya mawili iatakuwa vizuri
 
Baadhi yetu tunashiriki kikamilifu kuwalewesha sifa viongozi wetu wazuri tu. Matokeo yake wakishalewa sifa hizi wanakuwa watu wa kulialia tu, kujitetea tu, kudhani wana maadui wengi tu, kuamini kuwa baya lolote kwao lina mkono wa mtu....Matokeo yake tunawapoteza kwenye uongozi wanabaki kukimbizana na vivuli vyao tu.
 
Baadhi yetu tunashiriki kikamilifu kuwalewesha sifa viongozi wetu wazuri tu. Matokeo yake wakishalewa sifa hizi wanakuwa watu wa kulialia tu, kujitetea tu, kudhani wana maadui wengi tu, kuamini kuwa baya lolote kwao lina mkono wa mtu....Matokeo yake tunawapoteza kwenye uongozi wanabaki kukimbizana na vivuli vyao tu.



Ajali ya kujitakia hii .... Mwakyembe, siku nyingine awe makini, na amuache dereva afanye kazi yake na siyo kumlazimisha kuvunja taratibu za barabarani ... yeye ni abiria tu!!
 
Ajali ya kujitakia hii .... Mwakyembe, siku nyingine awe makini, na amuache dereva afanye kazi yake na siyo kumlazimisha kuvunja taratibu za barabarani ... yeye ni abiria tu!!

Na wewe ulikuwepo kwenye gari la Mwakyembe wakati linapata ajali? au Dereva wa gari lile kakwambia alikuwa ''anaendeshwa'' na Mwakyembe?
 
Swali: Mbona Chenge alipogonga na kuuwa watu wawili alitokea kwenye TV na magazeti yakaandika na ni mwaka huu huu akielezea ilivyokuwa na tena akisindikizwa na polisi wengi. Au sheria na makatazo hayo ya polisi yamepitishwa lini au polisi wamesahau. Chenge ni Mbunge na Mwanasheria kama mwakyembe? Polisi wakitoa ufafanuzi na tofauti ya matukio haya mawili iatakuwa vizuri

Shangazi,

Usipotoshe ukweli hapa; case ya Chenge na mwakyembe ni tofauti. Ajali ilipotokea polisi na Mwakyembe walitoa taarifa zilizokuwa zinapingana. Moja ikisema waligongwa kwa nyuma na polisi wakisema hawakugongwa na badala yake ilikuwa makosa ya dereva.

Pia Mwakyembe alionyesha kama kulikuwa na uwezekano wa kutokuwa ajali ya kawaida.

Kwenye mazingira kama hayo ilikuwa vizuri kwa polisi kuunda tume ili kuhakikisha ukweli unapatikana. Kibaya zaidi hii ajali imetokea wakati Mwakyembe yuko kwenye malumbano na baadhi ya watu (mafisadi).

Kama ilivyo Tanzania, polisi hawakuwa makini kwenye uchunguzi wao; wameacha mapengo mengi ambayo sasa Mwakyembe anayatumia kuonyesha mapungufu kwenye taarifa yao.

Kwa ujumla hii case na ya Chenge ni tofauti. Chenge hakusema kwamba kunaweza kuwa na mkono wa mtu. Polisi wamefanya uchunguzi na case ya Chenge iko mahakamani. Hata uchunguzi wa case ya Chenge ulikuwa wa haraka, labda case ndio itachukua muda mrefu kusikilizwa.
 
Mimi binafsi nilistushwa sana na taarifa ya ajali ya Mh Mwakyembe lakini baada ya maelezo kupatikana kutoka kwake na dereva wake na baadae Polisi nimepata ninashawishika kabisa kusema kuwa ni ajali ya kawaida ina kwa sehemu kubwa imesababishwa na uzembe wa dereva wa Mh Mbunge.

Nikirejea maelezo ya awali kuwa lorry ndiyo lilikuwa linataka kuipita gari ya mheshimiwa na wakati huohuo mbele kwa upande mwingine kulikuwa kuna kuja basi la abiria, badala ya dereva wa mheshimiwa kupunguza mwenndo ili lorry litangulie, yeye akafanya maamuzi ambayo hayakuwa sahihi kwa kuongeza mwendo wa gari lake.

Hali hiyo ilikuwa ni hatari kwa wale waliokuwa katika lorry na basi la abiria pia. Laiti kama asingeliongeza mwendo ni wazi angeweza kulimiki gari lake vizuri na kuondoa hofu aliyokuwa nayo kwa wakati ule.


Sasa nikirejea katika hayo maelezo ya Mh Mwakyembe, nadhani amekosea kabisa kufanya hivyo kwani nchi hii inaendeshwa kwa utawala wa sheria ambazo wao ndiyo watungaji. Hakupashwa kulalamika wakati huu ambapo tayari mamlaka husika zimesha sema kuwa tatizo alikuwa ni dereva wake na atafikishwa katika mahakama kujibu mashtaka. Haya ambayo Mwakyembe anayoyaongea alitakiwa akayatoe mahakama kama shahidi wa dereva wake na si vinginevyo.

Tafsiri inayojitokeza ni kuwa Mh anataka kupindisha shauri zima kwa ajili ya 'kumsaidia' dereva wake. Hayo ya kuanza kusema hii ajali inaweza kuwa na mkono wa mtu ni mawazo finyu sana kuongelewa na mtu kama mbunge kwenye hadhara.
 
Shangazi,

Usipotoshe ukweli hapa; case ya Chenge na mwakyembe ni tofauti. Ajali ilipotokea polisi na Mwakyembe walitoa taarifa zilizokuwa zinapingana. Moja ikisema waligongwa kwa nyuma na polisi wakisema hawakugongwa na badala yake ilikuwa makosa ya dereva.

Pia Mwakyembe alionyesha kama kulikuwa na uwezekano wa kutokuwa ajali ya kawaida.

Kwenye mazingira kama hayo ilikuwa vizuri kwa polisi kuunda tume ili kuhakikisha ukweli unapatikana. Kibaya zaidi hii ajali imetokea wakati Mwakyembe yuko kwenye malumbano na baadhi ya watu (mafisadi).

Kama ilivyo Tanzania, polisi hawakuwa makini kwenye uchunguzi wao; wameacha mapengo mengi ambayo sasa Mwakyembe anayatumia kuonyesha mapungufu kwenye taarifa yao.

Kwa ujumla hii case na ya Chenge ni tofauti. Chenge hakusema kwamba kunaweza kuwa na mkono wa mtu. Polisi wamefanya uchunguzi na case ya Chenge iko mahakamani. Hata uchunguzi wa case ya Chenge ulikuwa wa haraka, labda case ndio itachukua muda mrefu kusikilizwa.

Nakubaliana na wewe kabisa kuwa hizi case ni tofauti, moja iliua wawili na ilikuwa dar na nyingine hakuua na ilifanyikia Iringa

Ila kuna ukaribu wa hali ya juu hasa katika uundani wa kamati

Kamati iliyoundwa kwa ajili ya Chenge ilimchukua mpaka eneo la tukio na kumhojihoji kidogo kisha kufungua kesi ambayo mpaka leo haijulikani inaendelea vipi

Kamati ya ajali ya Mwakyembe ilitoa taarifa ikiwa ina ushahidi tosha kuwa Dereva wa Lorry hana makosa na wao walijua kila kitu kilichotendeka wakati wa ajali bila hata ya kumhoji Mwakyembe na Dereva wake. Sasa hapa ndipo tunajiuliza kuwa kuna nini?, iweje kamati itoe taarifa siku tatu tu wakati ile ya Chenge mpaka leo Ipo kimya?.

Ukweli ni kwamba wanasiasa wa bongo wanavipa wakati mgumu sana vyombo vya dola kufanya kazi kitaalam. Kila kitu ni maagizo tu fanyeni hivi fanyeni vile. Yaani mwanasiasa huyohuyo, hakimu huyo huyo, polisi huyo huyo and everything.

Wao wanaona wanalinda maslahi yao lakini kwa undani zaidi wanaiangamiza nchi kwa kiasi kikubwa. Huwezi kuwa na double standards katika kushughulikia mambo ni kinyume kabisa na utawala wa sheria ni kama tunatawaliwa kiimla.

Yaani ili uwe salama jipendekeze kwa aliyeshika dola vinginevyo huna haki hivi, siku akishika dola mwingine aliyenyimwa haki leo unatarajia na yeye afanye nini?. tunakoenda si kuzuri kama tutaendelea kuwa na viongozi wabovu wa fikra kiasi hiki.

Kwa nini Tume iwe na kiherehere cha kutoa taarifa bila kuwa na all facts on the table?, huku ni kuua professionalism. Ninaamini kabisa kuwa kuna undue influence towards all conclusion reached in Mwakenyembe's accident.

Tubadilike muda bado tunao tuache kutumia vyombo vya dola kwa manufaa ya wachache tutalipeleka taifa pabaya.
 
Hivi Mwakyembea mbona muongo hivi huyu Mbunge? Leo anadai alisema toka awali hii ni ajali, na hiki nini:
Ninamheshimu sana Dr Mwakyembe lakini kwa kauli zake za kutatanisha naanza kuwa na mashaka na uwezo wake kiuongozi he looks like mtu wa mitaani.Please sir acha kubishana bishana.Utajiongezea heshima kwa sisi tunaokuheshimu.
 
Hii ajali nilihisi kuna kitu lakini sasa naamini kabisa kulikuwa na kitu. Walitaka ku-kukolimba ndugu yangu
 
Mimi binafsi nilistushwa sana na taarifa ya ajali ya Mh Mwakyembe lakini baada ya maelezo kupatikana kutoka kwake na dereva wake na baadae Polisi nimepata ninashawishika kabisa kusema kuwa ni ajali ya kawaida ina kwa sehemu kubwa imesababishwa na uzembe wa dereva wa Mh Mbunge. Nikirejea maelezo ya awali kuwa lorry ndiyo lilikuwa linataka kuipita gari ya mheshimiwa na wakati huohuo mbele kwa upande mwingine kulikuwa kuna kuja basi la abiria, badala ya dereva wa mheshimiwa kupunguza mwenndo ili lorry litangulie, yeye akafanya maamuzi ambayo hayakuwa sahihi kwa kuongeza mwendo wa gari lake. Hali hiyo ilikuwa ni hatari kwa wale waliokuwa katika lorry na basi la abiria pia. Laiti kama asingeliongeza mwendo ni wazi angeweza kulimiki gari lake vizuri na kuondoa hofu aliyokuwa nayo kwa wakati ule.
Sasa nikirejea katika hayo maelezo ya Mh Mwakyembe, nadhani amekosea kabisa kufanya hivyo kwani nchi hii inaendeshwa kwa utawala wa sheria ambazo wao ndiyo watungaji. Hakupashwa kulalamika wakati huu ambapo tayari mamlaka husika zimesha sema kuwa tatizo alikuwa ni dereva wake na atafikishwa katika mahakama kujibu mashtaka. Haya ambayo Mwakyembe anayoyaongea alitakiwa akayatoe mahakama kama shahidi wa dereva wake na si vinginevyo. tafsiri inayojitokeza ni kuwa Mh anataka kupindisha shauri zima kwa ajili ya 'kumsaidia' dereva wake. Hayo ya kuanza kusema hii ajali inaweza kuwa na mkono wa mtu ni mawazo finyu sana kuongelewa na mtu kama mbunge kwenye hadhara.


Mzee unavyeleza kwa utaratibu mtu anaweza kusema unalamaana, hamna kitu yaani mie naona hujasema kitu! yaani baada Dk kushutumiwa kusema uongo na kuambiwa akae kimya kuhusu ajali yake wewe ulitaka akae kimya tu!!?
"Mamlaka zinazo husika zimeisha sema......" yaani kweli wewe na cheo chako humu JF wakuyasema haya?? mamlaka zikishasema basi tumeishamaliza? he? Mungu tusaidie.
 
Nakubaliana na wewe kabisa kuwa hizi case ni tofauti, moja iliua wawili na ilikuwa dar na nyingine hakuua na ilifanyikia Iringa

Ila kuna ukaribu wa hali ya juu hasa katika uundani wa kamati

Kamati iliyoundwa kwa ajili ya Chenge ilimchukua mpaka eneo la tukio na kumhojihoji kidogo kisha kufungua kesi ambayo mpaka leo haijulikani inaendelea vipi

Kamati ya ajali ya Mwakyembe ilitoa taarifa ikiwa ina ushahidi tosha kuwa Dereva wa Lorry hana makosa na wao walijua kila kitu kilichotendeka wakati wa ajali bila hata ya kumhoji Mwakyembe na Dereva wake. Sasa hapa ndipo tunajiuliza kuwa kuna nini?, iweje kamati itoe taarifa siku tatu tu wakati ile ya Chenge mpaka leo Ipo kimya?.

Ukweli ni kwamba wanasiasa wa bongo wanavipa wakati mgumu sana vyombo vya dola kufanya kazi kitaalam. Kila kitu ni maagizo tu fanyeni hivi fanyeni vile. Yaani mwanasiasa huyohuyo, hakimu huyo huyo, polisi huyo huyo and everything.

Wao wanaona wanalinda maslahi yao lakini kwa undani zaidi wanaiangamiza nchi kwa kiasi kikubwa. Huwezi kuwa na double standards katika kushughulikia mambo ni kinyume kabisa na utawala wa sheria ni kama tunatawaliwa kiimla.

Yaani ili uwe salama jipendekeze kwa aliyeshika dola vinginevyo huna haki hivi, siku akishika dola mwingine aliyenyimwa haki leo unatarajia na yeye afanye nini?. tunakoenda si kuzuri kama tutaendelea kuwa na viongozi wabovu wa fikra kiasi hiki.

Kwa nini Tume iwe na kiherehere cha kutoa taarifa bila kuwa na all facts on the table?, huku ni kuua professionalism. Ninaamini kabisa kuwa kuna undue influence towards all conclusion reached in Mwakenyembe's accident.

Tubadilike muda bado tunao tuache kutumia vyombo vya dola kwa manufaa ya wachache tutalipeleka taifa pabaya.
Hofstede,

Nakubaliana na yote uliyoyandika kuhusu vyombo vya dola na double standards. Leo hii ningelikuwa mimi mtanzania nimepata ajali, hata kufika tu kwenye tukio ingewachukua masaa kama sio siku.

Wanasiasa pia lazima wakubali kufuata sheria na kuwajibika pale wanapokosea. Mtu unapoanza kulalamika lalamika hata kwenye ajali ambayo hata kwa mtu aliye mbali inaonekana wazi kama hii, unaweza kuleta madhara kwa jamii badala ya kujenga.

Watanzania walio wengi hawaendeshi magari; hata wale wanaoendesha wamejifunzia mitaani na hawajui sheria za barabarani. Ni rahisi mno kuwavuruga wananchi kwenye nchi ya namna hiyo. Ukiona hata wana JF ambao mimi naamini ni katika wajanja wa Tanzania hawajui hata maximum speed ni ngapi, unategemea wale vijana wa Manzese au kule Kyela watajua nini zaidi ya kuamini wanachosema viongozi wao?

Ushauri wangu kwa wengine ni kwamba hakuna haja ya kwenda speed ya zaidi ya 120k/h kwa TZ. Ukiamua kufanya hivyo ni risk ambayo uwe tayari kupokea madhara yake. haya mambo ya kila jambo kuna mkono wa mtu ni finyu mno hasa yanapotolewa na watu ambao wanajiita wasomi na wenye uelewo mkubwa. Viongozi wakiwa hivyo, kweli tutaweza kukomesha mila potofu kule wilayani?
 
Back
Top Bottom