made
JF-Expert Member
- Jun 29, 2010
- 890
- 581
Jamani nimeandika kwa haraka lakini kuna ajali mbaya sana hapa Makongo imeua watu kadhaa,imehusisha gari kama tano hivi,daladala mbili.
==============
==============
WATU Sita wamekufa na wengine zaidi ya 12 kujeruhiwa katika ajali iliyotokea barabara ya kuelekea Bagamoyo eneo la Makongo, jijini Dar es Salaam, baada ya gari la abiria ‘daladala' iliyokuwa inatokea Tegeta kuelekea Mwenge kuacha njia na kugongana na daladala nyingine iliyokuwa ikitokea Mwenge kuelea Kunduchi.
Kamanda wa Polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni, Camillius Wambura, ameithibitishia FikraPevu kuwa tukio hilo limetokea Juni 21, 2014 saa Saba mchana na kuwa daladala iliyopata ajali inayofanya safari zake kati ya Tegeta Nyuki na Ubungo yenye namba T 441 CKT, imegongana na daladala nyingine inayofanya safari zake kati ya Makumbusho na Kunduchi yenye namba T 377 CKT mara baada ya kukosa mwelekeo.
Wambura, amesema ajali hiyo imehusisha magari matatu mara baada ya daladala hiyo kukosa mwelekeo, ambapo miili ya watu hao imehifadhiwa katika Hospitali ya Lugalo na majeruhi wamelazwa hospitalini hapo wakiendelea na matibabu huku dereva wa daladala iliyosababisha ajali hiyo akiwa anatafutwa baada ya kukimbilia mafichoni baada ya kusababisha ajali hiyo.
Kamanda wa kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Kamanda Awadhi Haji, amesema ajali hiyo imehusisha magari manne, moja likiwa ni la raia wa China, ambaye gari lake liliwakanyaga majeruhi na kuwaua sita kati yao.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Lugalo, ambapo maiti na majeruhi wamepelekwa Brigedia Jeneral, Josia Mekere, amethibitisha kupokea majeruhi 12, na maiti sita huku wengine hali zao zikiwa ni mbaya na kukimbizwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Mashuhuda wa ajali hiyo wamesema ajali hiyo imetokea wakati dereva wa gari la abiria ‘daladala' lilokuwa likielekea Mwenge kutokea Tegeta, kuwa katika mwendo kasi na kushindwa kulimuda hali iliyopelekea gari hilo kuhama barabara na kuingia katika upande wa pili na kusababisha ajali hiyo.
- See more at: http://www.fikrapevu.com/watu-6-wam...ajali-ya-barabarani-dar/#sthash.cVZdckCA.dpuf