Ajali mbaya ya Bodaboda

Ajali mbaya ya Bodaboda

Mshobaa

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2013
Posts
1,716
Reaction score
680
Ni magomeni mapipa ambapo imehusisha gari ya kampuni inayojenga barabara ya morogoro ya STRABAG kugonga muendesha pikipiki na kusababisha kifo chake palepale
 
picha ya nini mkuu!watu wanahangaika kuokoa we unataka picha kweli???
 
hii ni mojawapo ya changamoto ambazo hazitasahaulika katika ujenzi wa hii barabara,..
 
...ila madereva wa strabag ni wahuni sana(sio wote) maana siku moja walinifanyia uhuni wakizani na mimi ni mjinga flani ....
 
natoa pole kwa wafiwa, lakini sasa turudi kwenye ukweli, utii wa sheria bila shuruti kwa maana ya kufuata sheria za usalama barabarani, wenzetu wa bodaboda baadhi yao ama hawajui sheria au hawazingatii sheria za usalama barabarani, hili mimi binafsi nimekuwa nikishuhudia mara kwa mara, mimi nafikiri pamoja na kutoa pole kwa mwenzetu lakini tutumie mwanya huu kuwasisitizia wenye pikipiki kuheshimu sheria za usalama barabarani na pale ambapo yupo kwenye sheria lakini akaona gari inamfuata aipishe ili kuokoa maisha yake, mbona hata sisi wenye magari madogo unapoona kuna gari kubwa linakuja upande wako unalipisha kuokoa maisha yako na gari lako kitu ambacho madereva wengi wa bodaboda hawakifanyi.
 
natoa pole kwa wafiwa, lakini sasa turudi kwenye ukweli, utii wa sheria bila shuruti kwa maana ya kufuata sheria za usalama barabarani, wenzetu wa bodaboda baadhi yao ama hawajui sheria au hawazingatii sheria za usalama barabarani, hili mimi binafsi nimekuwa nikishuhudia mara kwa mara, mimi nafikiri pamoja na kutoa pole kwa mwenzetu lakini tutumie mwanya huu kuwasisitizia wenye pikipiki kuheshimu sheria za usalama barabarani na pale ambapo yupo kwenye sheria lakini akaona gari inamfuata aipishe ili kuokoa maisha yake, mbona hata sisi wenye magari madogo unapoona kuna gari kubwa linakuja upande wako unalipisha kuokoa maisha yako na gari lako kitu ambacho madereva wengi wa bodaboda hawakifanyi.

Lengo lako tujue kwamba unagari mwone kichwa chako
 
Ni magomeni mapipa ambapo imehusisha gari ya kampuni inayojenga barabara ya morogoro ya STRABAG kugonga muendesha pikipiki na kusababisha kifo chake palepale

OMG
Tumepoteza kura moja muhimu 2015!!
 
Back
Top Bottom